Umri wa kuishi aliosema Mungu mwenyewe kwa kinywa chake ni miaka 120. Kwanini mnakomaa na miaka ya tabu ya 70-80?

Umri wa kuishi aliosema Mungu mwenyewe kwa kinywa chake ni miaka 120. Kwanini mnakomaa na miaka ya tabu ya 70-80?

Morning_star

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2018
Posts
6,042
Reaction score
17,320
Mimi huwa nashangaa watumishi kuchukulia maneno ya Musa (Zaburi ya 90:10) na kuacha neno la Mungu mwenyewe la (Mwanzo 6:3) "Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini." (Yaani miaka 120)

Sasa watu wengi wakiongozwa na watumishi wa Mungu wamekomaa na Zaburi 90:10.

Ukitaka kujua maana ya huu mstari wa Zaburi 90:10, anzia kusoma mstari wa 5 hadi 12. Hapa anaongelea maisha ya mtu anayeishi katika dhambi, mateso na maangaiko huku hasira ya Mungu ikimkalia huwe na uhakika huwezi fikisha miaka 120. Lakini ukiishi kwa kufuata kanuni za kihistaarabu na kiungwana ukaachana na umalaya, pombe za kupindukia, vyakula visivyofaa, ukafanya mazoezi, ukaheshimu wazazi wako, ukatii mamlaka za nchi, ukatumia akili sawasawa ulizopewa na Mungu (maana wengi hatutumii hata 1% ya akili), ukamcha Bwana, ukajitenga na migogoro ya kuhamsha hasira za waliokuzunguka wasikuroge au kukudhuru, ni lazima utaishi hiyo miaka! Wachungaji semeni ukweli wa huu mstari wa Mwanzo 6;3. Miaka Mungu aliyotuhahidi ni 120 au angalau ukaribie! Wengi wanazima moto ndani ya miaka 70-80 kutokana na kuaminishwa na laana ya mdomo maana maneno yanaumba! Kataa hii laana! Sema mimi nitaishi miaka 120 aliyosema Mungu katika jina la Yesu!
 
Na kwanini Life span ina utofauti..., Kule Japan wanaishi zaidi na huku pengine vifo vya watoto ni vingi....; Hilo linapatikana wapi kwamba sehemu fulani wafe mapema na wengine wachelewe ?

Kuna kipindi cha hunters and gathers au kipindi cha vita na conquest life span ilikuwa about 30 to 40 years....

Moral of the Story..., Vifo / Kifo ni mikononi mwako ukicheza hata miaka 10 hauvuki
 
Kuna kosa lilifanywa miaka ikafupishwa, kwa wale wasomaji wa bibilia
Hii ni amri ya asili kabisa! Ukiwa mwizi lazima utakamatwa na kuuwawa! Ukidhurumu watu watakunenea mabaya, kukuua, au watakuroga, au utapata majanga na kufa kabla ya siku zako, ukifanya umalaya kuna magonjwa, kufumaniwa, matumizi mabaya ya fedha ambayo ingekulinda mwisho utakufa kabla ya siku zako. Tunaona viongozi vijana siku hizi wanapukutika! Wengi wanarogana na kutupiana majini, na wengi hutafuta nafasi hizo kwa wachawi na waganga na mizimu na ushirikina, na fitina na majungu, hivyo huwe na uhakika hutadumu utakufa siku sio zako.
 
Na kwanini Life span ina utofauti..., Kule Japan wanaishi zaidi na huku pengine vifo vya watoto ni vingi....; Hilo linapatikana wapi kwamba sehemu fulani wafe mapema na wengine wachelewe ?

Kuna kipindi cha hunters and gathers au kipindi cha vita na conquest life span ilikuwa about 30 to 40 years....

Moral of the Story..., Vifo / Kifo ni mikononi mwako ukicheza hata miaka 10 hauvuki
Uzuri mmoja hizi hadithi za biblia kuna risiti zake kabisa kuthibitisha ni stories tu😁
 
Hilo kosa Japan hawakufanya?
Ukitumia common sense ya akili uliyopewa na Mungu na ukaishi vizuri na mazingira (nature) ukahepuka migongano isiyo ya lazima na waliokuzunguka, ukazingatia lishe bora, kufanya mazoezi, kupumzika, kuachana na mambo ya kukuletea stress, ukazaa watoto utakaowamudu na kujipunguzia majukumu yasiyo ya lazima; nakuhakikishia miaka 120 unafika! Japan wanazingatia sana ushauri wangu huu!
 
Na kwanini Life span ina utofauti..., Kule Japan wanaishi zaidi na huku pengine vifo vya watoto ni vingi....; Hilo linapatikana wapi kwamba sehemu fulani wafe mapema na wengine wachelewe ?

Kuna kipindi cha hunters and gathers au kipindi cha vita na conquest life span ilikuwa about 30 to 40 years....

Moral of the Story..., Vifo / Kifo ni mikononi mwako ukicheza hata miaka 10 hauvuki
Mbona ameeleza pale kila kitu mkuu. Ametoa sababu zote pale juu.
 
