Umuhimu wa Sindano ya Anti D kwa wanawake wenye kundi negative la damu

Umuhimu wa Sindano ya Anti D kwa wanawake wenye kundi negative la damu

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Mwanamke mwenye kundi lolote la damu ambalo ni negative (A-, B-, AB- na O-) akipata ujauzito kutoka kwa mwanamme mwenye kundi la damu ambalo ni positive (A+, B+, AB+ au O+) mwili wake unaweza kutengeneza kinga mwili ambazo huwa ni hatari kwa ujauzito unaofuata.

Athari za kinga mwili hizi huanza kuonekana kwenye ujauzito wa pili na kuendelea ambapo humshambulia mtoto akiwa bado yupo tumboni na kumsababishia upungufu mkubwa wa damu, umanjano, kuharibika kwa ini pamoja na magonjwa ya moyo.

Mambo haya huwafanya watoto wafariki wakiwa tumboni au muda mchache baada ya kuzaliwa.

Ili kuondoa changamoto hizi, mwanamke mjamzito hupaswa kupata sindano yenye kinga (Anti D) kwenye wiki ya 28 ya ujauzito au ndani ya saa 72 baada ya kujifungua.

Ni muhimu kwa wachumba (wanandoa) kufahamu makundi yao ya damu kabla hawajaamua kupata ujauzito ili kujiandaa na changamoto za aina hii ambazo ni rahisi kuzikabili kabla hazijaleta madhara ya kudumu.

ACOG
 
Nina rafiki yangu, ni mjamzito kwa sasa lakini group lake la dam ni o- ila hajashauriwa chochote kuhusu hio sindano, mimi nimemdokeza tubkwa uelewa wangu nitamsomea hii mada inaweza msaidia huko alikoanza clinic akaulize maswali zaidi
 
Nina rafiki yangu, ni mjamzito kwa sasa lakini group lake la dam ni o- ila hajashauriwa chochote kuhusu hio sindano, mimi nimemdokeza tubkwa uelewa wangu nitamsomea hii mada inaweza msaidia huko alikoanza clinic akaulize maswali zaidi
Copy umtumie WhatsApp
 
Mwanamke mwenye kundi lolote la damu ambalo ni negative (A-, B-, AB- na O-) akipata ujauzito kutoka kwa mwanamme mwenye kundi la damu ambalo ni positive (A+, B+, AB+ au O+) mwili wake hutengeneza kinga mwili ambazo huwa ni hatari kwa ujauzito unaofuata.

Athari za kinga mwili hizi huanza kuonekana kwenye ujauzito wa pili na kuendelea ambapo humshambulia mtoto akiwa bado yupo tumboni na kumsababishia upungufu mkubwa wa damu, umanjano, kuharibika kwa ini pamoja na magonjwa ya moyo.

Mambo haya huwafanya watoto wanaofuata baada ya ujauzito wa kwanza wafariki wakiwa tumboni au muda mchache baada ya kuzaliwa.

Ili kuondoa changamoto hizi, mwanamke mjamzito hupaswa kupata sindano yenye kinga (Anti D) kwenye wiki ya 28 ya ujauzito au ndani ya saa 72 baada ya kujifungua.

Ni muhimu kwa wachumba (wanandoa) kufahamu makundi yao ya damu kabla hawajaamua kupata ujauzito ili kujiandaa na changamoto za aina hii ambazo ni rahisi kuzikabili kabla hazijaleta madhara ya kudumu.

NHS
Kinachonishangaza ni kwanini hii elimu hawaitoi ili watu wawe na uelewa.
 
Ukizaa na wanaume tofaui na wa kwanza ni A+, wa pili ni B+ mtoto wa pili atapata madhara?

Ndiyo, ni kwa group lolote A/B/AB/O -POSITIVE.

Kigezo ni mtoto akibeba group la baba ambapo ni POSITIVE.
 
Safi sana hii ki shule shule inaitwa... Hemolytic disease of new born...
 
Mimi niliinunua laki na nusu(150,000)

Ila miaka mi4 iliyopita na niliambiwa ghafla usiku na dokta,mzazi mwenzangu akiwa wodini anasubir kujifungua

Na dokta akaniambia ni lazma jitahidi uilete kesho tumpatie mgonjwa

Ukiinunua wanakuwekea kwenye barafu kabsa aisee nilijifunza mengi sana siku ile

Kumbe kuna watu huwa wanapoteza watoto wao au ujauzito kwa ajili ya hilo tatzo lakini wanahisi imani za kishirikina.
 
Mimi niliinunua laki na nusu(150,000)

Ila miaka mi4 iliyopita na niliambiwa ghafla usiku na dokta,mzazi mwenzangu akiwa wodini anasubir kujifungua

Na dokta akaniambia ni lazma jitahidi uilete kesho tumpatie mgonjwa

Ukiinunua wanakuwekea kwenye barafu kabsa aisee nilijifunza mengi sana siku ile

Kumbe kuna watu huwa wanapoteza watoto wao au ujauzito kwa ajili ya hilo tatzo lakini wanahisi imani za kishirikina.
Ni kweli kabisa vipi ilikuwa ujauzito wake wa ngapi shemeji ni wa kwanza au wa pili ndipo ilitakiwa hiyo sindano
 
Tatizo la hii sindano ni ghali sana,
Watu wengi wanashindwa kumudu, nadhani serikali ingeangalia namna ya kuwasaidia wazazi katika hili.
A single IVIG infusion can cost anywhere from $100 to over $350 or more per gram.
On average, the reported cost for IVIG treatment in the US is approximately $9,720, and if patients undergo 4 to 5 infusions per month, then it would cost them around $41,796 per month
 
Back
Top Bottom