Unajua au umewahi kusikia nini kwahusu kunguru?

Unajua au umewahi kusikia nini kwahusu kunguru?

I am Groot

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2018
Posts
3,929
Reaction score
10,747
Kunguru ni ndege mwenye sifa za kipekee sana. Mmoja kati ya ndege anayejulikana sana duniani. Je, unafahamu nini au umewahi kusikia jambo gani kumhusu ndege huyu? Ngoja tumpe maua yake.

images (1).jpeg


1. Kunguru wana akili kinoma noma. Ni kama akili walizo nazo watoto wa miaka saba kwa upande wa binadamu. Watu mbalimbali wmeshuhudia hawa jamaa wakiangusha vitu vigumu kulika toka juu hadi chini mfano barabarani kwenye lami au kuvitega njiani magari yakanyaje ili vitu hivyo vivunjike wale vya ndani.

2. Kunguru ni waaminifu kwa wenza wao. Inasemekana; kunguru huzaa na kulea jike au dume moja tu maisha yake yote. Na mmoja kati yao akifa; basi huyo mmoja atabaki single hadi atakapokufa. Kunguru hana baya!.

3. Kunguru ni mzuri katika kukariri. Kunguru wanauwezo wa kukariri sura ya mtu mbaya kwao na kubebelea kinyongo cha kulipiza kisasi hapo baadae.

4. Kunguru wana lugha na lafudhi zinazotofautiana. Kwa kila eneo Kunguru wa eneo hilo husika huwa na lugha yao. Kwa maana kuwa kunguru huwa na sauti moja ila namna ya utoaji wa sauti hizo hutofautiana kati ya Kunguru wa eneo moja hadi jingine. Watu wanaoishi na kunguru maeneo yao wataelewa zaidi point hii.

5. Kunguru huuzunikia na kuaga mwili wa maiti ya Kunguru mwenzao. Jambo hili ni nadra sana kwa viumbe wengine hasa aina nyingine ya ndege. Mara kadhaa Kunguru wameshuhudiwa kukusanyika kwa wingi hadi kwa makumi na mamia katika eneo ambapo kuna mwenzao kafia.

6. Kunguru huchelewa sana kuoza akifa. Na hata kuoza kwao huchukua muda mrefu na taratibu sana tofauti na viumbe wengine. Hapa ndipo huja ile dhana ya wengi kufikiri kunguru hawaozi ila kumbe sivyo!.

7. Hawa jamaa ndiyo ndege pekee mwenye ubongo mkubwa kuliko ndege mwingine yeyote.

8. Wanauwezo na ujuzi mzuri wa utatuzi wa changamoto mbalimbali. Inaelezwa kuwa wanaweza pia kutumia zana tofauti tofauti kufanikisha matakwa yao. Viumbe wengine wanaofaamika kutumia nyezo ni binadamu, Orangutans, Chipanzee na sokwe.

images.jpeg
 
Miaka ya 2000 Sinza dada wa salun alinunua mafuta ya nywele akayaacha nje yakiwa ndani ya mfuko, Kunguru aliubeba ule mfuko akaja kuudondosha nyumbani kwenye kichanja cha kuanikia vyombo.
 
Kunguru ni ndege mwenye sifa za kipekee sana. Mmoja kati ya ndege anayejulikana sana duniani. Je, unafahamu nini au umewahi kusikia jambo gani kumhusu ndege huyu? Ngoja tumpe maua yake.

View attachment 3011887

1. Kunguru wana akili kinoma noma. Ni kama akili walizo nazo watoto wa miaka saba kwa upande wa binadamu. Watu mbalimbali wmeshuhudia hawa jamaa wakiangusha vitu vigumu kulika toka juu hadi chini mfano barabarani kwenye lami au kuvitega njiani magari yakanyaje ili vitu hivyo vivunjike wale vya ndani.

2. Kunguru ni waaminifu kwa wenza wao. Inasemekana; kunguru huzaa na kulea jike au dume moja tu maisha yake yote. Na mmoja kati yao akifa; basi huyo mmoja atabaki single hadi atakapokufa. Kunguru hana baya!.

3. Kunguru ni mzuri katika kukariri. Kunguru wanauwezo wa kukariri sura ya mtu mbaya kwao na kubebelea kinyongo cha kulipiza kisasi hapo baadae.

4. Kunguru wana lugha na lafudhi zinazotofautiana. Kwa kila eneo Kunguru wa eneo hilo husika huwa na lugha yao. Kwa maana kuwa kunguru huwa na sauti moja ila namna ya utoaji wa sauti hizo hutofautiana kati ya Kunguru wa eneo moja hadi jingine. Watu wanaoishi na kunguru maeneo yao wataelewa zaidi point hii.

5. Kunguru huuzunikia na kuaga mwili wa maiti ya Kunguru mwenzao. Jambo hili ni nadra sana kwa viumbe wengine hasa aina nyingine ya ndege. Mara kadhaa Kunguru wameshuhudiwa kukusanyika kwa wingi hadi kwa makumi na mamia katika eneo ambapo kuna mwenzao kafia.

6. Kunguru huchelewa sana kuoza akifa. Na hata kuoza kwao huchukua muda mrefu na taratibu sana tofauti na viumbe wengine. Hapa ndipo huja ile dhana ya wengi kufikiri kunguru hawaozi ila kumbe sivyo!.

7. Hawa jamaa ndiyo ndege pekee mwenye ubongo mkubwa kuliko ndege mwingine yeyote.

8. Wanauwezo na ujuzi mzuri wa utatuzi wa changamoto mbalimbali. Inaelezwa kuwa wanaweza pia kutumia zana tofauti tofauti kufanikisha matakwa yao. Viumbe wengine wanaofaamika kutumia nyezo ni binadamu, Orangutans, Chipanzee na sokwe.

View attachment 3011888
 

Attachments

  • d0ea2c8ec7451815593405e8ee7c392c.mp4
    8.6 MB
Naongezea Toka nizaliwe sijawahi kula nyama tamu kama ya kunguru
images (25).jpeg
images (26).jpeg
 
Kunguru wanamakusudi saana. Nakumbuka mwaka mmoja nipo chuo. Katikati ya chuo kulikuwa na mti mrefu chini kunavimbweta. Sasa mfano mnafanya group assignment, mmejikussanya mnaangalia PC, mwamba anaachia pale pale kwenye PC pyaaaa,
 
Back
Top Bottom