Elections 2010 Unamuunga mkono Dr. Slaa kugombea URAIS mwaka 2010? Jiandikishe hapa

Elections 2010 Unamuunga mkono Dr. Slaa kugombea URAIS mwaka 2010? Jiandikishe hapa

Binafsi ningependa kuona Dr.Slaa akigombea,kwa kweli tuna ombwe la uongozi

hata hivyo,mwenywewe amesema hatagombea Urais,ingawa akibadilisha msimamo ,i will move heaven and earth to support him
 
Mkuu Luteni,
Wana siasa siku zote huwa wanasema Ahhh, sitaki, ahh hadi nimuulize mke wangu. Ni nchi chache sana ambazo kuna hiyo tabia ya kuanza kampeni mapema na kusema wazi kabisa ntagombea. Hata Kikwete sasa alikuwa akisema hivyohivyo. Kasema nini Dr. Slaa hilo si muhimu. Kwanza tunataka kuona anajiamini bila kujali kama atakosa kura au vipi. Kwani Karatu alianza vipi hadi akashinda? Tena huko alianza akiwa hata hafahamiki. Sasa hivi Dr. Slaa ni jina kubwa na ningelitegemea sasa awe msemaji kutoka CHADEMA kwenye hili swala la Wafanyakazi. Ni kipindi cha kutumia Lugha mbaya ya viongozi wa CCM na kujifagilia.

CCM hawajawahi kupata upinzani mkubwa kiasi hiki. Sasa wamekuwa kama Simba aliyejeruhiwa na wako tayari kumrarua mtu yeyote. Ila ukikutana na Maboxer wazuri kama Mohammed Ali au Johnson, ndiyo kwanza watazidi kukutukana kuwa ".... he wee vipi, mama yako anapiga zaidi kuliko wewe...." Sasa wewe zidi kuchukia na rusha makonde ovyo na uchoke. Hapo anakutwanga kama mtoto mdogo. Atakayekuwa Mvumilivu wa Kupokea mapigo ndiye atashinda.

Mwisho hii listi ni kutaka tu kumuonyesha kuwa tuko wengi wenye imani naye. Tanzania ni nchi ya Demokrasia. Na ni hilo leo hii tunalilaani na hivyo hatuwezi kumshambulia wala kumlazimisha mara akikataa. Kumbuka maneno ya jana ya Kikwete ya Mbayuwai kuwa "Akili za kuambiwa na changanya na akili zako......" Huyu nii Dr. wa sheria na nina imani muono wake utakuwa hata juu zaidi yetu sisi. Angelikuwa na imani na misimamo ya Watanzania ninaamini angeligombea na akamshinda Kikwete. Ila sisi ni Kigeugeu sana.

Clinton aliwaambia Wanyarwanda kuwa "mkikaa kujadiliana, hakuna uhakika mtaafikiana ila msipokaa basi hakuna kuafikiana". Na sisi tunapojaribu kuweka listi, hakuna uhakika kama Dr. Slaa atakubali ila TUSIPOJARIBU basi tuna uhakika kabisa kuwa HATAGOMBEA.
Well Sikonge bado naamini Dr. atatusaidia kwenye mambo mengine tofauti na urais, ni hazina kubwa kwa vijana tusii expose sana ikayeyuka, ukiona adui yako anakushangilia jua kuna walakini some where, hebu fikiria kwa nini sisiem wanasema hawaoni mwingine zaidi ya Slaa? ukifikiria kwa makini mantiki yao is divide and rule they want to import to people's mind that Chadema is nothing but Slaa.
 
Lets see if u get to a million.. Acheni kichaa even if the total members of JF vote hapati ata 4%..lol Muacheni bungeni, miaka mingine mitano CCM will be weak enough to get a significant percentage of the vote. This is not a movie people, progress is a slow process especially if you are under a large pile of crap as we are now. So acheni upinzani wajijenge, msiwajaze vichwa maji mwishoe vibasti CCM washangilie kwa Champagne.

Asiyekubali kushindwa si mshindani. Kashafumua SIRI kibao na ma SKENDO kibao Tanzania. Kuna kilichobadilika? Inabidi sasa Dr. Slaa aende hatua moja mbele. Mwanzo wa ngoma ni lele. Unatudharau kuwa tuko 4% siyo? Yale yale ya kusema Wafanyakazi wako laki tatu na nusu. Ila tuna ndugu, jamaa na marafiki na tukianza kampeni za nyumbani, zinaweza kuwa na nguvu zaidi ya unavyodhani.

Ahh, hiyo ya acheni kichaa, una bahati leo siku nzuri maana ningelikuambia neno la Kikuli wa bandarini.
 
