Infinite_Kiumeni
JF-Expert Member
- Jan 23, 2023
- 382
- 687
Aidha unaongea na mwanamke kwa mara ya kwanza au tayari upo na mwanamke lakini mazungumzo yenu yanakua kama mahojiano ya kutafuta kazi/ polisi hakuna hisia zozote, hakuna kuchombezana na we mwenyewe unaona haufurahii mazungumzo. Hivi ndivyo unaweza na kuyabadilisha kuwa mazungumzo yenye raha.
Yaongoze mazungumzo. Usije ukakaa na mwanamke ukasubiri ye ndo awe kiongozi. Muvi nyingi zinaonesha ivo lakini haifanyi kazi kwenye maisha halisi. Wewe ndo uongoze mazungumzo kuelekea utakako, mazungumzo utakayo wewe. Wanawake wanapenda kuwa na watu wanaowaongoza. Ukiamuachia mwanamke hili jukumu yeye atakuongoza kwenye urafiki, na atakuweka wewe kama rafiki yake tu (sio lengo lako hili).
Jibu maswali kwa stori badala ya jibu la moja kwa moja. Wanawake wanapenda taarifa hasa ikiwa na vitu vingi. Ukisimulia stori unakua unaweka mada tofauti tofauti hivyo inakua rahisi kwa mwanamke kuuliza maswali zaidi na kupata mazungumzo marefu kuliko kumuacha ayaongoze mazungumzo yeye. Mfano, unaulizwa unapenda chakula gani, badala ya kusema pilau na kubaki hakuna kitu, toa stori.
Mfano, kuna siku nilikua safarini kwenda Tanga, kuna shughuli tulikua tunaenda kufanya, kuna hoteli tulisimama wenzangu wakaenda kula ila mi nikawasindikiza tu, yule mhudumu alipoona sili akaniuliza na nikamuambia naogopa vyakula vya njiani, akaanza kunishawishi, akanishauri pilau na akaniambia kiasi cha kula mpaka nikashawishika, aisee sikuwahi kula pilau kama hilo na sikuumwa tumbo safari nzima, tangu siku hiyo nina hamu na pilau tu. Apo umetoa mada tofauti za kuendeleza mazungumzo, umeenda Tanga, ulikutana tena na huyo mhudumu?, mara ya mwisho umekula pilau lini tena, mlienda kwa shughuli gani. Lakini ungesema tu pilau kusingekua na chochote cha kuchochea mazungumzo.
Kuwa mcheshi. Sio lazima uwe kama MC Pilipili ila utengeneze hali ya kumfanya afurahi na kutabasamu. Njia rahisi ni kutoa stori yako ya utotoni ambayo we mwenyewe ukiikumbuka unacheka na pia anayoweza kuielewa kwa kuwa ni vitu vinavyojulikana sana. Mfano, labda uliwahi kumdanganya mzazi wako siku ya wajinga alafu ukaishia kuchapwa, au jinsi ulivojikojolea kwa kuogopa kuchapwa na mwalimu.
Tengeneza hali ya sisi (wewe na mwanamke). Tumia maneno yenye, tuna…, tuta… sana zaidi ya mimi na wewe. Hii inamfanya ajione yupo katika maisha yako hivyo inakua rahisi na yeye pia kuchangia.
Ongelea mambo ya baadaye. kama we ni mdogo au hauna maisha ya kuvutia sana au hauna hela ya kuishi maisha ya kukuvutia we mwenyewe hilo lisiwe kikwazo. Cha muhimu uwe na malengo. Unaweza zungumzia vitu unavotaka kuvifanya, sehemu unayotaka kwenda, unataka uwe nani lakini hauna haja ya kudanganya, au kumdanganya utampeleka Dubai. Ubaya wa uongo ni kutengeneza sumu ya kwenye mahusiano.
Toa stori ya kwanini unataka ivo, au kinachokusukuma (motisha).
Epuka kuuliza maswali yanayohitaji jibu la ndio/ hapana. Mfano, unapenda kusafiri? Aidha utajibiwa ndio au hapana. Njia ni nzuri ya kuuliza maswali yanayohitaji jibu la kuelezea. Mfano, sehemu gani ushawahi kusafiri ikakuvutia? Kwanini?. Njia nzuri zaidi ni kuanza kutoa wewe stori ya sehemu uliyosafiri na ukaifurahia alafu muulize na yeye ilikuaje stori yake. Hapa unakua kiongozi na kumuongoza kile mnachotaka kukizungumzia na jinsi ya kuzungumzia.
Ongea kwa kujiamini na ukiwa na tabasamu. Mara nyingi haijalishi unasema nini, kwa mwanamke inajalisha zaidi jinsi unavyokisema. Pia unapuliza uliza kwa kujiamini. Wanawake wanapenda kuwa na watu wanaojiamini, achana na zile muvi za Hollywood zinazoonyesha mwanaume anaongea kwa kujing’atang’ata.
