SoC02 Umuhimu wa kuwepo kituo cha sayansi ya anga nchini na jinsi kitakavyochochea maendeleo na mabadiliko ya uchumi wa taifa

SoC02 Umuhimu wa kuwepo kituo cha sayansi ya anga nchini na jinsi kitakavyochochea maendeleo na mabadiliko ya uchumi wa taifa

Stories of Change - 2022 Competition

Theorist Mosses

JF-Expert Member
Joined
Jul 16, 2022
Posts
345
Reaction score
253
FB_IMG_16585640961683505.jpg

(Pichani ni mwana anga Wa NASA)​

Utangulizi
maendeleo, ni hatua inayochukua nafasi kwenye kuboresha jambo na kuhakikisha jambo linakuja kufanikiwa kupiga hatua moja kwenda nyengine na kuleta mabadiliko na matokeo chanya.

Sayansi ya anga, ni miongoni mwanguzo kuu za maendeleo ambazo nchi nyingi zimejikita ndani yake katika teknolojia zikiwa na dhumuni la kujihimarisha kwenye nyanja zote ikiwemo kwenye elimu, siasa, kilimo, biashara pamoja na kijeshi nk.

INTERNATIONAL SPACE STATION (ISS). ni kituo kikuu cha kimataifa cha anga za mbali ambacho kilirushwa kwenye anga mnamo mwaka 1998. lengo likiwa ni kukuza teknolojia ya maisha ya mwanadamu, ambayo inaukubwa sawa na viwanja viwili vya mipira wa miguu. Ipo takribani umbali wa 400km kutoka usawa wa bahari kuelekea juu na muundo wake ni mita za eneo 110, times 100, times 30 kitu ambacho ni kikubwa sana. Kinaenda speed ya 7.66km/s au 28,000km/h huku ikitumia nishati ya solar pannel (nishati ya jua) ndani ikiwa na maabara, pamoja na mashamba ya mimea ambapo binadamu wanafanyia chunguzi na tafiti za kisayansi.
FB_IMG_16586085326174921.jpgFB_IMG_16586078985870972.jpg
(Pichani ni kituo cha anga cha kimataifa ISS)​

Tunapo zungumzia sayansi ya anga tuna maanisha nini, sayansi ni ujuzi, maarifa makubwa sana yaliyo jikita zaidi kwenye utafiti na uchunguzi ambapo ndani yake yanaongozwa na nadharia kuleta ubunifu na ugunduzi ili kurahisisha maisha.

Taifa letu ni miongoni mwanchi ndogo zilizo nyuma sana kimaendeleo na uchumi mdogo katika nyanja nyingi ikiwemo kwenye sayansi na teknolojia. Leo nitaeleza tatizo linalo tufanya tushindwe kimaendeleo pia nitaeleza ni namna gani kwamba nini kianze kufanyika ili taifa letu liweze kujikwamua kiuchumi kwenye nyanja zote.


Sababu za msingi kuhusu kueleza juu ya umuhimu wa taifa letu kujikita kwenye sayansi ni Kwasababu sayansi ya anga imehakisi maisha yetu halisi tunayoishi ya kila siku. asimilia 75% ndani ya taifa letu tunaendesha maisha yetu kwakutegemea maendeleo ya sayansi na teknolojia.

lakini teknolojia tunayo itegemea siyo ya kwetu lakini ni bora zaidi kuweka malengo ambayo na sisi kama taifa huru tuka jihusisha kwenye sayansi itakayo tuokoa kwenye majanga ya kushuka kwa uchumi, kupunguza kupanda kwa gharama za maisha na kupunguza hongezeko la njaa.

Sayansi na teknolojia ndani ya taifa letu kunadhana ambazo zinachochea kukwamisha mikakati madhubuti katika teknolojia ambazo taifa letu limekuwa halitoi kipaumbele kuanzia kwenye Elimu, utafiti, chunguzi na nadharia. naomba tuzungumzie nadharia ambayo ndiyo nyenzo kuu ya msingi wa sayansi kwamba inaumuhimu gani katika mabadiliko na kimaendeleo ya taifa letu kwenye sayansi na teknolojia.


