Unahisi kwanini P Diddy ametaja hayo majina yote hapo? Ukweli ni huu

Unahisi kwanini P Diddy ametaja hayo majina yote hapo? Ukweli ni huu


Mambo ya fb yanaletwa humu na mtu anaejinasibu kukomaa kiakili na kuaminika. Hovyo kabisa
Hivi FB mnaichukuliaje kwani? Kwani hiki kilichoandikwa FB na mengine yaliyoandikwa
Mambo ya fb yanaletwa humu na mtu anaejinasibu kukomaa kiakili na kuaminika. Hovyo kabisa
Unaua brand Mshana Jr wewe level uliyofikia sio wa kuchukua habari fb tena kwa Mange Kimambi

Tuletee habari kutoka source za maana

Achana na habari za kuunga unga kutoka kwa huyo malaya
 
Hivi FB mnaichukuliaje kwani? Kwani hiki kilichoandikwa FB na mengine yaliyoandikwa


Bro Mshana Jr hata ujitetee vipi leo mimi nakukataa na huu uzi kutoka fb kwa Mange.

Ila utabaki kuwa moja ya members ninaowappreciate sana mkuu

No hard feelings
 
This is too low mshana, Achana na izo Rumors Kwasababu sio Credible kabisa
 
Hu


Majamaa waliingia nyumbani kwa Diddy na wakachukua kila kitu, ikiwemo hard disk za kamera za siri ambazo Diddy alikuwa ameweka kwa ajili ya kurekodi kila kitu kilichokuwa kinaendelea.

Kamera za siri? Yaani alikuwa anarekodi kila kitu, hadi kitendo cha Diamond kuingia kwenye jumba lile, kilirekodiwa.

Hii ni kawaida sana hasa kwa watu maarufu. Wale TISS ya Marekani sasa wanajua kila kitu: nani alifanywa na Diddy, nani hakufanywa, nani alisalimika, na nani aliwahiwa.

Wasanii wengi wapo kimya kwa sababu wanajua kuwa majamaa wana ushahidi wa kila kitu. Wanachofanya ni kuvujisha taarifa moja baada ya nyingine, si kwa bahati mbaya, bali makusudi kabisa.

Jay Z kimyaaaa. Dj Khaled, Beyonce, na Lebron James pia wapo kimyaaaa. Unadhani zile sauti za Burna Boy zinatolewa bure? Ni kwa makusudi.

Mademu wengi wamemalizwa humo, ikiwemo mastaa wa Afrika walioshinda Grammy. Jiulize, kwa nini Davido hasemwi kwenye hili?

Ukizaliwa kwenye pesa na ukakua kwenye pesa, kuna ulimbukeni fulani huna. Tofauti na aliyekuwa choka akipata pesa, huwa tunakosa nidhamu. Hii ni changamoto kubwa kwa watu weusi. Washajua hilo, hivyo inakuwa rahisi kutudhibiti.

Hawakushindwa? Wanamtumia mkeo; anaomba talaka, unatozwa pesa nyingi. Hakuna mtu mweusi aliye salama kwa sababu ya ulimbukeni wa pesa tulionao.

Wakipata pesa, maslay queen wote wanataka kula, washikaji wanakula bata klabu, na mbaya zaidi, washauri wetu huwa ni watu weusi. Angalia wale walio na washauri wa kizungu huko US, kuna tofauti kubwa.

Mpaka sasa, hakuna staa aliye salama, hasa kwa Diddy. Diddy hawezi kuchomoka hili, ama atafungwa au mtu atatumwa aondoe roho yake.

Ukiua kwa upanga, utakufa kwa upanga. Huwezi kumuua 2pac ukabaki salama. Huwezi kumdedisha BIG na kumdhulumu mkewe Faith Evans ukabaki salama. Huwezi kumdhulumu Mase, akaangua kilio kanisani halafu ukabaki salama.

Mara nyingine, tunatengeneza hatima yetu hapa duniani. Umeua kwa upanga, utakufa kwa upanga.

H


Majamaa waliingia nyumbani kwa Diddy na wakachukua kila kitu, ikiwemo hard disk za kamera za siri ambazo Diddy alikuwa ameweka kwa ajili ya kurekodi kila kitu kilichokuwa kinaendelea.

Kamera za siri? Yaani alikuwa anarekodi kila kitu, hadi kitendo cha Diamond kuingia kwenye jumba lile, kilirekodiwa.

Hii ni kawaida sana hasa kwa watu maarufu. Wale TISS ya Marekani sasa wanajua kila kitu: nani alifanywa na Diddy, nani hakufanywa, nani alisalimika, na nani aliwahiwa.