Bila shaka natakiwa kuwa juu ya list....
Sio tu nataka Dr.Slaa agombee Urais the the sake of it...
Hii ni nafasi MOJA tu ya mgombea tofauti na nafasi za Wabunge ambazo zipo zaidi ya 200. Umuhimu wa mtu huyu mmoja unachukua nafasi kubwa ya ushindi wa Wabunge 150 ambao ndio pekee wanaweza kuleta mabadiliko bungeni..Kukosekana kwa mtu mmoja ktk ushindi hakuwezi kuleta mabadiliko bungeni haswa ukizingatia kwamba CCM will make sure wanashinda zaidi ya nusu.. Uchaguzi Zanzibar ni alama tosha kuwakumbusha madudu ya C CM.
Ushindani kwa JK ni muhimu sana ukizingatia tawala za nchi za Kiafrika - Winner takes all ina maana zaidi ya ushindi wa majimbo.
 
Lets see if u get to a million.. Acheni kichaa even if the total members of JF vote hapati ata 4%..lol Muacheni bungeni, miaka mingine mitano CCM will be weak enough to get a significant percentage of the vote. This is not a movie people, progress is a slow process especially if you are under a large pile of crap as we are now. So acheni upinzani wajijenge, msiwajaze vichwa maji mwishoe vibasti CCM washangilie kwa Champagne.
I agree with you but not at red, ulivyosema kwenye red ni sawa na JK alivyosema hata wafanyakazi laki tatu wakimnyima kura atashinda tu hajui impact ya hao laki tatu kuwa wanawakilisha wapigakura wangapi.
 
Bila shaka natakiwa kuwa juu ya list....
Sio tu nataka Dr.Slaa agombee Urais the the sake of it...
Hii ni nafasi MOJA tu ya mgombea tofauti na nafasi za Wabunge ambazo zipo zaidi ya 200. Umuhimu wa mtu huyu mmoja unachukua nafasi kubwa ya ushindi wa Wabunge 150 ambao ndio pekee wanaweza kuleta mabadiliko bungeni..Kukosekana kwa mtu mmoja ktk ushindi hakuwezi kuleta mabadiliko bungeni haswa ukizingatia kwamba CCM will make sure wanashinda zaidi ya nusu.. Uchaguzi Zanzibar ni alama tosha kuwakumbusha madudu ya C CM.
Ushindani kwa JK ni muhimu sana ukizingatia tawala za nchi za Kiafrika - Winner takes all ina maana zaidi ya ushindi wa majimbo.

Mkuu Mkandara tupo kwenye NJIA MOJA na ombi lako limetekelezwa kwa kukuweka wa Kwanza. Ila tu nimeweka namba 1. kwa mwenyewe Dr. Slaa na wewe nimeshakuweka namba mbili na hii haitabadilika.
 
please DR Slaa gombea tafadhali









Selous nataka pia lakini isingekuwa Karatu Dr. Sllaa asingekuwepo na huenda hataki lile jimbo lirudi CCM kwa udi na uvumba.
Nitakachomwezesha Dr kugombea urais sio nini wala nini ni haya yafuatayo kama sio abishe;
  • Mbadala kwa CCM pale karatu, naamini akijitokeza mwanaCHADEMA mwingine mwenye nguvu wa kukabili kishindo cha CCM atakuja kutuliza kiu yetu,
  • Hofu ya kupoteza jimbo na imani pekee aliopewa na wanakaratu.... Nilipita pale nikafanya ka test kidogo.... acha huyu mtu anaheshimika pale aka Willy or Father
 
Kama Dr. Slaa agombee urais wa JF mimi naona anafaa sana...nchi si lelemama nyie...Obama keshaota mvi tele kwa stress.
 
Dr.Slaa wana-usirudie makosa ya Mbowe... Ikiwezekana hamna haja ya CHADEMA kumsimamisha mgombea URAHISI... Kila mtu ajikite jimboni mwake...
Cha muhimu ni kuharibu kura za Mkwere... Ndio MKWERE...yeye si ametuita Mbayu-wayu Loh!!!
 
Mkuu, una majina mawili nini? Naona umechanganya mambo. Nashindwa kukuandika kwenye listi kwa sababu umeweka jina tofauti na jina lako la JF



Mkuu Luteni,
Wana siasa siku zote huwa wanasema Ahhh, sitaki, ahh hadi nimuulize mke wangu. Ni nchi chache sana ambazo kuna hiyo tabia ya kuanza kampeni mapema na kusema wazi kabisa ntagombea. Hata Kikwete sasa alikuwa akisema hivyohivyo. Kasema nini Dr. Slaa hilo si muhimu. Kwanza tunataka kuona anajiamini bila kujali kama atakosa kura au vipi. Kwani Karatu alianza vipi hadi akashinda? Tena huko alianza akiwa hata hafahamiki. Sasa hivi Dr. Slaa ni jina kubwa na ningelitegemea sasa awe msemaji kutoka CHADEMA kwenye hili swala la Wafanyakazi. Ni kipindi cha kutumia Lugha mbaya ya viongozi wa CCM na kujifagilia.

