Umuhimu wa chumvi enzi za Dola ya Warumi

Umuhimu wa chumvi enzi za Dola ya Warumi

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Chumvi ilikuwa na thamani kubwa sana katika utawala wa Warumi. Hakukua na umeme hivyo chumvi ilitumika kuhifadhia vyakula kama nyama na samaki. Kwa watu wa Pwani mnafahamu papa na ng’onda huu ni mfano wa vyakula vilivyo hifadhiwa na vilidumu kwa muda mrefu.

Chumvi iliitwa dhahabu nyeupe na ilitumika kulipia mishahara ya Askari. Neno salary limetokana na neno salarium kutoka katika lugha ya Latin ikimaanisha chumvi.

Warumi hawakuwa na umeme lakini walijenga majengo imara, barabara na madaraja. Siku yao ilianza saa 12 alfajiri. Walitumia vizuri mwanga wa mchana kufanya shughuli zao nyingi.

Kifungua kinywa ilikuwa ni glass ya maji, mchana wanaume walibeba mkate na cheese kula kazini. Siku ya kazi ikiisha saa nane mchana na walienda kuoga. Jioni ilikuwa ni sehemu muhimu kwao kwani walipumzika. Walicheza michezo wanayoipenda, walifanya mazungumzo ya biashara na pia walikula chakula cha jioni.

Chakula cha jioni kwa Warumi kilikuwa muhimu sana, walikaribisha marafiki na chakula kilikuwa na sehemu tatu. Wine na matunda ilikuw ni lazima kuwepo mezani. Hakukua na vijiko, umma na visu, walikula kwa mikono lakini walinawa mikono kabla na baada ya kula kila sehemu ya chakula.
 
Asante sana.

Nakumbuka hata wachina wakati wanaroute zao za silk road walikuwa wanatafuta sana chumvi katika biashara zao za nyumbani.

Na hata muvi maarufu ya historia yao ya Jumong imeweza weka historia hio, wakati kuna kabila la kibiashara pamoja na falme zilikuwa zikihangaika sana kutafuta chumvi.

Na haswaaa, chumvi ilikuwa kutunza vyakula. Hii ilikuwa kipindi kabla ya madini ya fedha kutengeneza fedha tuiitayo pesa leo. Pamoja na copper nafikiri.

Kazi kubwa ya chumvi ilikuwa kutunza mali zao ambazo bila kuhifadhiwa hueza kuoza kwa haraka, ambako kazi ya kuhifadhi mali ilikuja baadae kuchukuliwa na pesa.
 
Asante sana.

Nakumbuka hata wachina wakati wanaroute zao za silk road walikuwa wanatafuta sana chumvi katika biashara zao za nyumbani.

Na hata muvi maarufu ya historia yao ya Jumong imeweza weka historia hio, wakati kuna kabila la kibiashara pamoja na falme zilikuwa zikihangaika sana kutafuta chumvi.

Na haswaaa, chumvi ilikuwa kutunza vyakula. Hii ilikuwa kipindi kabla ya madini ya fedha kutengeneza fedha tuiitayo pesa leo. Pamoja na copper nafikiri.

Kazi kubwa ya chumvi ilikuwa kutunza mali zao ambazo bila kuhifadhiwa hueza kuoza kwa haraka, ambako kazi ya kuhifadhi mali ilikuja baadae kuchukuliwa na pesa.
GOOOOD
 
Back
Top Bottom