Unadhani ni Kitu gani kimembadili ghafla Profesa Shivji na sasa hana Uharaka wa Katiba Mpya huku akisema ni Jambo la Kimjadala zaidi?

Binafsi nakubaliana na Prof. Shivji na nina sababu kuu mbili.

1. Kwanza kabisa ni kwa nini mchakato wa awali ulishindikana kufika mwisho? Sababu ya msingi ilikuwa ni kwa sababu ya kundi fulani waliona kwamba wao ndo wanapaswa kusikilizwa tu. Hivyo wakajitoa na hatimaye kudhoofisha juhudi alizo zianzisha Mzee Kikwete.

Hapa hoja ya msingi kabisa ninkwamba katiba ni maridhiano. Inahitaji kukubaliana. Kuna makundi hayataweza kupata 100% ya wanachokitaka. Hivyo its a give and take process. Sasa kama bado kuna kundi linataka 100% ya kile wao wanachodhani ni sahihi na kiingizwe kwenye katiba bila kujali hoja za mwenzao ni tatizo.

Swali ni je katika huu mchakato mpya yatakuwepo maridhiano? Au utakuwa tena mchakato wa kupoteza fedha?

Hapa ndipo nadhani prof anaona kuna haja ya mjadala.

2. Pili ni dhamira ya makundi mbalimbali yanayo shinikiza katika mpya. Je dhamira yao ni nini? Ingawa wengi wanadai katiba lakini ukweli ni kwamba kila kundi lina dhamira iliyojificha. Makundi haya yanatumia kivuli cha wananchi kudai katiba mpya ingawa nyuma ya pazia wana agenda zao. Kuna wale ambao wanataka katika mpya iwasaidie kuingia madarakani, kuna wale wanataka katiba mpya iendelee kuwaweka madarakani na kuna wale wanaodai katiba mpya isaidie wananchi.

3. Pamoja na katiba ya sasa kuwa na upungufu kadhaa lakini katika awamu ya tano tumeona katika hiyo ikivunjwa waziwazi bila vyombo husika kuchukua hatua. Tumeshuhudia wanao takiwa kulinda katiba wakiisigina. Swali ni je katiba tu inatosha? Hapa ndo dhana ya katiba kuwa si mwarobaini wa matatizo ya watanzania inakuja. Kama tulishindwa kutetea katiba iliyopo hadi ikasiginwa wazi wazi pengine hata tukipata katiba nyingine mtawala atakaye kuwepo anaweza kuosigina vile vile. Hivyo ni muhimu kufikiria zaidi...je tatizo ni katiba?

Kwa hoja hizo tatu nakubaliana kabisa na prof kuwa pengine tatizo hasa si katiba, na tunahitaji kufanyia kazi vitu vingine zaidi. Na pengine hata tukianzisha mchakato mpya utaishia njiani au kuleta sinto fahamu.
 
Suala la katiba kwa tanzania ni mbinu ya kijasusi kuyumbisha nchi isifanye maendeleo badala yake kuwe na malumbano ya kisiasa yasiyokua na tija na kutumika ovyo fedha ya umma. Kama kuna nchi inahitaji katiba kwanza ni uingeteza maana hawana katiba imeandikwa. Halafu marekani katiba yao ina shida na wajinga tunaona hatusemi kitu. Badala yake tunakubali eti hatuwezi endelea hadi tuwe na katiba inaruhusu ushoga. Tunaomba mama samia asicheke na kina mbowe na watu kama mdude.
Walisemaga ukicheka na nyani utakula mabua.
 
Unajuwa kila ukizeeka na akili hupunguwa
 
Afu kuna genge wanadai ni takwa la wananchi

lini wananchi walidai Katiba?.
 
Jibidiishe kusoma machapisho yake.
 
Ni sawa kwa sababu upande mmoja unaaweza kuburruza wengine na kusababisha mzozo. Ni vizurri kila tahadhari ikachukuliwa.
 
Ni mzanzibar kama Mama Rais, Lazima amtetee
Shivji km lilivyo jina lake ni mhindi. Huyu alikuwa against na mchakato tangu mwanzo. Kumbuka shivji alikuwa anaunga mkono mfumo wa serikali 2 au bora tuwe na serikali moja. Lkn shivji habebi taswira ya mawazo yetu. Halafu kuwa professor haina maana kwamba unakuwa na na akili kubwa au mawazo bora. Hivi unajua aliyegundua maandishi hatimaye elimu ikawepo yeye mwenyewe hakuwa amesoma!?? Kama aliyegundua jambo kubwa hv na hakusoma basi hekima, busara na hoja nzuri hazitokani na elimu ya mtu. Hv professor kabudi anafanana kweli na mtu mwenye utimamu wa akili!??
 
Shida kubwa ya Profesa Shivji ni kwamba yupo upande wa serikali. Sijui ni kwa kulinda maslahi binafsi, au kwa sababu ingine anayoijua mwenyewe. Nakumbuka enzi za ujana wake alipambana sana na serikali. Lakini uzeeni naona amesalimu amri.
 
mimi naona prof shivji kaona rais ni mzanzibar mwenzake na pili prof shivji kapata uongozi zanzibar ndio sababu nae pia anatamaa na madaraka
 
Ni kama huwa wanapitiwa na upepo wa kisulisuli, Shivji, Kabudi, Polepole, Bashiru, Lipumba, JK siyo wa kufanya nao project
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…