Nadharia.
Ni uelewa au ubunifu wa juu sana ambao unatumika kwenye teknolojia kuelezea, kufundishia, kutengenezea, kutafitia vitu vingi ambavyo vinakuja kujikita zaidi kwenye ugunduzi, elimu, kilimo, siasa na teknolojia.

FB_IMG_16586083071562603.jpgFB_IMG_16586083184173734.jpgFB_IMG_16586083248875034.jpgFB_IMG_16586086152021605.jpgFB_IMG_16586085729392929.jpgFB_IMG_16586085875932903.jpg
(Pichani ni rocket inayoitwa starship imetengenezwa kwa nadharia na ubunifu)

Nadharia ndiyo nyenzo kuu kwenye sayansi na teknolojia iliyo hakisi maisha yetu halisi ambayo ni msingi wa maendeleo. Je, ni sababu zipi zinazo fanya taifa letu kushindwa kupiga hatua kwenye teknolojia ya sayansi na ipi ni njia bora ya kuinua teknolojia ndani ya taifa letu.


Vitu vinavyo changia kukwamisha maendeleo ya teknolojia ya sayansi hapa nchini.

• Taifa kuwa na wasomi wasio kuwa na vigezo kwenye sayansi na teknolojia. taifa kuwa na wasomi wasio kizi vigezo kuanzia walimu mpaka wanafunzi kwenye nafasi mbalimbali ni tatizo ambalo linachochea kujenga taifa lisilo kuwa na watu sahihi wenye ujuzi wa viwango vinavyo hitajika jambo ambalo linafanya taifa tushindwe kuendelea kwenye teknolojia.

• Taifa kuuwa vipaji vya vijana kwenye teknolojia. Ili ni pengo kubwa sana ambapo vijana wananyimwa haki zao za msingi wanapo jaribu kubuni au kugundua na kutengeneza chochote kinacho husiana na teknolojia ambapo kijana akitengeneza kitu basi mamlaka inamfungia kipaji chake asijihusishe na sayansi kitendo hiki kinachangia pia kupunguza kasi ya maendeleo katika taifa.

• Taifa kuwa na wasomi wasio wabunifu. Sisi kama taifa tunapo kuwa na wasomi ambao wasio na uwezo wa kugundua chochote au wakutengeneza hata vyombo vya usafiri ni tatizo kubwa linalo fanya taifa kushindwa kijukwamua kwenye teknolojia.

• Taifa kuwa na wasomi wengi wasio na malengo. Hili ni tatizo pale ambapo wasomi wanasoma tu bila kujiwekea malengo ambayo yangeweza kuchangia mchango mkubwa kwenye taifa kuhusu nyanja mbalimbali za maendeleo ili taifa liweze kujikwamua kiuchumi.

Vitu vitakavyo chochea maendeleo kwenye sayansi na teknolojia katika taifa letu

• Taifa kuwa na wataalam wenye malengo na ujuzi. Itasaidia sana kupiga hatua mbele kwenye suala zima la teknolojia ambapo taifa litanufaika kupitia kwa wataalam wenye malengo na maslahi bora kwaajiri ya kukuza uchumi wa taifa.

• Taifa kuhakikisha linaendeleza vipaji vya vijana. Nikitu ambacho kitasaidia sana kupunguza makundi mabaya ya vijana kama vile makundi ya kijambazi "panya road" kwamba taifa litakapo wasaidia vijana litakuza sayansi na teknolojia pia kwenye ajira.

• Taifa kuwa na wasomi wabunifu kwenye teknolojia. Itasaida taifa kupiga hatua kwenye sayansi na teknolojia ambapo wasomi watakuwa wakibuni vitu mbalimbali vitakavyo rahisisha maisha kwenye taifa itachochea kwenye uchumi.

