Unajua zinaa na uzinzi vinabeba baraka zako?

Unajua zinaa na uzinzi vinabeba baraka zako?

Pdidy

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2007
Posts
57,951
Reaction score
32,619
Nitakujuza tu yoyote unayemvulia chupi ama suruali yako kama sio mkeo wa ndoa kitendo cha kuingiza dudu lako kwake nikujuze anaondoka baraka zako

Haijalishi amevaa hajavaa condom nitakujuza NDUGU pambana na roho ya uzinzi

Watu wengi sana walikuwa matajiri wakajifanya wajanja Leo ni masikini wakutupa

Nikujuzee tu usije furahia kumwaga zile manii ni kwamba zinaenda na baraka zako...

Wanaume wengi wanateseka leo hii kupata watoto wanahisi wamelogwa hakuna ni Ile mizigo uliyokuwa ukiifakamia enzi hizo...

Amkeni
Amkeni
Amkeni vijana, sio muda wa kufanya na kupanua mapaja YENU nyie madada wanaume wengine wanawaingiza Wana Pepo la kutozaa kuanzia asili ya ukoo wao

Wewe ukifurahia kumwagiwa mananii na mapepo yao ya ukoo yanafurahia tumepata tasa mwingine

Muwe makini MKIWA kijana jilindeni mkiona jilindeni zaidi

Maisha n haya haya hayarudi mara mbili......
All d best
 
Ukimtazama mwanamke kwa tamaa ya kulala nae maana yake umezini naye ......kwa muktadha huo kila siku tunazini na kila siku tunapoteza baraka zetu maana yake kila siku tunalaaniwa maana yake kila mtu amelaaniwa maana yake hakuna mwenye baraka maana yake......
 
NJIA 7 UNAZOWEZA KUZITUMIA ILI KUEPUKA DHAMBI YA UZINZI.

Imeandikwa...

" Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.."

( 1 Wakorintho 6:18-20)

〰️ Lakini Maandiko hayakuishia hapo yakasema pia..

"Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalo mwangamiza nafsi yake"
( Methali 6:32 )

〰️ Kusudi la mwili wako sii kwa Ajili ya Ngono au kufanya mapenzi, katika hili Maandiko yalitukumbusha kwa kusema .....

" Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, .... Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe"
( Wimbo ulio bora 2:7 )

""Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na MUNGU? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni MUNGU katika miili yenu"
( 1 Wakorintho 6: 19-20)


**** ZIFUATAZO NI NJIA 7 AMBAZO UNAWEZA KUZITUMIA KATIKA KUEPUKA DHAMBI YA NGONO AU KUFANYA MAPENZI KABLA YA NDOA. (Dhambi ya uzinzi)

️⃣ Shinda vita yako akilini kwa kusoma Neno la MUNGU

〰️ Dhambi ya ngono huanzia akilini kwa kuifikiria, Ili uishinde vita yako akilini. Jifunze kuijaza akili yako kwa Neno la MUNGU.Kama kijana Ikiwa akili yako utaijaza kwa neno la MUNGU, Fikra zako wakati wote zitadumu katika kuimarisha uhusiano wako na MUNGU kwa muongozo wa Roho Mtakatifu na wala si kwakufikiria dhambi ya ngono.

Imeaandikwa....
" Nimewaandikia ninyi vijana, kwa Sababu mna nguvu, na neno la MUNGU linakaa ndani yenu nanyi mmemshinda yule muovu.
( 1 Yohane 2:14 )

2️⃣ Uchaguzi wa marafiki wazuri.

Imeandikwa....
" Enenda Pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu ataumia."
( Methali 13:20 )

Kuna usemi unasema nieleze rafiki zako nami nitakwambia tabia yako, usemi huu una maana ya kuwa idadi ya marafiki uliona huwakilisha tabia yako. Ikiwa una marafikia 4 wadangaji, malaya au makahaba nawewe utakuwa mdangaji, Malaya au kahaba wa 5.
Marafiki wana ushawishi mkubwa wa tabia yako, Ikiwa wewe ni Mkristo jifunze kuchagua marafiki watakao kuwa na mchango mkubwa katika mambo ya kiroho au safari yako ya kiimani.
Jifunze kuchagua marafiki ambao fikra zao Wala mawazo yao hayapo katika kuongelea wala kuwaza ngono zembe.
Ikiwa utaishi na marafiki wenye nia na malengo sawa na wewe itakuwa vyepesi kwako kuzishinda tamaa za mwili wako katika dhambi ya kufanya mapenzi kabla ya Ndoa.

