Umri unasogea

rosemarie

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2011
Posts
6,887
Reaction score
3,420
Jamani umri wangu naona kama unasogea taratibu,nina miaka 42 lakini sijaoa bado,lakini niliishi na mwanamke miaka ya nyuma tukazaa lakini tulipoachana mpaka leo sijafikiria kuoa tena,lakini nahisi nimejiandaa kupambana na uzee peke yangu,kuna ushauri?
 
ona hapa Asha,


The Following User Says Thank You to Aisha Adam For This Useful Post:

Susy (Today)​
 

Ndugu
Hata ulivyojieleza ni matatizo matupu
Huyo uliyeishi na kuzaa nae ulimuoa?? Mliachana kwa sababu zipi, na wakati gani?? Au ulimpa mimba akiwa shule???
Sasa uzee utaishiji peke yako?? Ukiumwa nani wa kukupeleka hospital?? Ukistaafu nani wa kukutunza?? Au unafikiri pensheni haiishi???
Badilika bana, wanawake wamejaa kibao siku hizi.

Ila tahadhari! Sio vyote vin'gaavyo ni dhahabu.
Jaribu kumfahamu kwanza mwanamke kabla ya hatua yoyote.
 
Daah! mi nahisi unamatatizo mzee, hebu kawaone wataalamu kwani unaweza ukawa unajiona upo sawa kumbe unamatatizo
 

nitafute wa umri upi?hakuna kitu nachukia kama kupigiwa mkeo,nisije zeeka yeye bado anadai
 
nitafute wa umri upi?hakuna kitu nachukia kama kupigiwa mkeo,nisije zeeka yeye bado anadai

Ndugu
Swali lako tu linaonyesha HUNA NIA ya kuishi na mwenza.
Mwanaume wa miaka 42 aniulize kijana kama mimi (umenizidi miaka kumi na kitu) eti atafute mwanamke wa umri gani???
Si baadae utaniuliza na kabila kabisa.
Kuna wanawake wa miaka mpaka 55 hawajaolewa mpaka sasa, sembuse kijana wa miaka 42.

We bado kijana mdogo sana, hata uzee wala hukaribii ila sema mawazo yako tu ndo yanakuzeesha
 


mmh kwa staili ulivyojieleza utaishia kupokea maneno ya kukuvunja nguvu,we mbona ni mtu mzima kabisa unashindwa nini kujieleza vizuri na kuweka mambo wazi upate ushauri wa kukufaa hapahapa.acha kujieleza kama mtoto wa chekechea ili usaidiwe.
 
Tulia bado umri unaruhusu tafuta mwenye kukufaa ila kumbuka sio kila mwanamke ni mke, usije kurupuka ukaangukia koroma. Mwombe mungu akufungue na umpate mke mwema.


Ila kumbuka watoto ulionao ni wakwako na mke wako pia usiwasahau
 
Tulia bado umri unaruhusu tafuta mwenye kukufaa ila kumbuka sio kila mwanamke ni mke, usije kurupuka ukaangukia koroma. Mwombe mungu akufungue na umpate mke mwema.


Ila kumbuka watoto ulionao ni wakwako na mke wako pia usiwasahau

Hapo nilipo bold sio sawa mpendwa acha kumpotosha mwenzako 42yrs unasema umri bado unaruhusu? Na ili ampate mwanamke atayeendana nae kwa sasa ni kuanzia age ya 35 na kuendelea ambapo kwa sisi wanawake wa sasa mtu akifikia age hiyo hajapata mtoto inakuwa ni shida sana kumpata so sijui mtazamo wako lbd kama ataamua kuwa na mke lbd atakuwa wa kula nae raha tu.
 
umri ukifika hapo ni ngumu sana kuishi na mwanamke
 
CPU,umetoa ushauri wa hekima sana,isipokuwa tu kwenye hizo red,hayo mambo siku zote ndo huwa nayakataa,'kuoa kwa sababu ya....',hapa unaongelea kuoa kwa sababu ya kukwepa upweke uzeeni,kuwa na nesi wa uhakika,kutunzwa....jamani hizi ndizo SABABU za kuoa kweli? ina maana kama nina invest kwenye 'nursing home' nikalipia pesa kabisa wakati wa ujana wangu basi kwa msingi huu sitakuwa na sababu ya kuoa kwa sababu uzee wangu uko secured?
 
kwa umri huo tafuta agemate wako mana ukitaka dogodogo utapata presha na hivi 50 haipo mbali na wewe utazeeka mara mbili..
 
bishanga naomba wanilewe,sina tatizo lolote ila nahisi naona labda sio lazima kuoa thats all

Ndio kuao sio lazima ni maamuzi tu!!Kama unaona unapenda/taka/hitaji kufanya hivyo usisubirir mpaka mvi ziote na
kipara kikolee!Zaidi ya hapo kua tayari kuishi maisha ya upweke kwasababu huna mtu wa uhakika....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…