Mbona ameeleza pale kila kitu mkuu. Ametoa sababu zote pale juu.
Sababu za nini za Afrika kuwa na Vifo vya watoto vingi..., na ni kipi kilichofanya sehemu kama Nagano Japan sasa hivi ndio among sehemu zenye highest life span ingawa kuna kipindi kabla ya Vita it was among the lowest..., walichofanya changing lifestyle...

Kama umri ungekuwa umepangwa kwa binadamu wote basi on average dunia nzima kungekuwa na same lifespan
 
Sababu za nini za Afrika kuwa na Vifo vya watoto vingi..., na ni kipi kilichofanya sehemu kama Nagano Japan sasa hivi ndio among sehemu zenye highest life span ingawa kuna kipindi kabla ya Vita it was among the lowest..., walichofanya changing lifestyle...

Kama umri ungekuwa umepangwa kwa binadamu wote basi on average dunia nzima kungekuwa na same lifespan
Unatumia akili nyingi kuelewa mambo yanayo hitaji imani. Amini kuna mambo ni siri hutokuja kuyaelewa.
 
Zaburi 90: 10 Siku za miaka yetu ni miaka sabini, Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini; Na kiburi chake ni taabu na ubatili, Maana chapita upesi tukatokomea mara.
 
Unatumia akili nyingi kuelewa mambo yanayo hitaji imani. Amini kuna mambo ni siri hutokuja kuya elewa.
Ukishaongelea Imani wala mimi siwezi kujadili.., takuwa chizi kujadili Imani yako hata kama unaamini kwamba haya maongezi hayapo bali upo ndotoni (huyo ni wewe)

LAKINI.., tunapoweka mambo katika majadiliano na unasema moja kujumlisha moja ni 3 lazima nikuulize kwanini isiwe mbili na kama kweli ni tatu kwanini nikitoa moja kwenye hiyo tatu nisibaki na moja nibakie na mbili ? Sababu huwezi kusema kwamba hapa ni hivi alafu baadae useme hapa ni vile (yaani unaanza na majibu alafu ndio unatunga maswali)
 
Kwa wengi wetu Kuishi miaka mingi ni mateso tu, kwanza usikute haya yote tunayo pambania tukiwa hai hayana maana yoyote
 
Mimi huwa nashangaa watumishi kuchukulia maneno ya Musa (Zaburi ya 90:10) na kuacha neno la Mungu mwenyewe la (Mwanzo 6:3) "Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini." (Yaani miaka 120)

Sasa watu wengi wakiongozwa na watumishi wa Mungu wamekomaa na Zaburi 90:10.

Ukitaka kujua maana ya huu mstari wa Zaburi 90:10, anzia kusoma mstari wa 5 hadi 12. Hapa anaongelea maisha ya mtu anayeishi katika dhambi, mateso na maangaiko huku hasira ya Mungu ikimkalia huwe na uhakika huwezi fikisha miaka 120. Lakini ukiishi kwa kufuata kanuni za kihistaarabu na kiungwana ukaachana na umalaya, pombe za kupindukia, vyakula visivyofaa, ukafanya mazoezi, ukaheshimu wazazi wako, ukatii mamlaka za nchi, ukatumia akili sawasawa ulizopewa na Mungu (maana wengi hatutumii hata 1% ya akili), ukamcha Bwana, ukajitenga na migogoro ya kuhamsha hasira za waliokuzunguka wasikuroge au kukudhuru, ni lazima utaishi hiyo miaka! Wachungaji semeni ukweli wa huu mstari wa Mwanzo 6;3. Miaka Mungu aliyotuhahidi ni 120 au angalau ukaribie! Wengi wanazima moto ndani ya miaka 70-80 kutokana na kuaminishwa na laana ya mdomo maana maneno yanaumba! Kataa hii laana! Sema mimi nitaishi miaka 120 aliyosema Mungu katika jina la Yesu!
Zaburi 90 iliandikwa wakati wa Musa wasomaji wa Biblia wanaelewa kwamba Zaburi haikuandikwa na Daudi pekee. Na inasemekana wakati huo Zaburi 90 ikiandikwa ndipo wakati ambao Mungu alichukizwa na kutoamini kwa waisraeli kwamba atawapa ushindi dhidi ya watu hodari na wenye nguvu kuliko wao.

Mungu alikasirika kwa sababu mpaka kufikia hapo alishawatendea miujiza mingi ikiwemo kutengeneza njia baharini, kwa hiyo akawaahidi ndani ya miaka 40 kizazi chote cha kuanzia miaka 20 kwenda juu lazima wafe kwanza ndipo waendelee na safari.
HESABU 32:11

Kwa hiyo Zaburi 90:10 ni kama maombolezo yao wakijua hawana siku nyingi za kuishi. Ukisoma mistari ya kabla ya hapo unaweza kupata muktadha huo nilioandika
 
Back
Top Bottom