Braza Kede
JF-Expert Member
- Nov 1, 2012
- 3,840
- 6,844
Hawa wamba ndio walikuwa wakileta burdani sana enzi hizo hamna Facebook Instagram Tiktok wala Youtube.
Unavyokaribia mwanzo wa mwaka mnasubiri kwa hamu toleo la jarida jipya lililobeba katuni zilizojaa visa na vitimbi vya hao wamba. Mwanzo wa mwaka kama hivi jarida linakuwa tayari limeshatoka na sasa waja mna-enjoy tu mwaka mpya na mambo mapya.
Hapo unakuta Dr love pimbi huyu alikuwa kifupi kama stuli lakini mara zote unakuta harakati zake ni kufukuzia vimwana wasio saizi yake hasa akimfukuzia huyu tandam anaitwa Zena, Zena yeye ni tandam alikuwa na bifu zisizoisha na kimbaumbau Betina na mititi yao isiyoisha kila uchao kiasi cha kushikana mwilini, Betina alikuwa mkorofi na mjuvi wa kutupa ndonga wakikutana ilikuwa lazima Zena akae.
Lodilofa, ni baba mwenye bonge la mkitambi wake akimiliki kigari chake ki-bettle na mara nyingi hupendea kuvaa shati moja kuubwa la vipande vitatu linalomeza kitambi chake chote. Huyu bwana kuna siku kapigwa mkono na trafiki akaambiwa awashe taa za gari yake. Yeye akaishia kumjibu yule trafiki "lete giza"🤣 bila kumsahau madenge akiwa na vitendeakazi vyake rungu na manati yake.
Kulikuwa na mechi kali sana kati ya bush starz wakiongozwa na mshambuliaji wao kipenzi mapung'o wakicheza na wenzao mabon town🤣Hizi mechi zilikuwa na visa vingi sana vya kuchekesha.
Ooh....Time flies!
RIP Maestro John Kaduma na wote waliotutangulia mbele za haki
Unavyokaribia mwanzo wa mwaka mnasubiri kwa hamu toleo la jarida jipya lililobeba katuni zilizojaa visa na vitimbi vya hao wamba. Mwanzo wa mwaka kama hivi jarida linakuwa tayari limeshatoka na sasa waja mna-enjoy tu mwaka mpya na mambo mapya.
Hapo unakuta Dr love pimbi huyu alikuwa kifupi kama stuli lakini mara zote unakuta harakati zake ni kufukuzia vimwana wasio saizi yake hasa akimfukuzia huyu tandam anaitwa Zena, Zena yeye ni tandam alikuwa na bifu zisizoisha na kimbaumbau Betina na mititi yao isiyoisha kila uchao kiasi cha kushikana mwilini, Betina alikuwa mkorofi na mjuvi wa kutupa ndonga wakikutana ilikuwa lazima Zena akae.
Lodilofa, ni baba mwenye bonge la mkitambi wake akimiliki kigari chake ki-bettle na mara nyingi hupendea kuvaa shati moja kuubwa la vipande vitatu linalomeza kitambi chake chote. Huyu bwana kuna siku kapigwa mkono na trafiki akaambiwa awashe taa za gari yake. Yeye akaishia kumjibu yule trafiki "lete giza"🤣 bila kumsahau madenge akiwa na vitendeakazi vyake rungu na manati yake.
Kulikuwa na mechi kali sana kati ya bush starz wakiongozwa na mshambuliaji wao kipenzi mapung'o wakicheza na wenzao mabon town🤣Hizi mechi zilikuwa na visa vingi sana vya kuchekesha.
Ooh....Time flies!
RIP Maestro John Kaduma na wote waliotutangulia mbele za haki