Unaamini katika uchawi? Tushirikishe uliyowahi kukumbana nayo

Unaamini katika uchawi? Tushirikishe uliyowahi kukumbana nayo

Da Vinci XV

JF-Expert Member
Joined
Dec 7, 2019
Posts
3,862
Reaction score
6,438
Do you believe In Witchcraft? Share you Experiences

Wasalaam,

Years ago in life movements, huko Songea katika harakati za msaka tonge, kama ilivyo silka ya Mwanaume kula kwa kutafuta Japo hata Tunda huliwa kimasihara lakini hutafutwa.

Binafsi yangu sijawahi kukumbana na Kioja chochote wala dhahama ya Uchawi Licha kutokea Tanga ambako kuna sifika kwa Uganga,Ulozi na Vioja vya Majini makata wa Subiani.

Zaidi zaidi nilipata kushuhudia tu wengine wakikumbana na dhahama na Ghilba chafu za Walozi, Binafsi ata kuchanjwa sikuwahi ,. nadhani ni kwasababu ya Taratibu na Miiko ya Nyumbani kwetu si vile Mwajua Tanga, nyumba sheikh, Nyumba Mganga, Nyumba Binti Mrembo basi hapa mimi nilitoka ile nyumba ya Masheikh kwetu Uchawi na Uganga ni Shiriki ,shiriki ambayo kesho kwa Allah kiama nitakosa msamaha wake wa kunisitiri katika Pepo na Neema Zake.

Tanga nlipata kushuhudia machache kama, siku moja nakumbuka nilipata kumwona Mama Mmoja ambaye alirogwa na Walozi mpaka akafikia hatua ya Kuwa kipofu hali hajiwezi basi mganguzi akawa anatoa uchafu kutoka katika macho yake (nlikuwa nashuhudia) hapa alitolewa vitu vingi machoni, yule mganga alikuwa anaweka mikono yake machoni na kufanya kama kuvuta kitu hivi.

Basi tuliona uchafu mwingi ukitoka ikiwemo Nyasi, Mabakuli, Vumbi, Mawe, Vipande vya Nguo, na Mifupa Just Imagine vyote vilitoka machoni mwa yule mama, na baada ya huduma hiyo maridhawa walao yule mama akaanza kuona japo kwa Tabu Tuliacha huduma Ikiendelea.

Tuachane na Hilo ambalo halikunikuta mimi

Wakati tunatia timu Songea, tulikuwa na Mission kama ya miezi 6 kama sio 7.
Mji huu umejaliwa watoto wazuri wa kingoni na hapa sikupata kumlaumu Msanii Nassibu Abdul alipopata kuwasifu katika ule wimbo wa "kwangwaru" alipopata kuwasifia kwa mjongeo wa viuno vyao, siku mbili tu baada ya kutia kambi hapo nikajiridhisha nalo hilo.

Kabla hata sijapata mahali pa kuishi kila ifikapo jioni nlikuwa siachi kutia timu , viwanja kama serengeti, krister park, La chaz na Vinginevyo kama hivyo na hapa ndipo nilipata wasaa wa kuwatazama vyema. Pongezi kwao.

Basi nlikuwa na Jamaa yangu ambae tulikuwa nae pamoja kwenye mission yetu, tulipata Nyumba Pale maeneo Mfaranyaki kwa wanaokufahamu.

Lakini siku chache tu baada ya kuanza, makazi katika nyumba hiyo tulianza kusikia Dodoso kadhaa kutoka kwa majirani haswa mama mmoja Muuza genge ambaye tulikuwa tunakwenda kununua mahitaji hapo kwa ajili ya madikodiko.

Hapa nami nikaanza kujiuliza Nyumba ile ina mpangaji mmoja tu ambaye alikuwa ni bidada afanyaye kazi benki Pale NMB Songea.
Na ilhali Vyumba vilikuwepo lakini havikupata wakazi na kwa maeneo yale ni ngumu kukosa mtu kwenye nyumba yenye kila mahitaji yote.

Nikaanza kufukua fukua fununu kutoka kwa yule dada kuna nini hapa, kwa hizi tetesi tusikiazo kuhusu hii nyumba. Alijibu kiutani utani kwamba kuna Maudhi madogo madogo ya kidunia ambayo hata hayana Madhara, kisha akatutoa hofu.

Hapa mimi na jamaa yangu tukajipa hope kama binti yule kaweza siye nani tushindwe na ukizingatia sisi watoto wa Tanga, japo imani yetu ilikuwa inajaribu kutufundisha kuwa ingawa binti yule kajinasibu pale labda huko kwao alikotoka aliaga vyema.

Basi ni kama wiki mbili au tatu baada ya kuhamia hapo, hatukukutana na Kisa chochote, Na mpaka wakati huo nilishaanza kupata washikaji kadhaa maana ilikuwa ni faradhi mimi kusakata kabumbu, pale Misufini shule ya Msingi wakati mwingi , ningepandisha mpaka kule uwanja wa Zimanimoto au kule Matarawe.

Na hapa wadau vijana niliozoeana nao pale uwanjani Misufini walishaanza kuniuliza masahibu tunayokumbana nayo lakini bado sikuwa na lolote la kuwajibu, Hatukukutana na lolote bado.

Jumamosi moja mimi na jamaa yangu ilikuwa tuchomoke ,job saa sita hivyo asubuhi tukakusanya Nguo zote chafu , na kuziacha uwani kwa Ajili ya kuja kufanyiwa Usafi Baadae tukirudi.

Hii siku tulitoka sote kwa pamoja nikimaanisha na yule dada ambaye tulikuwa naye mule ndani Pamoja, tukapanda gari ya Huyu binti, akatuacha eneo letu yeye akaendelea na ya kwake.