3️⃣ Jifunze Kuwa Busy Na Mambo Muhimu.

Kuna usemi mmoja unasema.....
" An idle mind is the devil's workshop".
(Akili isiyo na Kazi ni karakana ya Shetani)

Ikiwa utaishi maisha yako bila ratiba, Ikiwa utaishi maisha yako bila malengo, Ikiwa utaishi maisha yako bila kuwa na kitu Cha kufanya au kazi ya kufanya. Basi, Shetani atakutumia ili utimize kusudi na malengo yake.

Imeandikwa..
"Mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya BWANA"
( Waefeso 5: 16-17)

Kama kijana Ikiwa utakuwa busy kwa kufanya kazi na kwa kufikiria mambo muhimu ya maisha yako, hizo fikra za kuwaza ngono au kufanya mapenzi kabla ya Ndoa huwezi kuzipita. kwa Sababu, akili yako na mwili wako utakuwa umeshachoka tayari, na hautokuwa tayari kufanya Chochote zaidi ya kupumzika au kupata utulivu.

4️⃣ Usijiruhusu kuwa katika maeneo yenye vishawishi au katika maeneo ambayo mawazo ya kufanya ngono yanaongelewa zaidi.

Imeandikwa....

"Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema. Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui MUNGU"
( 1 wakorintho 15: 33-34)

5️⃣ Jiepushe na vitabu, magazeti, picha, au Tovuti na magroup katika mitandao ya kijamii yanayochochea kufanya ngono.

Imeandikwa..
" Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia,......Maana kila kilichomo duniani, yaani tamaa ya mwili, na tamaa ya macho na kiburi cha uzima, havitokani na BABA, bali vyatokana na dunia."
( 1 Yohane 2: 15-16)

6️⃣ Jenga uhusiano wa uwajibikaji na wazazi wako, wazazi wako wakiroho, Watumishi wa MUNGU waaminifu, na marafiki wenye nguvu za Ukristo ndani yao. Unapopitia wakati wa jaribu, wajulishe na uwaombe msaada wa mawazo, ushauri na maombi.

7️⃣ Mtume Paul alishauri kuwa.." Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe...'
( 1 Wakorintho 7 )

Ikiwa umri wako wa kuoa au kuolewa umefika basi Tafuta mtu huku ukimtanguliza MUNGU kwa maombi akuongozee, ili umpate wa kufanana na wewe Kama alivyo ahidi. Ili uepukane na dhambi ya NGONO au kufanya mapenzi kabla ya Ndoa...

MWISHO....

" KAMA VIJANA, MUNGU NA ATUSAIDIE ILI TUISHINDE DHAMBI HII. KUNA NGUVU KUBWA YA USHINDI AMBAYO MUNGU KAIWEKA NDANI YAKO, IKIWA UTAAMINI NA KUIISHI HAKUNA LISILOWEZEKANA KATIKA YEYE ATUTIAYE NGUVU"

Ubarikiwe sana kwa masomo mengine karibu
👇👇

View: https://youtu.be/Im-XnldBVTI
👆👆
 
Dhambi ya uzinzi ndio dhambi pekee ambayo mwanadamu hawezi kuishinda, ndo maana ukawekwa utaratibu kila mtu awe na partner wale. Ndo maana imeandikwa
1 Wakorintho 7
Neno: Bibilia Takatifu
Kuhusu Ndoa
7 Na sasa kuhusu mambo mliyoniandikia. Ni vizuri mtu asioe. 2 Lakini kwa kuwa dhambi ya zinaa imeenea, kila mwanamume awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke awe na mume wake mwenyewe.

