Methali 18:22 BHN
Anayempata mke amepata bahati njema; hiyo ni fadhili kutoka kwa Mwenyezi-Mungu.
Marko 10:9 BHN
Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asitenganishe.”
Methali 28:18 BHN
Aishiye kwa unyofu atasalimishwa, lakini mdanganyifu ataanguka kabisa.
Methali 6:32 BHN
Mwanamume anayezini na mke wa mtu hana akili kabisa; huyo hujiangamiza yeye mwenyewe.
2 Timotheo 2:22 BHN
Jiepushe na tamaa za ujana, fuata uadilifu, imani, upendo, amani, pamoja na watu wote ambao wanamwomba Bwana kwa moyo safi.