Mpaka Wakati tunarejea tukakuta hali ya Tofauti kidogo, zile nguo ambazo tuliacha pale zilikuwa zimefuliwa na kuanikwa vyema kwanzia mashuka, mpaka viatu sio hilo tu mpaka uwani na koridoni kulikuwa kumesafishwa vyema tofauti na Tulivyo acha hapa tukesema pengine yule dada kauvaa uhusika halisi wa kike kujishugulisha na yote hayo.

lakini haikuwa hivyo hii ni baada ya kufungua Chumba chetu, arrangement ilikuwa tofauti kabisaa, hapa tukabaki na viulizo

Mpaka wakati anarejea yule bidada tukampa informations ya yaliyojiri akaongeza yeye ashakutana nayo sana inafika muda hali inatulia na inafika muda, vioja vinaanza lakini Ashazoea.

Basi hapa kidogo uoga ukapungua, na kesho yake tu binti yule alikuja kututhibitisha hilo akaja kutuonyesha kwamba Asubuhi aliacha mchele na Mboga (samaki) aliooenda kanisani lakini aliporejea alikuta vimepikwa vyema na Nazi.

Basi zikakatika siku kadhaa usiku mmoja wakati natype data kadhaa za kazini kwenye PC, hapa haikuwa usiku mwingi ni kama saa 6 hivi huyu mwenzangu alikuwa Ashalala, mara nikaanza kusikia vishindo vya mtu akitembea koridoni kwa sauti viatu vya kike( highheels) hapa pengine uningedhani ni yule bidada lakini hali ilidumu mda mrefu sana.

Nikatuma SMS kwa yule dada kujua kwamba ni yeye au kama sio yeye anaskia akajibu vyema tu kwamba yuko macho na anaskia kila kitu, hapo mie nikatoka fasta kukodelea korido lakini sikuona chochote wala sauti hazikuwepo.

Sitaki kusema sikuwa na hofu ilikuwepo lakini sio kubwa na pengine kwakuwa nilishaandaliwa kisaikolojia ya kwamba walozi hao hawana madhara mengine zaidi ya usumbufu tu kama huo.

Baada ya kurejea ndani, ile kukaa tu mara taa ikaanza kujizima na kujiwasha yenyewe na huku sauti ya Socket switch ikisikika kama ilivyo kawaida, hapa nikamstua jamaa yangu ashuhudie kilichotokea mpaka tunalala hali ilikuwa hivyo , na asubuhi mambo yalikuwa kawaida.

Matukio yalikuwa mengi kila mtu akikutana na ya kwake kwa wakati wake kwanzia yule dada na sisi.

Nakumbuka wakati mmoja yule jamaa yangu alinihadithia kuwa alikutana na msichana, mmoja mrefu koridoni (sio yule dada tunaeishi nae)

akawa anaamuuliza

"We wanifahamu mimi"?

"Unaweza kunisaidia kubeba mizigo"?

Hapa jamaa angu alitimua mbio

Siku nyingine tena Mimi binafsi, nlikutana na mikono ya kike ikiwa imenishika isieleweke imetoka wapi yaani hapa mfano mtu awe amesimama halafu kutoka kwa nyuma mikono ije imshike mabegani niliona kucha zilizopakwa Rangi nyekundu nikagundua hilo kuwa ni ya kike.

Matukio yalikuwa mengi mno.

Muda mwingine tukiacha mboga tunakuta zishaandaliwa

Mara tusikie wanawake wakijadili na kucheka kwa sauti koridoni usiku

Mara upishane na wanawake muda wa kwenda chooni

Mara vitu vipite kwa kasi kama nyoka.

Hii nyumba ilikuwa ya don mmoja maarufu wa magari ya Mikoani (Songea to mikoani) inasemekana hapo ndiyo alikuwa ameweka vikolombwezi vyake humo hii ni kwa mujibu wa fununu za walimwengu wa Maeneo hayo.

Kwa wakazi wa maeneo yale watakuwa wanaijua hiyo skendo. Sijui kama hali inaendelea pale au laah kwa maana sisi bado tulimwacha yule Bidada na mara ya mwisho kuwasiliana nae akasema ashamishiwa Njombe.

Ushawahi kukutana na matukio ya ulozi/uchawi

Ilikuwaje?
 
bila blaa blaa nyingi kwani misaafu yetu inasemaje kuhusu uchawi na ulozi? upo haupo?
 
"Pepo na neema zake"

hebu fafanua hapa nimevutiwa napo

hizo neema za peponi ni zipi ambazo hazipo hapa duniani?
 
Uchawi umeandikwa kwenye biblia na miujiza ya Yesu kufufua watu na Musa kutenganisha bahari imeandikwa. Leo watu hawafufuliwi, wagonjwa hawaponi, wala bahari hazigawanywi. Nafikiri na uchawi upo useless namna hiyo.

Pia ukiona mambo mengine watu kuwa n wanaamini ni ya kichawi wakati yana explanations za kisayansi, inafanya nizidi kuamini kuwa uchawi ni useless na hauna effect yoyote. Watu waanaamini kuwa vichaa wengi wamerogwa, wanaamini kuwa mabusha yanatokana na uchawi, wanaamini kifafa kinatokana na uchawi na majini. Wanaamini utajiri wa uchawi. Hayw mambo yote yanafanya kuamini uchawi hauna effect yoyote kama ambavyo leo hakuna miujiza ile ya kibliblia
 
Do you believe In Witchcraft? Share you Experiences

Wasalaam,

Years Ago in Life movements, Huko songea katika harakati za msaka tonge , kama ilivyo silka ya Mwanaume kula kwa kutafuta Japo hata Tunda huliwa kimasihara lakini hutafutwa.