Unaona hata Mungu hapendi tuoe ila kwakua uzinzi hatuwezi kuushinda basi tukapewa utaratibu wa kuoa
 
SOMO: JINSI YA KUSHINDA DHAMBI YA UASHERATI NA UZINZI KATIKATI YA KIZAZI CHA ZINAA

1 Wakorintho 6:18
Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.

Dhambi ya uasherati na uzinzi ndiyo dhambi inayoongoza kuwaangusha watu wengi kiroho, na kihuduma! Ni dhambi ambayo inapeleka watu wengi motoni
Hosea 5:4
Matendo yao hayatawaacha kumgeukia Mungu wao; maana roho ya uzinzi imo ndani yao, wala hawamjui BWANA.

Uasherati na uzinzi ndo dhambi pekee ambayo mwanadamu ameambiwa aikimbie maanake ni dhambi ambayo mtu ukiishaifanya madhara yake ni makubwa!!
1 Wakorintho 6:18
Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.

Note: uasherati ni kufanya tendo la ndoa kabla kuoa au kuolewa, na uzinzi ni wanandoa kufanya tendo la ndoa na mtu ambaye sio mke wake au mme wake:

NINI MAANA YA KUFANYA UASHERATI
biblia imesema kwa watu tuliokoka kuwa uasherati usitajwe kwetu
Waefeso 5:3
Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;

Kufanya uasherati sio mpaka ushiriki tendo la ndoa kama wengine wanavyofikiria lakini kuna vitendea kazi vya uasherati ukiwa navyo tiyari wewe ni mwasherati!
HIVYI HAPA NI VITENDEA KAZI VYA UASHERATI /uzinzi
1: suruali zote kwa mwanamke ,nguo vupi za kuonyesha mapaja, nguo za mipasuo, nguo za makwapa wazi, nguo za kuacha matiti wazi, hivyi vyote ni vitendea kazi vya uasherati, maanake mtu anapokuwa na vyitu hivyi huyo mtu kibiblia ni mwasherati
Mithali 7:10
Na tazama, mwanamke akamkuta, <br>Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;

2: mwanamke ambaye anaweka, wanja, lipstick, nywele bandia, kucha bandia nk! Huyo ni mwasherati na mzinzi hata kama hafanyi tendo hilo
2 Wafalme 9:30
Hata Yehu alipofika Yezreeli, Yezebeli akapata habari; akatia uwanja machoni mwake, akapamba kichwa chake, akachungulia dirishani.

Yeremia 4:30
Na wewe, utakapotekwa, utafanyaje? Ujapojivika mavazi mekundu, ujapojipamba mapambo ya dhahabu, ujapojitia wanja machoni, unajifanya kuwa mzuri bure tu; wapenzi wako wanakudharau; wanakutafuta roho yako.

3: mwanaume yeyote anayevaa suruali za kuchora mwili wake, anayeaacha kifua wazi na anatembea mbele za watu, unyoaji wa kiduku, au kupunguza nywele sehemu moja ya masikio na kuacha zingine katikati ya kichwa huo ni uasherati na uzinzi

4: kuwa mpenzi wa michezo yote yenye roho ya kikahaba ndani yake, mfano mipira, movies, series,mziki na sherehe za kidunia zenye mambo ya kikahaba ndani yake huo ni uzinzi na uasherati( ukahaba)
1 Wakorintho 6:16
Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.

5: kibiblia hatuna neno mpenzi wangu huyu tutakuja kuoana baadaye, ndugu yangu kama umeokoka na una boyfriend au girl friend na uhusiano huo mnauendeleza kimya kimya, mnachati mda wote, huo ni uasherati na mnachokifanya ni kuyamsha mapenz kabla ya wakati, na mtaenda motoni msipoacha, watu waliokoka hawana boyfriend wala girl friend, mda ukifika wa mtu kuoa utaratibu wa watu waliokoka unajulikana,
Wimbo Ulio Bora 2:7
Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe.