• Taifa kuwa na kituo cha uchunguzi na tafiti za kisayansi. Hili pia ni nyenzo kuu itakayo saidia taifa kuendelea kiteknolojia na kupunguza gharama za maisha ambapo tutaweza kufanya safari ya anga za mbali na kutengeneza vitu vyetu wenyewe vikiwemo vyombo vya usafiri wa anga vitakavyo chochea uchumi na kukomesha kupanda kwa gharama za maisha ndani ya taifa.

Hitimisho
Tanzania kwenye sayansi na teknolojia inawezekana taifa bora zuri na imara hujengwa na watu wenyewe, lakini pia taifa bovu na baya hubomolewa na watu wenyewe.
FB_IMG_16586080130214760.jpg

(Pichani ni wana anga wa NASA wakiwa sambamba na kituo cha anga cha kimataifa ISS)





 
Upvote 18
Habari, kwa wageni wote jinsi ya kunipigia kura gusa kimshale hapa chini ya post chenye arama "^" chini ya chapisho.

Kama ukipata shida kwenye kupiga Kura Tafadhali nijulishe kwenye comment kwa maelekezo zaidi.

Tafadhali lakini pia usisahau Ku-like chapisho na kuacha maoni yako kuhusiana na sayansi na teknolojia pia nikaribisha mijadara.​
 
Ndugu yangu umeandika mambo mazuri. Hongera. Ila mimi Nina shida na haya mashitaka na lawama tunayoipa elimu yetu na wasomi wetu.

Hivi ni kweli kuwa Taifa letu lina elimu na wasomi wabovu kiasi cha kila mtu anayeandika au kusema juu ya maendeleo lazima abeze elimu yetu na wasomi wetu?

Kwa nijuavyo mimi, mifumo ya elimu ya nchi yetu inafanana na mifumo mingi ya nchi zilizotawaliwa na mwingereza ikiwemo India.

Lakini India iko juu sana kimaendeleo ya sayansi na teknolojia hata hiyo ya anga za juu. Mimi nafikiri kuna tatizo nje na mifumo ya elimu yetu na wasomi wetu. Au wewe unaonaje?
 
Ndugu yangu umeandika mambo mazuri. Hongera. Ila mimi Nina shida na haya mashitaka na lawama tunayoipa elimu yetu na wasomi wetu...​
Upo sahihi, swali zuri ni kwamba tunapo zungumzia maendeleo ya sayansi lazima tuwahusishe wataalam wetu na wasomi pamoja na serikali kwa sababu wao kwa nafasi kubwa ndiyo wahusika katika kuchochea maendeleo ya tasnia hii ya anga.

Moja ya maswali, ni kwamba kwanini tusitengeneze hata pikipiki zetu inamaana mainjinia walikuwa wanasomea nini vyuoni hapa ni lazima lawama zitabebwa na serikali na wasomi na jibu ni kwamba mainjia walio hitimu hawana ujuzi wowote kwenye kozi walizo somea.

Unajua hatuwezi kusema moja kwa moja kwamba elimu itolewayo hapa Tanzania aifai nazani elimu yetu inafundisha masomo darasani siyo kwa vitendo lakini mbona wapo watanzania walio somea masomo ya sayansi nje ya Tanzania bado wakawa hawana vigezo vinavyo itajika unazani lawama hata beba nani Kama siyo serikali na wasomi ?
 
Jinsi ya kunipigia kura angalia arama hii "^" chini kabisa ya post kibonyeze utakuwa ushanipigia kura.


Asante sana
 
Nimesoma hili andiko lakini nimeshindwa kuelewa.