Binafsi yangu sijawahi kukumbana na Kioja chochote wala dhahama ya Uchawi Licha kutokea Tanga ambako kuna sifika kwa Uganga,Ulozi na Vioja vya Majini makata wa Subiani.

Zaidi zaidi nilipata kushuhudia tu wengine wakikumbana na dhahama na Ghilba chafu za Walozi, Binafsi ata kuchanjwa sikuwahi ,. nadhani ni kwasababu ya Taratibu na Miiko ya Nyumbani kwetu si vile Mwajua Tanga, nyumba sheikh, Nyumba Mganga, Nyumba Binti Mrembo basi hapa mimi nilitoka ile nyumba ya Masheikh kwetu Uchawi na Uganga ni Shiriki ,shiriki ambayo kesho kwa Allah kiama nitakosa msamaha wake wa kunisitiri katika Pepo na Neema Zake.

Tanga nlipata kushuhudia machache kama, siku moja nakumbuka nilipata kumwona Mama Mmoja ambaye alirogwa na Walozi mpaka akafikia hatua ya Kuwa kipofu hali hajiwezi basi mganguzi akawa anatoa uchafu kutoka katika macho yake (nlikuwa nashuhudia) hapa alitolewa vitu vingi machoni, yule mganga alikuwa anaweka mikono yake machoni na kufanya kama kuvuta kitu hivi.

Basi tuliona uchafu mwingi ukitoka ikiwemo Nyasi, Mabakuli, Vumbi, Mawe, Vipande vya Nguo, na Mifupa Just Imagine vyote vilitoka machoni mwa yule mama, na baada ya huduma hiyo maridhawa walao yule mama akaanza kuona japo kwa Tabu Tuliacha huduma Ikiendelea.

Tuachane na Hilo ambalo halikunikuta mimi

Wakati tunatia timu Songea, tulikuwa na Mission kama ya miezi 6 kama sio 7.
Mji huu umejaliwa watoto wazuri wa kingoni na hapa sikupata kumlaumu Msanii Nassibu Abdul alipopata kuwasifu katika ule wimbo wa "kwangwaru" alipopata kuwasifia kwa mjongeo wa viuno vyao, siku mbili tu baada ya kutia kambi hapo nikajiridhisha nalo hilo.

Kabla hata sijapata mahali pa kuishi kila ifikapo jioni nlikuwa siachi kutia timu , viwanja kama serengeti, krister park, La chaz na Vinginevyo kama hivyo na hapa ndipo nilipata wasaa wa kuwatazama vyema. Pongezi kwao.

Basi nlikuwa na Jamaa yangu ambae tulikuwa nae pamoja kwenye mission yetu, tulipata Nyumba Pale maeneo Mfaranyaki kwa wanaokufahamu.

Lakini siku chache tu baada ya kuanza ,makazi katika nyumba hiyo tulianza Kusikia Dodoso kadhaa kutoka kwa majirani haswa mama mmoja Muuza genge ambaye tulikuwa tunakwenda kununua mahitaji hapo kwa ajili ya madikodiko.

Hapa nami nikaanza kujiuliza Nyumba ile ina mpangaji mmoja tu Ambaye alikuwa ni bidada afanyaye kazi benki Pale NMB songea.
Na ilhali Vyumba vilikuwepo lakini havikupata wakazi na kwa maeneo yale ni ngumu kukosa mtu kwenye nyumba yenye kila mahitaji yote.

Nikaanza kufukua fukua fununu kutoka kwa yule dada kuna nini hapa, kwa hizi tetesi tusikiazo kuhusu hii nyumba. Alijibu kiutani utani kwamba kuna Maudhi madogo madogo ya Kidunia ambayo hata hayana Madhara., kisha akatutoa hofu.

Hapa mimi na jamaa yangu tukajipa hope kama binti yule kaweza siye nani tushindwe na ukizingatia sisi watoto wa Tanga, japo imani yetu ilikuwa inajaribu kutufundisha kuwa ingawa binti yule kajinasibu pale labda huko kwao alikotoka aliaga vyema.

Basi ni kama wiki mbili au tatu baada ya kuhamia hapo, hatukukutana na Kisa chochote, Na mpaka wakati huo nilishaanza kupata washikaji kadhaa maana ilikuwa ni faradhi mimi kusakata kabumbu, pale Misufini shule ya Msingi wakati mwingi , ningepandisha mpaka kule uwanja wa Zimanimoto au kule Matarawe.

Na hapa wadau vijana niliozoeana nao pale uwanjani Misufini walishaanza kuniuliza masahibu tunayokumbana nayo lakini bado sikuwa na lolote la kuwajibu, Hatukukutana na lolote bado.

Jumamosi moja mimi na jamaa yangu ilikuwa tuchomoke ,job saa sita hivyo asubuhi tukakusanya Nguo zote chafu , na kuziacha uwani kwa Ajili ya kuja kufanyiwa Usafi Baadae tukirudi.

Hii siku tulitoka sote kwa pamoja nikimaanisha na yule dada ambaye tulikuwa naye mule ndani Pamoja, tukapanda gari ya Huyu binti, akatuacha eneo letu yeye akaendelea na ya kwake.

Mpaka Wakati tunarejea tukakuta hali ya Tofauti kidogo, zile nguo ambazo tuliacha pale zilikuwa zimefuliwa na kuanikwa vyema kwanzia mashuka, mpaka viatu sio hilo tu mpaka uwani na koridoni kulikuwa kumesafishwa vyema tofauti na Tulivyo acha hapa tukesema pengine yule dada kauvaa uhusika halisi wa kike kujishugulisha na yote hayo.

lakini haikuwa hivyo hii ni baada ya kufungua Chumba chetu, arrangement ilikuwa tofauti kabisaa, hapa tukabaki na viulizo

Mpaka wakati anarejea yule bidada tukampa informations ya yaliyojiri akaongeza yeye ashakutana nayo sana inafika muda hali inatulia na inafika muda, vioja vinaanza lakini Ashazoea.

