Unajenga nyumba utakula hiyo nyumba!?

Hili wazo ni sahihi kwa mfanya biashara kwakua biashara ndiyo kazi na mwajili ni mtaji ,na huiamini biashara ndiyo inayo mpa pesa na hawezi
kuto iamini biashra anayo fanya kila siku na siyo mfanya kazi yeye hajui biashara anacho jua ni mshahara tu hana imani kama ukiwekeza kwenye biashra utapta faida.
Mtoa mada mfanya biashra na wengi walio changia ni wafanya kazi ndiyo sababu ya kukinzana.
Kila mtu anya lake analo ona jema
 
well said, labda niongezee tu unakuwa kwako uko free kuleta ndugu ambao watafikia badala ya kuwapangishia gesti ikiwa nyumba ya kupanga ndogo, ninaweza kufuga, kulima bustani kwa matumizi yangu na biashara, kufundisha tuition, kufanya consultancy etc, ninaweza kuweka fremu nikafanya biashara duka au chochote bila kulipa kodi.
Kifupi kuwa kwangu ni amani na faida zaidi kuliko kupanga, ninajua jinsi gani nitumie maji na umeme kulingana na kipato changu kuliko kushare sijui servent quarter au nyumba na tu,
value ya nyumba inakua kila kukicha na pia ni collateral nzuri kuchukulia mkopo
investment yake ni kidogo kidogo kwani ujenzi sihitaji kuinvest mamilioni kwa mkupua bali kila nipatapo ndio najenga tofauti na biashara nyingine inabidi uwekeze mtaji mkubwa la sivyo inakuwa liability
Kusema kweli mimi bado na struggle hadi niwe mama mwenye nyumba zaidi ya moja!
NB mtoa mada nimekuelewa uliposema wazi wewe unakaa nyumba ya serikali hivyo usidangannye wenzio, ila siku ukitolewa hapo utakumbuka hii thread
 
Mtoa mada una akili sana, mwenye uwelewa wa dunia inavyoenda hawez kubishana nawe, kwa mtu bachelor kuanza biashara kwanza ni jambo muhimu sana kwani experience atayopata itamsaidia maisha yake yoote. Mkopo wa pili anaweza kuugawa, nusu akanunua kiwanja na nusu akaiboresha biashara aliyoianza then kwa faida na mashahara kidogo anaopata anajenga taratibu.
Kujengea nyumba mkopo wa kwanza ni kuzika fedha, kuzika changamoto za maisha, kuukaribisha umaskini tu, kwani nauhakika huwez jenga nyumba ya kupangisha kwa mkopo wa kwanza, na hata ukipangisha je we utakaa wapi? Utapata kiasi gani kwa mwezi? Return on investment itachukua miaka mingapi? Then compare na anaefanya biashara utaona yupi atafaidika zaidi kwa baadae
 
Wakubwa muwe mnasikiliza na upande wa pili wa kila jambo! Hili jambo la kuhusu kujenga au kuwekeza linaongelewa sana hivi sasa! Ni mtazamo mpya kama mkakati kwa wanaotaka kujikomboa kifedha (financial independence)! Ni mawazo mapya kabisa kama mkakati wa kujikomboa kifedha.

Kuna thread hapa jamii forums ya wahasibu ambako kunaubishi mkali sana kwamba je nyumba ni asset au liability! Katika mtazamo mpya wa kujikomboa kifedha unaowakumba wengi imedhihirika kuwa ununuzi wa vitu ambavyo haviingizi pesa kama magari ya kutembelea, ujenzi wa nyumba za kuishi, na mavitu mengine mengi yasiyoingiza pesa humwongezea mzigo mtu kwani huhitajika kuvihudumia hivyo vitu badala yeye vimhudumie!

Wajuzi wanaelekeza kuwa ili kujikomboa kifedha yapaswa kununua vitu vinavyoingiza pesa ili hata kama umelala unaumwa au uko kwenye kazi zingine hivyo vitu vinakuingizia pesa! Kutokana na makusanyo ya pesa ya hivyo vitu (Assets) sasa waweza kujenga na hata kununua gari la anasa! Utakapokuwa unajenga au kununua gari la anasa, hivyo vitu vitakuwa vinaendelea kukuingizia pesa kama kawaida. Vitu vya kukuingizia pesa si biashara za mali kuoza au zenye kukufanya ukae kutwa unafuatilia na bp ya kupanda na kushuka la, inaweza kuwa ni kitu cha kukodisha kama toroli, mashine na mitambo, magari ya biashara, nyumba za kupangisha hasa Guest house!

Kwa anaetaka kujikomboa hawezi kushindwa kuvumila kero za muda mfupi za nyumba ya kupanga ili aweze kutimiza malengo ya muda mrefu ya kujikomboa kifedha. Ujenzi ni kitu kinakausha pesa kupita maelezo labda kama ni fisadi! Lakini kwa vile si lazima kila mtu ajikomboe kifedha ujumbe huo unawahusu waelewa hata kama atakuwa mmoja akielewa atajikomboa!

