UN kuchangisha dola bilioni moja za msaada kwa Ukraine

UN kuchangisha dola bilioni moja za msaada kwa Ukraine

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Umoja wa Mataifa (UN) unakusudia kuchangisha dola bilioni moja (Sh triloni 2.3) kwa kufadhili misaada ya kibinadamu kwa ajili ya Ukraine katika kipindi cha miezi mitatu ijayo.

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Martin Griffiths anayeshughlikia misaada ya kibinadamu, ameeleza hayo alipozungumza na waandishi habari.

Umoja wa Mataifa pia umesema unatenga haraka msaada wa dola milioni 20 kwa ajili ya Ukraine, umeeleza kuwa hata kabla ya Ukraine kuvamiwa na Urusi watu wapatao milioni tatu wa nchi hiyo tayari walikuwa wanahitaji misaada baada ya miaka kadhaa ya mapigano kati ya serikali ya Ukraine na waasi wa majimbo yaliyojitenga mashariki mwa nchi hiyo wanaoungwa mkono na Urusi.

Hata hivyo, Griffiths amesema viwango vya misaada kwa ajili ya Ukraine sasa vimeongezeka.



Source: DW
 
... Ukraine wanaonewa sana! The beginning of the end of Putin is now obvious.
 
Waweke namba ya M-pesa na mimi nichangie. Na bado Pope Francis kashatuagiza waumini wake tufunge (fasting) kwa ajili ya kuiombea Ukraine. Kuna mambo yatamgeukia Russia hadi atajiona boya.

By the way, ile dhuluma waliyomfanyia Dr.Shika haitawaacha salama.
 
Waweke namba ya M-pesa na mimi nichangie. Na bado Pope Francis kashatuagiza waumini wake tufunge (fasting) kwa ajili ya kuiombea Ukraine. Kuna mambo yatamgeukia Russia hadi atajiona boya.

By the way, ile dhuluma waliyomfanyia Dr.Shika haitawaacha salama.
Yemen, Syria uko watoto wanakufa kwa njaa, anza kuchangia uku kwanza kabla hujaifikiria Ukrane
 
...Russia haijawahi kuitawala Africa kwa Mabavu, hawajawahi kuiba rasilimali zetu, kutesa babu zetu na pia hawajawahi kuivamia Africa kwa vifaru na Mabomu kama NATO na Mataifa ya Ulaya. Napenda Demokrasia ila sipendi Demokrasia inayoenezwa kwa Mtutu wa Bunduki.

Sent from my SM-A022F using JamiiForums mobile app
 
Waweke namba ya M-pesa na mimi nichangie. Na bado Pope Francis kashatuagiza waumini wake tufunge (fasting) kwa ajili ya kuiombea Ukraine. Kuna mambo yatamgeukia Russia hadi atajiona boya.

By the way, ile dhuluma waliyomfanyia Dr.Shika haitawaacha salama.
Dua za kuku
 
Waweke namba ya M-pesa na mimi nichangie. Na bado Pope Francis kashatuagiza waumini wake tufunge (fasting) kwa ajili ya kuiombea Ukraine. Kuna mambo yatamgeukia Russia hadi atajiona boya.

By the way, ile dhuluma waliyomfanyia Dr.Shika haitawaacha salama.
Hao ni walewale tu, gadaf amepigwa mbona hakutoa agizo la kufunga
 
Back
Top Bottom