5: kukaa watu wawili wa njisia tofauti sehemu za faragha, au gizani au mnatembea pamoja na mmeshikana mikono kama mke na mme huo wote ni uasherati na uzinzi, tuliokoka tunamipaka yetu
Waefeso 5:3
Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;

Watu wengi wataenda motoni sio kwa sababu walifanya uzinzi na uasherati ni kwa sababu walishiriki kazi za uasherati na uzinzi( dhambi za kutokujua)
Na hili kundi ni wengi, wengi ni makahaba japo hawafanyi ukahaba, Ndugu yangu Mungu akusaidie kulijua hili

Mahakamani hawakuhukumu tu kwa sababu umeua wanaangalia mpaka na mazingira ya kuua, yawezekana ushishiriki kuua moja kwa moja lakini ukahukumiwa kwa kutengeneza mazingira ya kuua, ndivyo na Mungu wetu alivyo yawezekana kweli uzizini lakini kupitia kuvaa suruali ya kubana umewaingiza wengi kwenye tamaa!!
Luka 17:1
Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake!

Luka 17:2
Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa.

JINSI YA KUSHINDA DHAMBI HII YA UASHERATI NA UZINZI
swala la kushinda dhambi hii ni la mtu mwenyewe aliyeamua kutoka moyoni, biblia imesema mtii Mungu mpingeni shetani Naye atawakimbia, ukitaka kushinda dhambi ya uzinzi na uasherati fanya yafuatayo

1: acha vitendea kazi vya uasherati na uziniz, vyote ambavyo nimevitaja hapo juu!
2: usiruhusu wazo la uzinzi kufanya kazi kwenye akili yako, pamoja na kuokoka kwako lakini shetani atakujaribu kwa kukuletea wazo la uzinzi kwenye akili yako, mfano atakukumbusha uzuri wa mchepuko wako uliyemuacha, uzuri wa girl friend,au boyfriend wako uliwaacha kwa sababu ya kuokoka, wanawake uliotembea nao,au wanaume , wazo hilo linapokuja jaribu kulikemea na kutoliruhusu kufanya kazi,
Yakobo 1:14
Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.

Utakaporuhusu hilo wazo na kuwaza mda mrefu mwisho wa siku litakomaa na likishakomaa litazaa dhambi, ndo unakuta unaanguka dhambini
Yakobo 1:15
Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.

Shetani akijua umeokoka utakutana na wanawake ambao wamevaa vibaya, nguo za kubana, nguo fupi nk! Ukishamwangalia mara moja wazo mbaya litakuja linakuambia mwangalie tena, ndugu yangu kama mnapishana usigeuke kumwangalia nyuma!! Wanaume wengi wamenaswa kwa kuvutwa kuangalia makalio ya wanawake waliovaa vibaya, ukigeuka tu ndo unaanza kulikomaza hilo wazo mwisho wa siku utamtamani na ukishamtamani umezini tiyari

3: kwenye mitandao ya kijamii mfano facebook nk! huko pia utajaribiwa utafungua tu unakutana na mwanamke yupo uchi au mwanaume, au picha za kikahaba! Zipite haraka usiruhusu macho yako kuangalia mara mbili, ndugu yangu ukiiangalia mara ya pili hizo picha maanake tiyari ndo unaenda kujinasisha mwenyewe mwishowe utajikuta unavaliwa na nguvu ya kikahaba na unaanguka dhambini

4: kwenye TV pia epuka kuangalia mara ya pili vipindi vya kiuasherati mfano ndo unabadilisha channel ghafula unaweka labda mfano tbc ile kuweka unakutana na singeli, ondoa mara moja usiingalie mara mbili mbili
Marko 7:21
Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,

Marko 7:22
wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.

Marko 7:23
Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi.

Ndugu ukiweza kufanya hayo yote na mengineyo kadri Roho wa Mungu atakavyokuongoza dhambi ya uasherati na uzinzi utaishinda huko ndiko tunaita kujitesa nafsi
2 Petro 2:8
maana mtu huyu mwenye haki akikaa kati yao, kwa kuona na kusikia, alijitesa roho yake yenye haki, siku baada ya siku, kwa matendo yao yasiyo na sheria;

Yawezekana ndugu wewe pamoja na kuimba kwako umewakosesha wengi kwenye ufalme wa Mungu, usifikiri utapona na wewe, haijalishi wewe ni mchungaji,nabii, mtume, muinjilisti, mwalimu nk,,
Mathayo 18:6
bali atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio, yamfaa afungiwe shingoni jiwe kubwa la kusagia, na kutoswa katika kilindi cha bahari.
 