Huyo ndugu aliejenga nyumba kwa million 20 na kuokoa laki 2 kila mwezi, ataokoa million 2.4 kwa mwaka, lakini kama angenunua trekta la Farmtrac kwa bei ya sasa Milioni 16 halafu akapanga nyumba laki 2 kila mwezi, kipato chake baada ya mwaka mmoja hadi miwili lazima atajenga nyumba hiyo na ataendelea kudumu na trekta hilo kwa miaka 20 na zaidi huku akiendelea kukamua.

Hebu kumbuka vitu vingine vingi vidogo kwa vikubwa ambavyo ukinunua mara moja vinaanza kukuingizia pesa kila siku! Hatusemi ukipata pesa ufungue biashara ya samaki au nyanya au Bar, wazo hapa ni kununua 'assets' vitu vinavyoingiza pesa, siyo vitu vinavyotumia pesa na siyo ujenzi wa nyumba inayozuia pesa isizae. Nyumba na vinginevyo visivyoingiza pesa vitanunuliwa na vitu vinavyoingiza pesa yaani assets! Nyumba siyo asset labda kama ni ya kupangisha au Guest house, lakini unayokaa mwenyewe hiyo ni LIABILITY, kalaga baho!!

Akili ni nywele kila mtu ana zake ndiyo maana wengine wanajikomboa kifedha na wengine ni kupanda maua na kupaka rangi nyumba zao kila siku. Acha vitega uchumi vyako vijenge na vikununulie gari la kutembelea!
 
Mawazo ya mtoa mada ni ya kijasiriamali zaidi. Na wajasiriamli ni wachache sana kwenye ulimwengu wa leo. Ndiyo maana wengi wao wanampinga. Ni mara chache sana unaweza kumwambia mtu aache kazi ajiajiri mwenyewe akubaliane na wewe. Wengi wao watakujibu niache kazi nile nini? Familia yangu ile nini? Nitaishije? Maswali chungu nzima. Ndo maana hata hapa utakutana na maswali kama, si afadhali kuishi kwenye nyumba yako..., si afadhali kuachana na kero za kupanga? Wao maisha ni kutatua kero moja leo na kuendelea kuishi kwenye utumwa mwingine miaka nenda rudi.

SO MTAZAMO WANGU NI HUU;

1. Kama aliyechukua mkopo siyo mjasiriamali, ni afadhali akajenga nyumba ya kuishi maana hela yote itaishia kwenye starehe na kubakia kuwa omba omba maana mshahara ndo hivyo tena anagawana mdai wake.

2. Kama aliyechukua mkopo ana ndoto ya kuwa mjasiriamali na amebanwa sana kazini, na hataweza kufuatilia biashara yoyote namshauri ajenge nyumba kwa ajili ya biashara, atakusanya hela ya kodi, value ya nyumba na kiwanja vitakuwa vinaongezeka kila siku, mwisho wa siku kama atakuwa anataka kuacha kazi anaweza kuuza nyumba, changanya na hela ya kodi ni mtaji tosha wa kufanyia biashara na kuachana na utumwa wa kufanyia kazi watu wengine.

3. Kama aliyechukua mkopo ni mjasiriamali muajiriwa ambaye hajabanwa kazini, basi fungua biashara ambayo umeifanyia utafiti wa kutosha na kuridhika kuwa ukingiza mtaji wako hela yako itakuwa inazunguka vizuri na kupata faida ya kuweza kufanya hayo mambo mengine kama kujenga makazi ya kuishi n.k.

Huu ni mtazamo wangu tu kama mjasiriamali.
 
Halo Mwanawao hiyo uliyoandika inaitwa summation (majumuisho) yaani umegonga penyewe kabisa, hakuna cha kuongeza wala chakupunguza, waoga umewaridhisha, wale wa mishahara umewaridhisha na wajasilia mali pia umewaridhisha, I salute you Mwanawao! Nyie ndo mgeshirikishwa kwenye kutoa ufumbuzi wa kugombea ziwa nyasa.
 

Umesema kila kitu wengi wetu ndo hilo kundi la pili, ujasiriamali tunaupenda ila ndo tunajifunza, baadae tukiingia kundi la tatu tutatumia viwanja, nyumba au pension kuingia kwenye biashara. Imagine mtu unatoka nyumbani saa kumi na mbili unarudi kumi na mbili au saa moja jioni na hii ni wote baba, mama na watoto kuna biashara gani wewe uta risk kuchukulia mkopo uwaachie wafanyakazi? Kwasababu anavyoongelea ni kuwa unakopa kama mfanyakazi na utalipa kwa mshahara hadi hiyo biashara ianze kulipa sasa biashara kwa remote control ndo maana tunamwambia ni bora nyumba, hata iwe mbali nikijenga ukuta nitaukuta ulinzi ni nadra baada ya kumaliza napangisha sihitaji kumfatilia mpangaji vilevile vi fremu huko nje sina haja kumfatilia mpangaji mwisho wa mwaka au nakusanya kodi yangu.
Kwa sisi wafanyakazi home business ni muafaka kwa kuanzia na huwezi kuiweka kwenye nyumba ya kupanga. Ukiisha jifunza na kupata wateja wa uhakika unaweza kuacha kazi vinginevyo unatafuta kuwa omba omba. Ni mtazamo wangu.
 
Kuna mawazo huwezi kuyatekeleza ukiwa nyumba ya kupanga au kwa shemeji,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…