Unamkumbuka Deborah Mwenda wa Radio Tanzania?

Unamkumbuka Deborah Mwenda wa Radio Tanzania?

Tamu ya michezo ya radio ili kamilishwa wakiwemo watu hawa, mzee Ibrahim Raha(mzee Jongo),Ali Keto,Hamisi Tajiri,Mangushi,Mzee Kipara,Mama Hambiliki,Zena Dilip,Batholomeo Milulu, na hao hao uliwakuta kwenye mahoka, pwagu na pwaguzi ni ubunifu tu wa kucheza na sauti ila redio ili kuwa zaidi ya tv za sasa kwa vichekesho sio hawa macomedian wetu wa kutoa mimacho sijui kingwendu na wengine kubinjua midomo na visauti vya ajabu ajabu.
 
Mtangazaji mwenzie na huyu Deborah Mwenda aitwae Sarah Dumba katangulia mbele ya haki.
Nakumbuka sana hivi vipaji sijui nani ila nawa wakumbuka sana kina Abdul Masoud(kutangaza mpira),Bati Kombwa,Athumani Magoma,Juma Ngondae,Tumbo Tamimu,Nelly Mkeremi,Suleiman Hegga,Athumani Ngalawa,Stephen Mlatie,Enock Ngombale,Tido Mhando,Chama Omari Matata,Salim Seif Nkamba,Sekione Kitojo,Abisai Stephen, wengi wame tanguli Mungu awa Rehemu na kuna walio hai ila vilikuwa ni vichwa.
 
Na Aloisia Maneno
Hapana. Aloisia Maneno bado yuko hai. Hata kwenye huu msiba wa Sarah Dumba yeye Aloisia Maneno ni mmoja wa watu waliomzungumzia marehemu enzi za uhai wake na akakiri kwamba marehemu ndiye aliyemfundisha kuandaa kipindi cha watoto cha Cheichei Shangazi. Wengine waliomzungumzia marehemu ni pamoja na watangazaji wa zamani Abdul Ngarawa na Halima Kihemba.
 
Hapana. Aloisia Maneno bado yuko hai. Hata kwenye huu msiba wa Sarah Dumba yeye Aloisia Maneno ni mmoja wa watu waliomzungumzia marehemu enzi za uhai wake na akakiri kwamba marehemu ndiye aliyemfundisha kuandaa kipindi cha watoto cha Cheichei Shangazi. Wengine waliomzungumzia marehemu ni pamoja na watangazaji wa zamani Abdul Ngarawa na Halima Kihemba.
Ahsante kwa ufafanuzi mkuu
 
Back
Top Bottom