MADHARA YA DHAMBI YA UZINZI NA UASHERATI•

JE, WAJUA MADHARA YA KUTENDA DHAMBI YA UZINZI AU UASHERATI HATA UKITUBU NA KUSAMEHEWA?

KUHUSU SEX..

NI KWELI UTATUBU LAKINI MAMBO HAYA YATABAKI KWAKO DAIMA...! 👇👇

Vijana wengi sasa (waliokoka) wana fanya SEX wakat wa mahusiano (kabla ya ndoa), na huku Mioyoni mwao wanasema tukifanya Tutatubu.

Ni kweli utatubu na kama Toba yako ni ya KWELI Mungu Atakusamehe lakini mambo haya hayataondoka hata kama Utatubu.

1️⃣HOFU YA MUNGU KUPUNGUA.

Kwa mara ya kwanza kabla mtu hajafanya sex, huwa na Hofu Moyoni mwake kuhusu dhambi hiyo na Hofu hii humfanya ajilinde na kujitunza.

Lakini Baada ya kufanya Sex, ile Hofu huondoka na badala yake suala la kuvua Nguo linakuwa ni jambo la kawaida tu.

2️⃣KUMBUKUMBU KUBAKI KICHWANI.

Ukishafanya sex, utatubu lakini kuna muda yale matukio ya tendo hilo yatakuwa yanarudi kwenye ufahamu wako mara kwa mara.

Kumbukumbu hizi huwa hazifutiki na ndio maana wengi hujikuta wakizini tena baada ya KUTUBU.

3️⃣UJASIRI WA KUFANYA UONGEZEKA.

Mtu aliyefanya uzinzi ni rahisi zaidi kurudia kufanya tena, Ukweli ni kwamba lile tendo lina Raha ila ubaya unakuja tu pale linapofanyika kinyume na UTARATIBU.

Na kwa sababu ulifanya ukatubu, na haukuona madhara yoyote yaliyokupata zaidi ya Burudani uliyopata hivyo unaona urudie Tena, kujipa raha Zaidi.

Lakini Biblia inasema mshahara wa dhambi ni MAUTI

Warumi 6:23
Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.

4️⃣KUKOSA NGUVU YA KUJIZUIA.

Baada ya kufanya Sex, Nguvu ya kujizuia USIFANYE tena hupungua na yamkini kufa kabisa.

Tangia hapo utakuwa ni mtu wa kuanguka na kasimama, kuanguka na kusimama. Unakuwa sawa na mji usio na Ukuta, nyumba isiyo na milango mwizi ni RAHISI kuingia au sawa na gari linalotembea bila ya Breki.

Ni wachache sana waliofanya halafu wakasimama kikamilifu bila kuanguka tena hasa pindi wanapokuwa kwenye uhusiano ambao unawafanya wakutane mara kwa mara.

5️⃣KUMBUKUMBU KUBAKI VICHWANI MWA WATU.

Unapoanguka kwenye dhambi ya UZINZI na watu wakafahamu basi dhambi hiyo haitafutika Katika FIKRA za watu hata Ukifa.

Mpaka Leo tunasoma dhambi ya Daudi alipozini na mke wa Uria, ingawa Daudi alitubu, akasemehewa na TAYARI ameshakufa lakini dhambi hiyo bado ipo HAI inaishi kwenye vichwa vyetu na mpaka kwa wajukuu zetu bado watasoma na kusikia

Mbali na Mimba, mgonjwa ya zinaa na kupoteza Ujana Wako (bikira) Baada ya kufanya Sex, hayo tuliyoona ni MADHARA ya KUDUMU ambayo huweka KOVU Katika Maisha yako LISILOFUTIKA.

MITHALI 6 : 32-33

Mithali 6:32
Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.

Mithali 6:33
Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika.

1 Wakorintho 6:18
Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.


🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
 
Sisi ndio wale tunaopiganiwa na Bwanaa
 
Uzinzi huwezi kuushinda hata kidogo, ni dhambi itakayokufuata siku zote....hata ufanyaje huishindi. Tutadanganyana tu humu ndani lakini jibu wote tunalijua.....unachotakiwa ni ku-balance uzinzi basi sio kuuacha
 
Watu wangu wanaanngamia kwa kukosaa maarifaaaaaaa
 
Back
Top Bottom