Wasanii wengi wapo kimya kwa sababu wanajua kuwa majamaa wana ushahidi wa kila kitu. Wanachofanya ni kuvujisha taarifa moja baada ya nyingine, si kwa bahati mbaya, bali makusudi kabisa.

Jay Z kimyaaaa. Dj Khaled, Beyonce, na Lebron James pia wapo kimyaaaa. Unadhani zile sauti za Burna Boy zinatolewa bure? Ni kwa makusudi.

Mademu wengi wamemalizwa humo, ikiwemo mastaa wa Afrika walioshinda Grammy. Jiulize, kwa nini Davido hasemwi kwenye hili?

Ukizaliwa kwenye pesa na ukakua kwenye pesa, kuna ulimbukeni fulani huna. Tofauti na aliyekuwa choka akipata pesa, huwa tunakosa nidhamu. Hii ni changamoto kubwa kwa watu weusi. Washajua hilo, hivyo inakuwa rahisi kutudhibiti.

Hawakushindwa? Wanamtumia mkeo; anaomba talaka, unatozwa pesa nyingi. Hakuna mtu mweusi aliye salama kwa sababu ya ulimbukeni wa pesa tulionao.

Wakipata pesa, maslay queen wote wanataka kula, washikaji wanakula bata klabu, na mbaya zaidi, washauri wetu huwa ni watu weusi. Angalia wale walio na washauri wa kizungu huko US, kuna tofauti kubwa.

Mpaka sasa, hakuna staa aliye salama, hasa kwa Diddy. Diddy hawezi kuchomoka hili, ama atafungwa au mtu atatumwa aondoe roho yake.

Ukiua kwa upanga, utakufa kwa upanga. Huwezi kumuua 2pac ukabaki salama. Huwezi kumdedisha BIG na kumdhulumu mkewe Faith Evans ukabaki salama. Huwezi kumdhulumu Mase, akaangua kilio kanisani halafu ukabaki salama.

Mara nyingine, tunatengeneza hatima yetu hapa duniani. Umeua kwa upanga, utakufa kwa upanga.

Huko hakuna kesi za ushoga nihalali....wao wameleta ushoga hawana kipengele cha kumfanya lolote
 
Diddy hawezi kuchomoka hili
Kweli kabisa, yajayo yanafurahisha!

Sean 'Diddy' Combs faces more than 100 new assault allegations​


More than 100 people are to sue rap musician Sean 'Diddy' Combs for sexual assault, rape and sexual exploitation, a US lawyer has said.

9 hours ago

 
Miaka ile ya 90 wakati Bad Boys wakiwa juu, juu karibu na mawingu kabisa, kulikuwa na mwamba wa kuitwa Mase. Huyu mchizi alikuwa mkali sana kwenye kuimba, ni moto mkubwa sana.

Alikuwa mshikaji sana na Diddy, yaani naye alikuwa ndani ya Bad Boys, aliona kila aina ya uchafu, aliona kila aina ya manyanyaso. Jamaa aliimba na Diddy kwenye ngoma nyingi, yaani by then ukisikia Diddy katoa ngoma, jua Mase yupo, anaimba kama amechoka hivi.

Miaka iliposgea, Mase akajiengua kutoka Bad Boys. Binafsi niliumizwa sana, tena sana kwa sababu jamaa alikuwa hatari sana na walikuwa wanapendeza sana kufanya ngoma na Puff Daddy.

Ni kama piece of Diddy iliondoka maishani mwake. Na nadhani hii ndiyo ilimfanya kuwa vigumu sana kuweka ukaribu kimuziki na mtu mwingine kama ilivyokuwa kwa Mase.

Mase aliondoka na kuamua kumtumikia Mungu, akaachana na kila kitu, akaingia kanisani. Baada yake akaja jamaa wa kuitwa Loon, huyu aliwekwa kwa lengo la kuchukua nafasi ya Mase aliyeamua kuondoka na alikuwemo kwenye ngoma ya I Need A Girl.

Jamaa naye baadaye akaondoka zake, akasilimu na kuwa Muslamu safi kabisa wa swala tano. Diddy akabaki peke yake, washikaji zake wakaondoka. Siku nyingine nitakuja na stori ya huyu Loon kilichotokea mpaka kusepa.

Tuendelee.

Mase akafanya kipindi kabisa kuzungumzia kilichokuwa kimetokea. Kubwa zaidi lilikuwa ni maslahi binafsi. Unajua wakati BIG alipokuwepo, mambo yalikuwa yanakwenda poa tu, Bad Boys ilikuwa inawajali wasanii wake, malipo mazuri tu ila baada ya kufariki, kila kitu kibadilika.