Njoo Huku unieleweshe mambo machache.
1: Kituo Cha anga kitachochea je uchumi wa taifa?
2 :bajeti ya utafiti hadi kuwekeza kwenye kuunda vyombo vya kurushwa huko , nikiasi gani?
3 :ukiachana anga za mbali , je tumesha Fanya majaribio ya vyombo kama vya mawasiriano?
 
Swali zuri

Mimi nikujibu kwa swali ujawai kusikia kuna mtu katengeneza gari hapa Tanzania anaitwa "kipanya" kwani kutengeneza gari siyo sayansi hiyo Kama yeye ameweza kutengeneza gari. Je, taifa litashindwa kutengeneza hata baiskeli ?

Kama inawezekana na malighafi tunayo sasa tunapo fundisha watu masomo ya sayansi kwamba huyu amesomea chemistry, huyu physics, huyu hesabu sasa tunawafundisha hili waje kufanya nini ?

Shika Hiyo!!!!

Tunapo ongelea sayansi Tanzania tatizo siyo kwenye kuwekeza tatizo ni kwamba wasomi wakutengeneza rocket, magari, na baiskeli hawapo kwamba hawana ujuzi sijawai kusikia msomi wa Tanzania mwenye PhD zake ametengneza hata injini ya ndege alafu utasikia kuna kijana katengeneza injini kwani kijana ametumia bajeti gani ambayo serikali itashindwa.


je, sayansi inaweza kuchochea uchumi ? Jibu ni ndiyo


nisikupeleke huko kwenye kuwekeza njoo huku unajua nje ya sayansi kuna vitu Kama uchunguzi na tafiti pamoja na nadharia kwamba wanasayansi watakapo gundua nadharia mpya lazima tuite hiyo nadharia inakuwa ndiyo elimu sasa kutengeneza tu elimu yetu sindiyo uchumi huo sasa piga mwenyewe mahesabu kwenye kutoa elimu yetu wenyewe tutaingiza kiasi gani ? "wahenga wanasema elimu aiozi"


Swali lako limejijenga kwenye biashara ambapo hapa sisi tunazungumzia sayansi na siyo biashara ambayo umesema ni uwekezaji kwamba gharama za biashara za kununua ni za juu kuliko gharama za utengenezaji tulizo tengeneza wenyewe kwaiyo sayansi Tanzania inawezekana.

Mimi ni mwanasayansi na nimejifunza katika sayansi ni kwamba Mwanasayansi, hatakiwi kusema "hawezi"​
Haujajibu swali, kituo cha anga kinaongezaje uchumi WA nchi kama Tanzania? Mada yako yote haijaelezea hili na IPO kwenye title.
 
Mbona hapo juu mwanzoni mwapost nimezungumzia kuhusu suala la kukua kiuchumi na mifano ya kutosha.

Nikaja mpaka nikaeleza kuwa kwa asilimia flani watanzania tunategemea sayansi ya anga kwenye usafiri, mawasiliano pamoja na ajira.

Nikaja nikasema lakini hizi teknolojia tunazo zitegemea siyo za kwetu kwamba ni vyema na sisi tujiusishe nazo tutengeneze kituo chetu cha sayansi ya anga.

Mfano, Internet kwani Internet aichangii uchumi wa nchi Kama Tanzania unajua Internet inatumia mfumo wa wave (wireless) Kusambazwa kutoka kwenye mifumo kama satellite kwani hii siyo sayansi ya anga.



Hili ndiyo mdau umucyo lilimchanganya Lakini sikuchambua Sana kwamba lilikua ni jambo la kujiongeza tu.


Haujajibu swali, kituo cha anga kinaongezaje uchumi WA nchi kama Tanzania? Mada yako yote haijaelezea hili na IPO kwenye title.
 
Mbona hapo juu mwanzoni mwapost nimezungumzia kuhusu suala la kukua kiuchumi na mifano ya kutosha.

Nikaja mpaka nikaeleza kuwa kwa asilimia flani watanzania tunategemea sayansi ya anga kwenye usafiri, mawasiliano pamoja na ajira.