Basi hapa kidogo uoga ukapungua, na kesho yake tu binti yule alikuja kututhibitisha hilo akaja kutuonyesha kwamba Asubuhi aliacha mchele na Mboga (samaki) aliooenda kanisani lakini aliporejea alikuta vimepikwa vyema na Nazi.

Basi zikakatika siku kadhaa usiku mmoja wakati natype data kadhaa za kazini kwenye PC, hapa haikuwa usiku mwingi ni kama saa 6 hivi huyu mwenzangu alikuwa Ashalala , mara nikaanza kusikia vishindo vya mtu akitembea koridoni kwa sauti viatu vya kike( highheels) hapa pengine uningedhani ni yule bidada lakini hali ilidumu mda mrefu sana.

Nikatuma SMS kwa yule dada kujua kwamba ni yeye au kama sio yeye anaskia akajibu vyema tu kwamba yuko macho na anaskia kila kitu, hapo mie nikatoka fasta kukodelea korido lakini sikuona chochote wala sauti hazikuwepo.

Sitaki kusema sikuwa na hofu ilikuwepo lakini sio kubwa na pengine kwakuwa nilishaandaliwa kisaikolojia ya kwamba walozi hao hawana madhara mengine zaidi ya usumbufu tu kama huo.

Baada ya kurejea ndani, ile kukaa tu mara taa ikaanza kujizima na kujiwasha yenyewe na huku sauti ya Socket switch ikisikika kama ilivyo kawaida, hapa nikamstua jamaa yangu ashuhudie kilichotokea mpaka tunalala hali ilikuwa hivyo , na asubuhi mambo yalikuwa kawaida.

Matukio yalikuwa mengi kila mtu akikutana na ya kwake kwa wakati wake kwanzia yule dada na sisi.

Nakumbuka wakati mmoja yule jamaa yangu alinihadithia kuwa alikutana na msichana, mmoja mrefu koridoni (sio yule dada tunaeishi nae)

akawa anaamuuliza

"we wanifahamu mimi"?

"unaweza kunisaidia kubeba mizigo"?

Hapa jamaa angu alitimua mbio

Siku nyingine tena Mimi binafsi, nlikutana na mikono ya kike ikiwa imenishika isieleweke imetoka wapi yaani hapa mfano mtu awe amesimama halafu kutoka kwa nyuma mikono ije imshike mabegani niliona kucha zilizopakwa Rangi nyekundu nikagundua hilo kuwa ni ya kike.

Matukio yalikuwa mengi mno.

Muda mwingine tukiacha mboga tunakuta zishaandaliwa

Mara tusikie wanawake wakijadili na kucheka kwa sauti koridoni usiku

Mara upishane na wanawake muda wa kwenda chooni

Mara vitu vipite kwa kasi kama nyoka.

Hii nyumba ilikuwa ya don mmoja maarufu wa magari ya Mikoani ( songea to mikoani) inasemekana hapo ndiyo alikuwa ameweka vikolombwezi vyake humo hii ni kwa mujibu wa fununu za walimwengu wa Maeneo hayo.

Kwa wakazi wa maeneo yale watakuwa wanaijua hiyo skendo. Sijui kama hali inaendelea pale au laah kwa maana sisi bado tulimwacha yule Bidada na mara ya mwisho kuwasiliana nae akasema ashamishiwa Njombe.

Ushawahi kukutana na matukio ya ulozi/uchawi.

Ilikuwaje?
Asee mna roho ngumu
 
ukiona mambo mengine watu kuwa n wanaamini ni ya kichawi wakati yana explanations za kisayansi, inafanya nizidi kuamini kuwa uchawi ni useless na hauna effect yoyote.


Shetani ni mjanja kuliko unavyoweza kuzani na hicho ndicho kinachompa nguvu ya kuteka fahamu za watu. Na mtu yoyote akifanikiwa kuteka ufahamu wako ameweza kuku control
 
Nilishawahi kulipia gheto miez 6 mkoa ambao mm n mgeni na mtaa huo siujui vzuri kweny hyo nyumba ilionekana kama wanakaa watu ila sikuwahi kuwaona ila nlikua usik nkilala naskia wakiangalia Tv kucheka na kupiga stori.

Siku moja nimeenda kupigapiga stori na wana dukani maeneo ya karibu na nyumban ikabid niwaulize hiv watu wanao ishi kwenye ile nyumba ninayo ish mm wanafanya kaz gan maana sijawahi kuonana nao huwa wanakuja usk baada ya mm kufka na asubuh soon dalili ya wao kuwepo

Jamaa wakaniambia kwenye hyo nyumba hakuna mtu anaeishi ila Ni mimi tu ndo huwa wananiona naingia na kutoka, aah nikawapuuza nikajua hata wao hawajui chochote

ila siku zilivyoenda niliona mauzauza flan ikabidi nihame na nisamehe kodi yote
Aiseee haya mambo yapo , bwanah
 
Kuna mzee mmoja alikua ni rafiki sana na mshua, huyu mzee alikua muuzaji wa magogo ya mbao, hua anaenda bush mwenyewe na kukata kisha kuja kuyauza mjini.