Ndio maana katika kundi la infinite kiumeni ndio sehemu pekee utakayojifunza na wanaume wengine ili kuwa bora na kujiamini zaidi katika mahusiano na mapenzi na mwanamke unayehitaji kujenga naye maisha.
Yaongoze mazungumzo. Usije ukakaa na mwanamke ukasubiri ye ndo awe kiongozi. Muvi nyingi zinaonesha ivo lakini haifanyi kazi kwenye maisha halisi. Wewe ndo uongoze mazungumzo kuelekea utakako, mazungumzo utakayo wewe. Wanawake wanapenda kuwa na watu wanaowaongoza. Ukiamuachia mwanamke hili jukumu yeye atakuongoza kwenye urafiki, na atakuweka wewe kama rafiki yake tu (sio lengo lako hili).
Jibu maswali kwa stori badala ya jibu la moja kwa moja. Wanawake wanapenda taarifa hasa ikiwa na vitu vingi. Ukisimulia stori unakua unaweka mada tofauti tofauti hivyo inakua rahisi kwa mwanamke kuuliza maswali zaidi na kupata mazungumzo marefu kuliko kumuacha ayaongoze mazungumzo yeye. Mfano, unaulizwa unapenda chakula gani, badala ya kusema pilau na kubaki hakuna kitu, toa stori.
Mfano, kuna siku nilikua safarini kwenda Tanga, kuna shughuli tulikua tunaenda kufanya, kuna hoteli tulisimama wenzangu wakaenda kula ila mi nikawasindikiza tu, yule mhudumu alipoona sili akaniuliza na nikamuambia naogopa vyakula vya njiani, akaanza kunishawishi, akanishauri pilau na akaniambia kiasi cha kula mpaka nikashawishika, aisee sikuwahi kula pilau kama hilo na sikuumwa tumbo safari nzima, tangu siku hiyo nina hamu na pilau tu. Apo umetoa mada tofauti za kuendeleza mazungumzo, umeenda Tanga, ulikutana tena na huyo mhudumu?, mara ya mwisho umekula pilau lini tena, mlienda kwa shughuli gani. Lakini ungesema tu pilau kusingekua na chochote cha kuchochea mazungumzo.
Kuwa mcheshi. Sio lazima uwe kama MC Pilipili ila utengeneze hali ya kumfanya afurahi na kutabasamu. Njia rahisi ni kutoa stori yako ya utotoni ambayo we mwenyewe ukiikumbuka unacheka na pia anayoweza kuielewa kwa kuwa ni vitu vinavyojulikana sana. Mfano, labda uliwahi kumdanganya mzazi wako siku ya wajinga alafu ukaishia kuchapwa, au jinsi ulivojikojolea kwa kuogopa kuchapwa na mwalimu.
Tengeneza hali ya sisi (wewe na mwanamke). Tumia maneno yenye, tuna…, tuta… sana zaidi ya mimi na wewe. Hii inamfanya ajione yupo katika maisha yako hivyo inakua rahisi na yeye pia kuchangia.
Ongelea mambo ya baadaye. kama we ni mdogo au hauna maisha ya kuvutia sana au hauna hela ya kuishi maisha ya kukuvutia we mwenyewe hilo lisiwe kikwazo. Cha muhimu uwe na malengo. Unaweza zungumzia vitu unavotaka kuvifanya, sehemu unayotaka kwenda, unataka uwe nani lakini hauna haja ya kudanganya, au kumdanganya utampeleka Dubai. Ubaya wa uongo ni kutengeneza sumu ya kwenye mahusiano.
Toa stori ya kwanini unataka ivo, au kinachokusukuma (motisha).
Epuka kuuliza maswali yanayohitaji jibu la ndio/ hapana. Mfano, unapenda kusafiri? Aidha utajibiwa ndio au hapana. Njia ni nzuri ya kuuliza maswali yanayohitaji jibu la kuelezea. Mfano, sehemu gani ushawahi kusafiri ikakuvutia? Kwanini?. Njia nzuri zaidi ni kuanza kutoa wewe stori ya sehemu uliyosafiri na ukaifurahia alafu muulize na yeye ilikuaje stori yake. Hapa unakua kiongozi na kumuongoza kile mnachotaka kukizungumzia na jinsi ya kuzungumzia.
Ongea kwa kujiamini na ukiwa na tabasamu. Mara nyingi haijalishi unasema nini, kwa mwanamke inajalisha zaidi jinsi unavyokisema. Pia unapuliza uliza kwa kujiamini. Wanawake wanapenda kuwa na watu wanaojiamini, achana na zile muvi za Hollywood zinazoonyesha mwanaume anaongea kwa kujing’atang’ata.
Ndio maana katika kundi la infinite kiumeni ndio sehemu pekee utakayojifunza na wanaume wengine ili kuwa bora na kujiamini zaidi katika mahusiano na mapenzi na mwanamke unayehitaji kujenga naye maisha.