Unakumbuka visa vya wamba hawa lodilofa madenge ndumilakuwili cmrd kipepe dr love pimbi zena & betina

Ilikua kulikosa gazette la Sani ni kama kukosa mbingu, unasoma unamuazimisha Ndugu Jamaa na marafiki zako, likirudi unalisoma tena!
 
Ilikua kulikosa gazette la Sani ni kama kukosa mbingu, unasoma unamuazimisha Ndugu Jamaa na marafiki zako, likirudi unalisoma tena!
kabisa aisee lilikuwa halichoshi ukimaliza kusoma unalihifadhi ulisome kwa siku zijazo. akija mgeni unamtolea asome🤣muda unakimbia sana.
 
kabisa aisee lilikuwa halichoshi ukimaliza kusoma unalihifadhi kusoma siu zijazo. akija mgeni unamtolea asome🤣muda unakimbia sana.
Jamaa anasimulia Hadi na wewe unajikuta uko live, yaani yalikua kama matukio halisi kabisa.

Sasa kuna wale Jamaa wa mtaani, anawakusanya kijiweni na yeye anaanza sasa kusimulia, hahahahahha na chumvi Kibao. Ole wako ukutane na msimuliaji awe mchaga.
 
Kuna huyu mjomba ndumila alikua mwizi sana afu ana rafiki yake sokomoko mlevi sana, dah aisee umetukumbusha miaka ya 2005 afu kulikua na mjomba nchumali, ukitoka hapo kulikua na simulizi ya mzee OLE na OBI na demu mmoja Alikua anaitwa Linda na tajari mmoja alikua anaitwa MAYUKU
 
Bush Stars kabla ya mechi lazima wafanye tambiko. Utakuta jamaa wako kwenye sufuria kubwa kama chini kuna moto kama vile wanapikwa. Kuna mechi walikipiga na Man U ya kina Giggs, Scholes, Beckham na wengine... kipindi cha pili akaingia mzee Meko aliyekuwa ametoka South Africa. Mzee Meko ndo aliyeifungia Bush Stars na kushinda hiyo mechi dhidi ya Man U. Kwenye pitch majamaa yanatukanana tu.
 
Mchoraji Chris Katembo, mtunzi Ibra Radi Washokera. Unakutana na riwaya za kusisimua kama Msako wa Mr.X, Msako wa Hayawani na Eddie Ganzel. Huko unakutana na watabe kama kina Mark Steven Chenje. Ilianza Sani baadae wakaja Bongo. The return of James Akeke na Fortunatus Ndila alikua akijiita 4T Ndila
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…