BIG ndiye aliyekuwa akimkontroo Diddy nini cha kufanya na nini si cha kufanya. Sasa dizaini ni kama kulikuwa na mambo mengi ambayo Diddy alitamani kufanya lakini alikuwa akizuiliwa na BIG.

Mambo ya pesa ndiyo yalikuwa kila kitu. BIG alipofariki, Diddy akaichukua Bad Boys jumla, akabadilisha kila kitu na kuweka umiliki wake kwa 100% na ndiyo maana mpaka leo ukiangalia mwanzilishi wa lebo hiyo kubwa alikuwa nani, utakuta ni Diddy, alibadilisha kila kitu na akawa anampoza Faith Evans hela za kubadilishia mboga na mavazi.

So BIG amefariki, Mase alikaa Bad Boys kwa miaka michache na ndipo akaamua kujiondokea zake kwani alikuwa anadai pesa nyingi sana na kila alipokuwa akimkumbusha Diddy, alimwambia bado cheki haikusainiwa.

Hili lilimuuma mchizi kwa sababu alijua Diddy ndiye bosi, nani alitakiwa kusaini cheki? BIG? Craig M? Loon? Nani alitakiwa kusaini hizo cheki ili alipwe pesa zake?

Okay! Mase anasema kwamba kabla ya kujiondoa na kuuweka wazi aliamua kufanya mambo manne kwanza kwa Diddy. Hakutaka kukurupuka na kuondoka tu, alihitaji kuona nini kingetokea kama angeyafanya haya manne, je, angelipwa pesa zake ama la.

Jambo la kwanza kabisa lilikuwa ni kumfuata kama kaka yake, kama ndugu na kuzungumza naye. Alimzoea sana, walikuwa kama walizaliwa na mama mmoja, walizungumza masuala ya kipesa, kulipwa, ila Diddy akakataa.

Mara ya pili alikwenda na shahidi. Alitaka kuwemo na mtu ambaye hata kama baadaye kutatokea la kutokea, kuwe na shahidi wa kuwa upande wake. Alimchagua shahidi gani? Rodney Jerkins. Huyu jamaa alikuwa prodyuza na rapa. Anasema alifanya hivi kama Biblia ilivyoagiza kwamba kama hutokubaliana naye, nenda na shahidi.

Anasema jambo la tatu ni kwenda kanisani na kukutana na viongozi. Mase anasema alifanya hivyo, alikwenda kanisani na kukutana na askofu wake Diddy. Bado akakataa.

Na kitu cha nne kabisa alichokifanya ni kuamua kutoka hadharani na kuyazungumza hayo yote kwa kuwa hayakuwa yamefikiwa muafaka.

Kumbuka kipindi ambacho Mase alikuwa anaondoka Bad Boys watu walimdhiaki sana, walimuita kila jina la ujinga. Inakuwaje unaondoka kwenye lebo kubwa kama hiyo? Yaani watu wengi waliikimbilia na kuomba kila siku waingie humo, ila wewe unaikimbia. Alionekana kama mjinga fulani hivi. Hawakujua aliyokuwa akiyapitia, ila miezi mitatu iliyopita, kila mmoja akasema “The guy was right.”

Mase anaendelea kufunguka kwamba ukaribu wake na Diddy haukuwa kutengeneza ngoma kali ama kutengeneza pesa tu bali alikuwa analazimisha kutoka ili awe na uhuru, amani kwani watu waliokuwa wakifika kwenye jumba lake kubwa, walimuona kama mtu mzuri lakini nyuma ya pazia hakuwa kama vile watu walivyomuona.

Kuna siku ndani ya ukumbi alipewa kipaza sauti na kuongea, aliyasema haya:

“Nilipokuwa chini ya Diddy nilishinda njaa kwa kuwa nilifanya kazi kubwa bila malipo. Unapofanya kazi ofisini na hulipwi, hakuna umuhimu wa kurudi ofisini. Watu walikuwa wananiuliza kama hulipwi kwa nini unarudi kazini? Nikawa nawajibu ni kwa sababu niliahidiwa kulipwa, so ilikuwa ni lazima niwe narudi mara kwa mara. Nilipoona mambo hayajanyooka, nikaamua kuondoka mazima.”

Kwa watu ambao hawajui hili ni kwamba kila kitu anachomiliki Diddy kimeandikwa kwa jina la mama yake. Yaani ni kama Hakimi alivyoandika kila kitu kwa umiliki wa mama yake, so kama watataka kumfilisi harakaharaka watashindwa na ndiyo maana FBI walianza kufu
FB_IMG_1727849131063.jpg
atilia umiliki wa mali hizo kwa mama yake.
 
Back
Top Bottom