Unaelewa nini kuhusu mfumo dume?

Unaelewa nini kuhusu mfumo dume?

IKARAHANSI

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2019
Posts
398
Reaction score
479
Hivi karibuni kumekuwepo na wimbi la watu wengi kupinga mfumo dume kwa kusema, eti uondolewe, hawautaki na ni mfumo wa kikandamizaji. Hii imetokana na propaganda za mashirika ya Ulaya na Marekani kupitia mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO'S).

Binafsi nimefanya utafiti na kugundua kuwa baadhi yetu hatujui nini maana ya neno "mfumo" na neno "Dume" kwa wale wanaofahamu baadhi wameamua kujitia wazimu ili wasikose misaada toka kwa "wakubwa wa dunia" na wengine wameamua kukaa kimya na kuacha tukiangamia taratibu.

Kwa maoni yangu "Mfumo dume" ni utaratibu endeshi wa maisha ya binadamu na viumbe hai vingine kasoro mimea. Ni ile hali ya kutoa maamuzi ya mwisho kuhusu jambo/ mambo yaende vipi.

Mfumo huu ulianzia pale Adamu (binadamu wa kwanza mwanaume) kuumbwa na kuelezwa majukumu na wajibu wake katika hii dunia. baadae alilazwa usingizi na kuondokewa ubavu wa kushoto akapatikana Hawa (binadamu wa kwanza Mwanamke) ili awe msaidizi wa Adamu na siyo mshindani.

Kwa mujibu wa wanasayansi, Mwanaume kupitia mwili wake na bila hiyari yake ndiye anaamua mtoto wa jinsia gani azaliwe na ndiye mwenye kuanzisha utaratibu wa kuendeleza kizazi kwa kuwa wa kwanza kusimamisha tupu yake (Katika haya yote Mwanamke ni msaidizi)

Hivyo basi ieleweke kuwa hakuna hata siku moja ambayo wanaume waliwahi kukaa na kuanzisha kinachoitwa "mfumo dume" bali ni MUNGU mwenyewe.

Ikiwa kuna Mwanaume hatimizi moja wapo ya majukumu ambayo alipewa na MUNGU kupitia Adamu, basi alaumiwe Mwanaume huyo na siyo mfumo. Hatua zichukuliwe kwa mkosaji na siyo kulaumu mfumodume.

Mwenye mchango wa mawazo karibu tuelimishane.
 
Huo mfumo ndio umeifanya Dunia kuwa salama mpaka saizi, ndoa za Miaka ya nyuma kuwa salama na hizo ndoa zimezalisha viongozi mahiri, sasa hao wanaoupinga wanataka mfumo jike au et kuwe na usawa ambao kiuhalisia hata wapindue dunia hakuna usawa kati ya mwanaume na mwanamke,

Mfano mdogo tu angalia mwanamke akiwa na uwezo mzuri wa kiuchumi kuliko mwanaume ndani ya familia mambo huenda kombo, hata ukimchapa mwanao Kwa kumfunza adabu utakuta mwanamke anakuja juu "usinipigie mwanangu" mbele ya mtoto
 
Kitu kinachoitwa Mfumo dume kimeingizwa kwenye jamii kihuni sana.

Neno mfumodume limeshindwa kutenganisha majukumu ya mwanaume na mwanamke na kwa kutozingatia majukumu yao kwa asili ya uumbaji wa Mungu.

Neno mfumodume limefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuweka gap kubwa sana na kuharibika kwa maana halisi ya ndoa kadri ya uumbaji na imani zetu.

Leo wanawake vichwa ngumu na wanaume vichwa ngumu.... hata lile andiko la Efeso 5:23 "Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili." linapoteza maana kila siku. Bila kujua maana ya haki sawa na zipi haki sawa Siku hizi mwanaume anadai haki sawa na mwanamke anadai haki sawa

Jameni haki sawa zipogi tuu kama kupata elimu sawa, matibabu, kazi za jamii ila mengine tukiingiza hii kitu tutakufa tukiwa tumechoka sanaa
 
Men wametawala muda mrefu sana; duniani sasa ni zamu ya females. Just relax guys, power is stealthily & steadily sleeping from your flimsy hands!
 