Huyu mzee biashara hii alikua akiifanya kimagendo kwasababu hakua na vibali vya serikali

Sasa siku moja wakati ameyabeba kwenye gari yake akiwa bush anayasafirisha kuja nayo mjini, kama mkosi ghafla mamwela nao hao wanamfukuza

Yule mzee akakimbiza gari yake mpaka kijijini kwao kisha akafunga break wale mamwela waliokua wanamfukuza wakasimama wakasema mzee hii gari pamoja na huu mzigo vinqpelekwa polisi.

Yule mzee akawaambia "haina shida hapa ndo nyumbani walilozika kitovu changu na gari yangu ipo katika usalama"

Wale mamwela wakawa wanapakua yale magogo na kuyaamishia kwenye gari lao, mzee alichokifanya ye akawa anachota mchanga kwenye taili za lile gari la polisi. Akatoka hapo akazoa tena mchanga ulioko kwenye taili za gari lake kisha akasema "haya vijana muwe na siku njema gari yangu hapo ipo kwenye usalama mi naondoka tutakutana hapo polisi"

Wale mapolisi wakasema "we mzee unatutishia uchawi unafikiri si tunaogopa"?

Mzew akawajibu akasema "hapana watawala na wakubwa zangu yanj neno dogo tu mnataka kulifanya kubwa, mi nimewaambia tu gari yangu ipo salama basi"

Mamwela wakampotezea wakafanya kilichowaleta kisha wakatambaa

Baada ya hapo miezi kadhaa ikapita

Sasa siku moja dingi yangu alikua anamginjwa hospitali, wakati ameenda kumtembelea akastuka kusikia sauti ya mtu ambaye alionekana akiita kwa shida sana, ndipo alipogeuka na kuona kuna mgonjwa kutoka kitanda cha nyuma kabisa ya wodi akinyoosha mkono ishara ya kuita

Aliposogea ndo akapata mshangao kua ni polisi wa misitu ndo alikua anamuita afu yupo katika condition mbaya sana. Yule polisi akamuambia mzee "samahani mzee nakuomba sana kaniombee msamaha kwa rafiki yako"

Mzee naye haamini uchawi akauliza "msahama wa nini kwani kakufanyia nini"?

Polisi akasema "nilipokua namkamata na kumpola magogo alikua anazoa mchanga naamini yeye ndio kanipa huu ugonjwa nakuomba ukaniombee msamaha"

Mzee hakutaka maneno mengi kwasababu aliona kumuongelesha na kumuuliza maswali ni kuzidi kumpa mateso mgonjwa kutokana na uongeaji wake kua wa shida na kuonesha kua yuko kwenye maumivu makali, so akamjibu sawa nitafanya hivyo

Sasa karudi kwa rafiki yake anampa habari kua yule poti aliyekukamata nimemkuta hospitali, 'naye huyu mzee akawa anastaajabu'

Mzee akamuambia rafiki yake kua yule poti "anakuomba msamaha" yule mzee akasema "jamani sio mimi itakua ni wengine wamemfanyia maana kawaudhi wengi, mi nilifanya vile kuwatisha tu nikiwa najua wataniachia mzigo wangu"

Yule mgonjwa alipoona hali inazidi kua mbaya akatuma na wazee waende kumuomba msamaha lakini jibu la yule mzee lilikua ni lile lile kua hausiki na yeye alifanya vile kwa kuwatisha tu wala si kivingine

Baada ya siku kadhaa yule mgonjwa akafariki
 
Do you believe In Witchcraft? Share you Experiences

Wasalaam,

Years ago in life movements, huko Songea katika harakati za msaka tonge, kama ilivyo silka ya Mwanaume kula kwa kutafuta Japo hata Tunda huliwa kimasihara lakini hutafutwa.

Binafsi yangu sijawahi kukumbana na Kioja chochote wala dhahama ya Uchawi Licha kutokea Tanga ambako kuna sifika kwa Uganga,Ulozi na Vioja vya Majini makata wa Subiani.

Zaidi zaidi nilipata kushuhudia tu wengine wakikumbana na dhahama na Ghilba chafu za Walozi, Binafsi ata kuchanjwa sikuwahi ,. nadhani ni kwasababu ya Taratibu na Miiko ya Nyumbani kwetu si vile Mwajua Tanga, nyumba sheikh, Nyumba Mganga, Nyumba Binti Mrembo basi hapa mimi nilitoka ile nyumba ya Masheikh kwetu Uchawi na Uganga ni Shiriki ,shiriki ambayo kesho kwa Allah kiama nitakosa msamaha wake wa kunisitiri katika Pepo na Neema Zake.

Tanga nlipata kushuhudia machache kama, siku moja nakumbuka nilipata kumwona Mama Mmoja ambaye alirogwa na Walozi mpaka akafikia hatua ya Kuwa kipofu hali hajiwezi basi mganguzi akawa anatoa uchafu kutoka katika macho yake (nlikuwa nashuhudia) hapa alitolewa vitu vingi machoni, yule mganga alikuwa anaweka mikono yake machoni na kufanya kama kuvuta kitu hivi.

Basi tuliona uchafu mwingi ukitoka ikiwemo Nyasi, Mabakuli, Vumbi, Mawe, Vipande vya Nguo, na Mifupa Just Imagine vyote vilitoka machoni mwa yule mama, na baada ya huduma hiyo maridhawa walao yule mama akaanza kuona japo kwa Tabu Tuliacha huduma Ikiendelea.

Tuachane na Hilo ambalo halikunikuta mimi

Wakati tunatia timu Songea, tulikuwa na Mission kama ya miezi 6 kama sio 7.
Mji huu umejaliwa watoto wazuri wa kingoni na hapa sikupata kumlaumu Msanii Nassibu Abdul alipopata kuwasifu katika ule wimbo wa "kwangwaru" alipopata kuwasifia kwa mjongeo wa viuno vyao, siku mbili tu baada ya kutia kambi hapo nikajiridhisha nalo hilo.

