Pre GE2025 Unafikiri nini kimewaondoa Makamba na Nape kwenye Uwaziri?

Pre GE2025 Unafikiri nini kimewaondoa Makamba na Nape kwenye Uwaziri?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Could be. wanaamini kuwa godfather wao Kikwete ni more powerful kuliko rais aliyekuwa madarakani; hivyo wanaweza kufanya na kusema lolote.
Wasijue mtu akishakalia kiti pale hakuna ambacho kinaweza mshinda labda awe muoga tu. Yan remote iendeshe tv wakat TV ina batan zake pale basic za kujiendesha hata bila remote au kubatilisha maamuzi ya remote
 
Hawa wote walihusika kwenye mipango ya kuidogosha Ofisi ya Raisi. Waliweza wakati ule, watashindwa nini sasa?

Naweza kusema walikuwa ni watu hatari kwa Usalama wa Nchi.
 
Wakuu,


Usiku umekuwa mchungu kwa Nape na Januari Makamba, tena Nape katenguliwa akiwa akiwa kwenye warsha! Pale unaenda sehemu kama waziri unaondoka mbunge!

Makamba naye alitoa boko lake, huenda hiki ndio kimemuondoa: Kauli ya January Makamba ''hata kama hatumkubali Samia ni wetu'', ina maana gani kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi

Wewe unafikiri nini kimewaondoa wawili hawa kwenye nafasi ya Uwaziri? Kwa nape ni kauli yake ya 'utani' kuhusu ushindi wa Box? Na kwa Makamba je? Byabato naye kaliwa kichwa, itakuwa Nape kamponza!

Au Mama alisoma pendekezo la Erythrocyte - Pendekezo: Nape Nnauye avuliwe Uwaziri haraka kwa kauli hii aliyoitoa jimbo la Bukoba Mjini:KEKLaugh::KEKLaugh::KEKLaugh:

Pia soma: Nape Nnauye: Nawapa pole na naomba radhi kwa kauli yangu ya ushindi nje ya boksi

Nyie mnaonaje wakuu?
Kwa makamba kuna cha zaidi. Kama kauli yake ndio shida basi angeondoka mwenyewe peke yake kama ambavyo kaondoka Nape, FA kabaki lakini wameondoka wote yani waziri na manaibu. Steven huwa hana makuu lakini naye kaondoka nahisi pale wizara ya nje kuna jambo si kauli tu ya January.
 
Hawa nawatabilia kama watashindwa kwenye uchaguzi wa ubunge, wataondoka ccm
 
Kwa Nape inajulikana ni kauli zake za utata kuhusu uchaguzi.

NIJE KWA JANUARY.
Huyu Bwana aliandaa miradi ya upigaji Kama waziri wa mambo ya ndani.
Alianza na kutoa wazo kuhusu kujenga balozi za Tanzania katika nchi Mbali mbali.

Akiwa ameshaanza mchakato wa mradi mmoja haraka haraka bila hata kufanya Feasibility study Rais akasema Mifuko ya Hifadhi ya Jamii uache kufanya miradi isiyo na Tija inadumaza uwezo wao.

Mradi wa Jengo la ubalozi wa Tanzania Jijini Nairobi Kenya.
Jamaa alizindua ujenzi wa mradi wa kujenga jengo la ubalozi wa Tanzania Kenya wa ghorofa sikumbuki ngapi akidai tutapangisha sehem zinazobaki na kuiingizia nchi Pesa.Ila Mfadhiri ni NSSF! Kwa Bilions of Money.
Ajabu hakuna upembuzi yakinifu, Pili unapangishaje eneo la nchi kwa wafanyabiashara.
Maandalizi yalifanyika pia kwa balozi nyingine huko duniani ili apate pa kuchota maji.
 
Nchi hii ina matatizo mengi sana amieacha Nyerere!

Angalia Raisi ni Mzanzibari, Waziri Wa Mambo ya Ndani Mzanzibari, Waziri wa Nje Mzanzibari! Mabalozi wengi Wazanzabari! Wabunge 80 WazanzibarI!!! Na asilimia 20 kazi Muungano ni Wazanzibari!

Halafu visiwa hivi vina watu milioni moja na laki nane tu... na eneo dogo kama Wliaya ya Sikonge!
 
Kibaya tu ni namna hawa jamaa walivyowaponza wale wakuu wa Taasisi tatu - TTCL, Posta na USCAF. Hawa nao walikuwa viherehere sana - yaani walikuwa wanadhamini tu safari za hawa wakubwa bila kujua kuwa fedha hizo jamaa walishapanga kutengenezea network yao. Byabyato pamoja naye kubyabyatuliwa ndiyo alikuwa chanzo kwani juhudi kuuuuuubwaaa zilikuwa zinafanyika kumcovert kwenye mtandao wa Nape na Janu. Hawa jamaa ati walikuwa wanaiga mbinu za JK na Lowasa - bila kujua kuwa teknolojia itawadefeat. Yaani waandishi hao hao wamewapandisha na kuwashusha shwaaaaaaaaaaaaaaa!

Angalia gemu lao - walijisahau hadi kuacha kutamka kuchukua mahela ya Maharage, Ulanga na Mshiba na kutaka na za makampuni ili ati wakamjengee Byababato soko. Hawa wana bwanaaaaa! Mama akaliona gemu zima, akaanza na KUMNAPUA mhusika halafu akaMJANUA mhusika mwingine. Hao ati huitwa watoto wa wafalme (Tundu Lisu alisema). Mama pamoja na apizo langu la hivi karibuni kutokukupa kura, leo ninakuhakikishia kura hiyo ushaipata tena - kwa mwendo huu unaoenda nao. Hawa majamaa wa-jinga sana sana - yaani wana matambo ya hovyoooooo kabisa! Wakati fulani JANU aliongea mbele yako ati sababu kumi za kwa nini wewe uendelee kuwa Rais mwaka 2025 - yaani kwa maneno yale tu mie alinikera na kumfanya nihisi kumbe alishajishtukia kwa kushtukiwa kwake kutaka URais mwaka 2025. Yalikuwa ni maneno ya kukupigia debe na kukukejeli pia kana kwamba ati yeye anawaambia watu kuhusu sababu za wewe kuendelea na nafasi hiyo mwakani. Hivi wazo la wewe kutoendelea lilitoka wapi? Au makali-oni mwake yule bwana. Lakini mbona hata hayo makalio hana?
Hawa watu wabaya sana ndiyo maana walianza kujitengenezea network yao kabambe huku tayari wakishawahadaa akina Peter Ulanga kuanza kudhamini safari zao huku Shirika la TTCL likiwa ilmedorara kwishney kabisa!
 
Back
Top Bottom