Nikaja nikasema lakini hizi teknolojia tunazo zitegemea siyo za kwetu kwamba ni vyema na sisi tujiusishe nazo tutengeneze kituo chetu cha sayansi ya anga.

Mfano, Internet kwani Internet aichangii uchumi wa nchi Kama Tanzania unajua Internet inatumia mfumo wa wave (wireless) Kusambazwa kutoka kwenye mifumo kama satellite kwani hii siyo sayansi ya anga.



Hili ndiyo mdau umucyo lilimchanganya Lakini sikuchambua Sana kwamba lilikua ni jambo la kujiongeza tu.
Unazungumzia kituo cha sayansi ya anga ukatoa mfano ISS Kwa maana unazungumzia space laboratory? Au mi ndio sijaelewa?
 
Sawa mtaalamu​
Ujaelewa ndiyo maana umeuliza naomba na mimi unieleweshe jambo moja.

Hivi ndege za Tanzania zinachangia kukua kwa uchumi ? Kwani wasomi na mainjinia hawapo walio somea uongozaji wa ndege mpaka tununue ?

Kwani kitu cha kutengeneza mwenyewe maabara na cha kununua kipi kina gharama kubwa ?


 
Habari, kwa wageni wote jinsi ya kunipigia kura gusa kimshale hapa chini ya post chenye arama "^" chini ya chapisho.

Kama ukipata shida kwenye kupiga Kura Tafadhali nijulishe kwenye comment kwa maelekezo zaidi.

Tafadhali lakini pia usisahau Ku-like chapisho na kuacha maoni yako kuhusiana na sayansi na teknolojia pia nikaribisha mijadara.
 
Habari, kwa wageni wote jinsi ya kunipigia kura gusa kimshale hapa chini ya post chenye arama "^" chini ya chapisho.

Kama ukipata shida kwenye kupiga Kura Tafadhali nijulishe kwenye comment kwa maelekezo zaidi.

Tafadhali lakini pia usisahau Ku-like chapisho na kuacha maoni yako kuhusiana na sayansi na teknolojia pia nikaribisha mijadara.
 
Habari, kwa wageni wote jinsi ya kunipigia kura gusa kimshale hapa chini ya post chenye arama "^" chini ya chapisho.

Kama ukipata shida kwenye kupiga Kura Tafadhali nijulishe kwenye comment kwa maelekezo zaidi.

Tafadhali lakini pia usisahau Ku-like chapisho na kuacha maoni yako kuhusiana na sayansi na teknolojia pia nikaribisha mijadara.
 
Habari, kwa wageni wote jinsi ya kunipigia kura gusa kimshale hapa chini ya post chenye arama "^" chini ya chapisho.

Kama ukipata shida kwenye kupiga Kura Tafadhali nijulishe kwenye comment kwa maelekezo zaidi.

Tafadhali lakini pia usisahau Ku-like chapisho na kuacha maoni yako kuhusiana na sayansi na teknolojia pia nikaribisha mijadara.
 
Habari, kwa wageni wote jinsi ya kunipigia kura gusa kimshale hapa chini ya post chenye arama "^" chini ya chapisho.

Kama ukipata shida kwenye kupiga Kura Tafadhali nijulishe kwenye comment kwa maelekezo zaidi.

Tafadhali lakini pia usisahau Ku-like chapisho na kuacha maoni yako kuhusiana na sayansi na teknolojia pia nikaribisha mijadara.
 
Habari, kwa wageni wote jinsi ya kunipigia kura gusa kimshale hapa chini ya post chenye arama "^" chini ya chapisho.

Kama ukipata shida kwenye kupiga Kura Tafadhali nijulishe kwenye comment kwa maelekezo zaidi.

Tafadhali lakini pia usisahau Ku-like chapisho na kuacha maoni yako kuhusiana na sayansi na teknolojia pia nikaribisha mijadara.
 
Back
Top Bottom