Kabla hata sijapata mahali pa kuishi kila ifikapo jioni nlikuwa siachi kutia timu , viwanja kama serengeti, krister park, La chaz na Vinginevyo kama hivyo na hapa ndipo nilipata wasaa wa kuwatazama vyema. Pongezi kwao.

Basi nlikuwa na Jamaa yangu ambae tulikuwa nae pamoja kwenye mission yetu, tulipata Nyumba Pale maeneo Mfaranyaki kwa wanaokufahamu.

Lakini siku chache tu baada ya kuanza, makazi katika nyumba hiyo tulianza kusikia Dodoso kadhaa kutoka kwa majirani haswa mama mmoja Muuza genge ambaye tulikuwa tunakwenda kununua mahitaji hapo kwa ajili ya madikodiko.

Hapa nami nikaanza kujiuliza Nyumba ile ina mpangaji mmoja tu ambaye alikuwa ni bidada afanyaye kazi benki Pale NMB Songea.
Na ilhali Vyumba vilikuwepo lakini havikupata wakazi na kwa maeneo yale ni ngumu kukosa mtu kwenye nyumba yenye kila mahitaji yote.

Nikaanza kufukua fukua fununu kutoka kwa yule dada kuna nini hapa, kwa hizi tetesi tusikiazo kuhusu hii nyumba. Alijibu kiutani utani kwamba kuna Maudhi madogo madogo ya kidunia ambayo hata hayana Madhara, kisha akatutoa hofu.

Hapa mimi na jamaa yangu tukajipa hope kama binti yule kaweza siye nani tushindwe na ukizingatia sisi watoto wa Tanga, japo imani yetu ilikuwa inajaribu kutufundisha kuwa ingawa binti yule kajinasibu pale labda huko kwao alikotoka aliaga vyema.

Basi ni kama wiki mbili au tatu baada ya kuhamia hapo, hatukukutana na Kisa chochote, Na mpaka wakati huo nilishaanza kupata washikaji kadhaa maana ilikuwa ni faradhi mimi kusakata kabumbu, pale Misufini shule ya Msingi wakati mwingi , ningepandisha mpaka kule uwanja wa Zimanimoto au kule Matarawe.

Na hapa wadau vijana niliozoeana nao pale uwanjani Misufini walishaanza kuniuliza masahibu tunayokumbana nayo lakini bado sikuwa na lolote la kuwajibu, Hatukukutana na lolote bado.

Jumamosi moja mimi na jamaa yangu ilikuwa tuchomoke ,job saa sita hivyo asubuhi tukakusanya Nguo zote chafu , na kuziacha uwani kwa Ajili ya kuja kufanyiwa Usafi Baadae tukirudi.

Hii siku tulitoka sote kwa pamoja nikimaanisha na yule dada ambaye tulikuwa naye mule ndani Pamoja, tukapanda gari ya Huyu binti, akatuacha eneo letu yeye akaendelea na ya kwake.

Mpaka Wakati tunarejea tukakuta hali ya Tofauti kidogo, zile nguo ambazo tuliacha pale zilikuwa zimefuliwa na kuanikwa vyema kwanzia mashuka, mpaka viatu sio hilo tu mpaka uwani na koridoni kulikuwa kumesafishwa vyema tofauti na Tulivyo acha hapa tukesema pengine yule dada kauvaa uhusika halisi wa kike kujishugulisha na yote hayo.

lakini haikuwa hivyo hii ni baada ya kufungua Chumba chetu, arrangement ilikuwa tofauti kabisaa, hapa tukabaki na viulizo

Mpaka wakati anarejea yule bidada tukampa informations ya yaliyojiri akaongeza yeye ashakutana nayo sana inafika muda hali inatulia na inafika muda, vioja vinaanza lakini Ashazoea.

Basi hapa kidogo uoga ukapungua, na kesho yake tu binti yule alikuja kututhibitisha hilo akaja kutuonyesha kwamba Asubuhi aliacha mchele na Mboga (samaki) aliooenda kanisani lakini aliporejea alikuta vimepikwa vyema na Nazi.

Basi zikakatika siku kadhaa usiku mmoja wakati natype data kadhaa za kazini kwenye PC, hapa haikuwa usiku mwingi ni kama saa 6 hivi huyu mwenzangu alikuwa Ashalala, mara nikaanza kusikia vishindo vya mtu akitembea koridoni kwa sauti viatu vya kike( highheels) hapa pengine uningedhani ni yule bidada lakini hali ilidumu mda mrefu sana.

Nikatuma SMS kwa yule dada kujua kwamba ni yeye au kama sio yeye anaskia akajibu vyema tu kwamba yuko macho na anaskia kila kitu, hapo mie nikatoka fasta kukodelea korido lakini sikuona chochote wala sauti hazikuwepo.

Sitaki kusema sikuwa na hofu ilikuwepo lakini sio kubwa na pengine kwakuwa nilishaandaliwa kisaikolojia ya kwamba walozi hao hawana madhara mengine zaidi ya usumbufu tu kama huo.

Baada ya kurejea ndani, ile kukaa tu mara taa ikaanza kujizima na kujiwasha yenyewe na huku sauti ya Socket switch ikisikika kama ilivyo kawaida, hapa nikamstua jamaa yangu ashuhudie kilichotokea mpaka tunalala hali ilikuwa hivyo , na asubuhi mambo yalikuwa kawaida.

Matukio yalikuwa mengi kila mtu akikutana na ya kwake kwa wakati wake kwanzia yule dada na sisi.

