x - mas
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 931
- 612
amani iwe nanyi ndugu zangu,kuna hii kitu inanishangaza sana utakuta kijana mfanya kazi za kawaida sana tukiachana na kazi zenye mishahara mikubwa kama ubunge hapa nazungumzia kwa mwanajeshi, mwalimu,askari,bibi/bwana shamba au nesi halafu ni bachela hana mke wala familia amepata pesa labda kwa mkopo,sasa huyu mtu badala ya kufungua mradi aongeze kipato ana kimbilia kununua kiwanja na kujenga nyumba ya kuishi na sio ya biashara utafikiri kaambiwa kuwa viwanja vitaisha kesho ndugu yangu nakwambia viwanja haviishi leo Tanzania hii utazeeka na kufa wewe viwanja vitaendelea kupatakana labda kwa baadae sana ndo tutasema viwanja vimeisha kwani hata marekani pamoja na kuwa na majengo mengi hukitaka kuwa na nyumba yako leo hii utapata hela yako tu..naomba uniwieradhi kama nimekuvunja moyo ila ndo ukwali huo ongeza kipato chako kwanza ndo ujenge nyumba.