Kitu kinachoitwa Mfumo dume kimeingizwa kwenye jamii kihuni sana.
Neno mfumodume limeshindwa kutenganisha majukumu ya mwanaume na mwanamke na kwa kutozingatia majukumu yao kwa asili ya uumbaji wa Mungu.
Neno mfumodume limefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuweka gap kubwa sana na kuharibika kwa maana halisi ya ndoa kadri ya uumbaji na imani zetu.
Leo wanawake vichwa ngumu na wanaume vichwa ngumu.... hata lile andiko la Efeso 5:23 "Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili." linapoteza maana kila siku. Bila kujua maana ya haki sawa na zipi haki sawa Siku hizi mwanaume anadai haki sawa na mwanamke anadai haki sawa

Jameni haki sawa zipogi tuu kama kupata elimu sawa, matibabu, kazi za jamii ila mengine tukiingiza hii kitu tutakufa tukiwa tumechoka sanaa
Kwa mara ya kwanza nakusoma mama D ukiandika kwa hisia sana! Dah! Ulivyotumia hilo neno hapo sasa: ^kihuni sana^ 🙂 🙂 🙂
 
Ahsante mleta Uzi..naendelea kusoma comments na kujifunza
 
Kwa hiyo generation hii haina dawa tena, mama D ? Au ndiyo yale ya samaki akikauka hakunjiki tena?

Hii generation ya ajabu sana. Nilikutana na ugomvi wa mume na mke siku moja hii familia ina watoto 3, mke anasema amechoka na kutumikishwa... pesa yake ndio inatunza familia(kula,kulala, kuvaa, ada), na bado ameto mtaji ambao mume ndio anasimamia biashara lakini huyo mume hataki kulipa hata school fees za watoto.

Nikasema wanawake sie mabingwa wa kujieleza hebu nimsikilize mume wake!

Weeeee! Mwanaume kacharauka povu kama loteeee anasema mke ana biashara nyingine pia hiyo ndio inatakiwa kulisha familia, halafu suala schoolfess kwa watoto wao lazima wagawane sawa kwa watoto wawili; na kama huyo mmoja hatamlipia atajua mwenyewe😥😥😥
 
Hii generation ya ajabu sana. Nilikutana na ugomvi wa mume na mke siku moja hii familia ina watoto 3, mke anasema amechoka na kutumikishwa... pesa yake ndio inatunza familia(kula,kulala, kuvaa, ada), na bado ameto mtaji ambao mume ndio anasimamia biashara lakini huyo mume hataki kulipa hata school fees za watoto.

Nikasema wanawake sie mabingwa wa kujieleza hebu nimsikilize mume wake!

Weeeee! Mwanaume kacharauka povu kama loteeee anasema mke ana biashara nyingine pia hiyo ndio inatakiwa kulisha familia, halafu suala schoolfess kwa watoto wao lazima wagawane sawa kwa watoto wawili; na kama huyo mmoja hatamlipia atajua mwenyewe😥😥😥
Sasa familia ni yao, mume ni wa mke, na mke ni wa mume. Shida iko wapi? What's the difference? Au mimi ndiye sijaelewa ^key-two^ hapa? I mean, ukitoa pesa kwenye mfuko mmoja, zinaingia mfuko wa pili.

Nakwambia mama D kazi unayo ya kuwapa ushauri! Anyways, Bi Mikopo nasikia anaupiga mwingi mpaka unatoka uwanjani mpira!
 
Unaelewa nini Kuhusu mfumo Dume.!?

Jibu :
Ni ile hali ambayo Mwanaume anashindwa Kutambua wajibu wake na Kuutimiza huo Wajibu wake na Kulazimisha Mwanamke kuliziba hilo Ombwe huku Mwanamke huyo naye akiwa na Wajibu Wake Wa kutekeleza katika utengemao Wa Familia.
Nini Matokeo Ya Hali hiyo?
Mwanaume huyo Kuishi Maisha ya Umariooo au Mwanaume huyo Kuishi akiwa na Gubu Kali au Anakuwa Mkali mkali hivi Ukimgusa Kidogo tu Lazima atajifanya Yeye ni 'Mike Tyson' Au 'Mohamed Ally' , au Mwakinyo au Twaha Kiduku au Dullah Mbabe au Tyson Furry Au......Au ...... Bro Ongezea
 
Back
Top Bottom