Nakumbuka wakati mmoja yule jamaa yangu alinihadithia kuwa alikutana na msichana, mmoja mrefu koridoni (sio yule dada tunaeishi nae)

akawa anaamuuliza

"We wanifahamu mimi"?

"Unaweza kunisaidia kubeba mizigo"?

Hapa jamaa angu alitimua mbio

Siku nyingine tena Mimi binafsi, nlikutana na mikono ya kike ikiwa imenishika isieleweke imetoka wapi yaani hapa mfano mtu awe amesimama halafu kutoka kwa nyuma mikono ije imshike mabegani niliona kucha zilizopakwa Rangi nyekundu nikagundua hilo kuwa ni ya kike.

Matukio yalikuwa mengi mno.

Muda mwingine tukiacha mboga tunakuta zishaandaliwa

Mara tusikie wanawake wakijadili na kucheka kwa sauti koridoni usiku

Mara upishane na wanawake muda wa kwenda chooni

Mara vitu vipite kwa kasi kama nyoka.

Hii nyumba ilikuwa ya don mmoja maarufu wa magari ya Mikoani (Songea to mikoani) inasemekana hapo ndiyo alikuwa ameweka vikolombwezi vyake humo hii ni kwa mujibu wa fununu za walimwengu wa Maeneo hayo.

Kwa wakazi wa maeneo yale watakuwa wanaijua hiyo skendo. Sijui kama hali inaendelea pale au laah kwa maana sisi bado tulimwacha yule Bidada na mara ya mwisho kuwasiliana nae akasema ashamishiwa Njombe.

Ushawahi kukutana na matukio ya ulozi/uchawi

Ilikuwaje?
hiyo misosi iliyopikwa na jini mlikuwa mnakula au......
Do you believe In Witchcraft? Share you Experiences

Wasalaam,

Years ago in life movements, huko Songea katika harakati za msaka tonge, kama ilivyo silka ya Mwanaume kula kwa kutafuta Japo hata Tunda huliwa kimasihara lakini hutafutwa.

Binafsi yangu sijawahi kukumbana na Kioja chochote wala dhahama ya Uchawi Licha kutokea Tanga ambako kuna sifika kwa Uganga,Ulozi na Vioja vya Majini makata wa Subiani.

Zaidi zaidi nilipata kushuhudia tu wengine wakikumbana na dhahama na Ghilba chafu za Walozi, Binafsi ata kuchanjwa sikuwahi ,. nadhani ni kwasababu ya Taratibu na Miiko ya Nyumbani kwetu si vile Mwajua Tanga, nyumba sheikh, Nyumba Mganga, Nyumba Binti Mrembo basi hapa mimi nilitoka ile nyumba ya Masheikh kwetu Uchawi na Uganga ni Shiriki ,shiriki ambayo kesho kwa Allah kiama nitakosa msamaha wake wa kunisitiri katika Pepo na Neema Zake.

Tanga nlipata kushuhudia machache kama, siku moja nakumbuka nilipata kumwona Mama Mmoja ambaye alirogwa na Walozi mpaka akafikia hatua ya Kuwa kipofu hali hajiwezi basi mganguzi akawa anatoa uchafu kutoka katika macho yake (nlikuwa nashuhudia) hapa alitolewa vitu vingi machoni, yule mganga alikuwa anaweka mikono yake machoni na kufanya kama kuvuta kitu hivi.

Basi tuliona uchafu mwingi ukitoka ikiwemo Nyasi, Mabakuli, Vumbi, Mawe, Vipande vya Nguo, na Mifupa Just Imagine vyote vilitoka machoni mwa yule mama, na baada ya huduma hiyo maridhawa walao yule mama akaanza kuona japo kwa Tabu Tuliacha huduma Ikiendelea.

Tuachane na Hilo ambalo halikunikuta mimi

Wakati tunatia timu Songea, tulikuwa na Mission kama ya miezi 6 kama sio 7.
Mji huu umejaliwa watoto wazuri wa kingoni na hapa sikupata kumlaumu Msanii Nassibu Abdul alipopata kuwasifu katika ule wimbo wa "kwangwaru" alipopata kuwasifia kwa mjongeo wa viuno vyao, siku mbili tu baada ya kutia kambi hapo nikajiridhisha nalo hilo.

Kabla hata sijapata mahali pa kuishi kila ifikapo jioni nlikuwa siachi kutia timu , viwanja kama serengeti, krister park, La chaz na Vinginevyo kama hivyo na hapa ndipo nilipata wasaa wa kuwatazama vyema. Pongezi kwao.

Basi nlikuwa na Jamaa yangu ambae tulikuwa nae pamoja kwenye mission yetu, tulipata Nyumba Pale maeneo Mfaranyaki kwa wanaokufahamu.

Lakini siku chache tu baada ya kuanza, makazi katika nyumba hiyo tulianza kusikia Dodoso kadhaa kutoka kwa majirani haswa mama mmoja Muuza genge ambaye tulikuwa tunakwenda kununua mahitaji hapo kwa ajili ya madikodiko.

Hapa nami nikaanza kujiuliza Nyumba ile ina mpangaji mmoja tu ambaye alikuwa ni bidada afanyaye kazi benki Pale NMB Songea.
Na ilhali Vyumba vilikuwepo lakini havikupata wakazi na kwa maeneo yale ni ngumu kukosa mtu kwenye nyumba yenye kila mahitaji yote.

Nikaanza kufukua fukua fununu kutoka kwa yule dada kuna nini hapa, kwa hizi tetesi tusikiazo kuhusu hii nyumba. Alijibu kiutani utani kwamba kuna Maudhi madogo madogo ya kidunia ambayo hata hayana Madhara, kisha akatutoa hofu.

Hapa mimi na jamaa yangu tukajipa hope kama binti yule kaweza siye nani tushindwe na ukizingatia sisi watoto wa Tanga, japo imani yetu ilikuwa inajaribu kutufundisha kuwa ingawa binti yule kajinasibu pale labda huko kwao alikotoka aliaga vyema.

Basi ni kama wiki mbili au tatu baada ya kuhamia hapo, hatukukutana na Kisa chochote, Na mpaka wakati huo nilishaanza kupata washikaji kadhaa maana ilikuwa ni faradhi mimi kusakata kabumbu, pale Misufini shule ya Msingi wakati mwingi , ningepandisha mpaka kule uwanja wa Zimanimoto au kule Matarawe.

Na hapa wadau vijana niliozoeana nao pale uwanjani Misufini walishaanza kuniuliza masahibu tunayokumbana nayo lakini bado sikuwa na lolote la kuwajibu, Hatukukutana na lolote bado.

Jumamosi moja mimi na jamaa yangu ilikuwa tuchomoke ,job saa sita hivyo asubuhi tukakusanya Nguo zote chafu , na kuziacha uwani kwa Ajili ya kuja kufanyiwa Usafi Baadae tukirudi.

Hii siku tulitoka sote kwa pamoja nikimaanisha na yule dada ambaye tulikuwa naye mule ndani Pamoja, tukapanda gari ya Huyu binti, akatuacha eneo letu yeye akaendelea na ya kwake.

Mpaka Wakati tunarejea tukakuta hali ya Tofauti kidogo, zile nguo ambazo tuliacha pale zilikuwa zimefuliwa na kuanikwa vyema kwanzia mashuka, mpaka viatu sio hilo tu mpaka uwani na koridoni kulikuwa kumesafishwa vyema tofauti na Tulivyo acha hapa tukesema pengine yule dada kauvaa uhusika halisi wa kike kujishugulisha na yote hayo.

lakini haikuwa hivyo hii ni baada ya kufungua Chumba chetu, arrangement ilikuwa tofauti kabisaa, hapa tukabaki na viulizo

Mpaka wakati anarejea yule bidada tukampa informations ya yaliyojiri akaongeza yeye ashakutana nayo sana inafika muda hali inatulia na inafika muda, vioja vinaanza lakini Ashazoea.

Basi hapa kidogo uoga ukapungua, na kesho yake tu binti yule alikuja kututhibitisha hilo akaja kutuonyesha kwamba Asubuhi aliacha mchele na Mboga (samaki) aliooenda kanisani lakini aliporejea alikuta vimepikwa vyema na Nazi.

Basi zikakatika siku kadhaa usiku mmoja wakati natype data kadhaa za kazini kwenye PC, hapa haikuwa usiku mwingi ni kama saa 6 hivi huyu mwenzangu alikuwa Ashalala, mara nikaanza kusikia vishindo vya mtu akitembea koridoni kwa sauti viatu vya kike( highheels) hapa pengine uningedhani ni yule bidada lakini hali ilidumu mda mrefu sana.

Nikatuma SMS kwa yule dada kujua kwamba ni yeye au kama sio yeye anaskia akajibu vyema tu kwamba yuko macho na anaskia kila kitu, hapo mie nikatoka fasta kukodelea korido lakini sikuona chochote wala sauti hazikuwepo.

Sitaki kusema sikuwa na hofu ilikuwepo lakini sio kubwa na pengine kwakuwa nilishaandaliwa kisaikolojia ya kwamba walozi hao hawana madhara mengine zaidi ya usumbufu tu kama huo.

Baada ya kurejea ndani, ile kukaa tu mara taa ikaanza kujizima na kujiwasha yenyewe na huku sauti ya Socket switch ikisikika kama ilivyo kawaida, hapa nikamstua jamaa yangu ashuhudie kilichotokea mpaka tunalala hali ilikuwa hivyo , na asubuhi mambo yalikuwa kawaida.

Matukio yalikuwa mengi kila mtu akikutana na ya kwake kwa wakati wake kwanzia yule dada na sisi.

Nakumbuka wakati mmoja yule jamaa yangu alinihadithia kuwa alikutana na msichana, mmoja mrefu koridoni (sio yule dada tunaeishi nae)

akawa anaamuuliza

"We wanifahamu mimi"?

"Unaweza kunisaidia kubeba mizigo"?

Hapa jamaa angu alitimua mbio

Siku nyingine tena Mimi binafsi, nlikutana na mikono ya kike ikiwa imenishika isieleweke imetoka wapi yaani hapa mfano mtu awe amesimama halafu kutoka kwa nyuma mikono ije imshike mabegani niliona kucha zilizopakwa Rangi nyekundu nikagundua hilo kuwa ni ya kike.

Matukio yalikuwa mengi mno.

Muda mwingine tukiacha mboga tunakuta zishaandaliwa

Mara tusikie wanawake wakijadili na kucheka kwa sauti koridoni usiku

Mara upishane na wanawake muda wa kwenda chooni

Mara vitu vipite kwa kasi kama nyoka.

Hii nyumba ilikuwa ya don mmoja maarufu wa magari ya Mikoani (Songea to mikoani) inasemekana hapo ndiyo alikuwa ameweka vikolombwezi vyake humo hii ni kwa mujibu wa fununu za walimwengu wa Maeneo hayo.

Kwa wakazi wa maeneo yale watakuwa wanaijua hiyo skendo. Sijui kama hali inaendelea pale au laah kwa maana sisi bado tulimwacha yule Bidada na mara ya mwisho kuwasiliana nae akasema ashamishiwa Njombe.

Ushawahi kukutana na matukio ya ulozi/uchawi

Ilikuwaje?
hiyo misosi iloyopikwa na jini mlikuw mnakula....
 
Back
Top Bottom