CCM hawajawahi kupata upinzani mkubwa kiasi hiki. Sasa wamekuwa kama Simba aliyejeruhiwa na wako tayari kumrarua mtu yeyote. Ila ukikutana na Maboxer wazuri kama Mohammed Ali au Johnson, ndiyo kwanza watazidi kukutukana kuwa ".... he wee vipi, mama yako anapiga zaidi kuliko wewe...." Sasa wewe zidi kuchukia na rusha makonde ovyo na uchoke. Hapo anakutwanga kama mtoto mdogo. Atakayekuwa Mvumilivu wa Kupokea mapigo ndiye atashinda.

Mwisho hii listi ni kutaka tu kumuonyesha kuwa tuko wengi wenye imani naye. Tanzania ni nchi ya Demokrasia. Na ni hilo leo hii tunalilaani na hivyo hatuwezi kumshambulia wala kumlazimisha mara akikataa. Kumbuka maneno ya jana ya Kikwete ya Mbayuwai kuwa "Akili za kuambiwa na changanya na akili zako......" Huyu nii Dr. wa sheria na nina imani muono wake utakuwa hata juu zaidi yetu sisi. Angelikuwa na imani na misimamo ya Watanzania ninaamini angeligombea na akamshinda Kikwete. Ila sisi ni Kigeugeu sana.

Clinton aliwaambia Wanyarwanda kuwa "mkikaa kujadiliana, hakuna uhakika mtaafikiana ila msipokaa basi hakuna kuafikiana". Na sisi tunapojaribu kuweka listi, hakuna uhakika kama Dr. Slaa atakubali ila TUSIPOJARIBU basi tuna uhakika kabisa kuwa HATAGOMBEA.
Nkwingwa...nami natofautiana nawe...Dr.Slaa akigombea kitakachotkea ni changamoto tu...piga ua mshindi atakuwa wa CCM,na akishindwa atakuwepo tu...upinzani bungeni utakuwa umelala doro....Ni vema akajipanga akagombea mwaka 2015 na mgombea wa CCM ambaye atakuwa ni mpya kwa kipindi hicho...yeye agombee tu ubunge mwaka huu ili ashinde na kuzidi kuleta changamoto na uhai wa opposition bungeni....Naomba agombee tu ubunge wa Karatu...Mbilinge mbilinge zake za bungeni bado zahitajika sana...pale anakuwa na uhuru sana wa kuongea na kuibua yasiyoibulika...Ningependa sana kumuona akiingia ulingoni 2015...Ni ushauri tu
 
Alpha

Just get rid of CCM. Enough is Enough, the country cannot afford five more years of these corrupt, incompetent fools.
 
labda huyu dr. Slaa anatakiwa kuamshwa. Nimeona tufanye sensa ya haraka haraka humu ndani ya jf. Kwa wale wote wanaoona dr slaa agombee mwaka huu basi hebu jiandikishie jina lako tuone mwisho wa wiki tutakuwa wangapi. tujitokeze kwa wingi ili kumuonyesha dr. Slaa anavyohitajika.

Dr. Slaa, samahani nimeamua kuanzia jina lako kwa makusudi kabisa maana jemadari lazima awe mbele na wengine watafuata.

1. Dr. Slaa 2. Mkandara 3. King of kings 4. Masanilo kugema 5. Fidel80

6. Bht 7. Tanzania 8. Ndege ya uchumi 9. Jiwe 10. Jakathesi

11. Technician 12. Kilembwe 13. Ndjabu da dude 14. Bollo yeng 15. Selous

16. Nyamizi 17. Mfwatiliaji 18. Sikonge 19. Ben 20.
21. Muhindi
 
Kama Dr. Slaa agombee urais wa JF mimi naona anafaa sana...nchi si lelemama nyie...Obama keshaota mvi tele kwa stress.
Junius unataka kuharibu uzuri wa thread urais wa bongo si sawa na wa US kule wanapima uwezo wa mtu kufikiri na kupambanua mambo urais wa Tanzania hata Kikwete anaweza bora liende.
 
Wakuu zangu,
Nitarudia maneno niliyoyasema mwaka 2005 baada ya Uchaguzi.
Kulingana na mazingira ya nchi za Kiafrika Kiti cha Urais ni muhimu sana kuliko position yeyote ile na itachukua ushindi wa Rais kuweza kubadilisha katiba, mfumo wa Utawala na hata kupunguza nguvu za rais.. Ni rais anayeweka sahihi mabadiliko ya aina yeyote kisheria..Muswada hauwezi kuwa act pasipo rais kuanguka..Akikataa kuweka sahihi kazi inarudi palepale kama haya maandamano. mtalalamika weee, hakuna kitakachobadilika. Hizi kelele za Bungeni tumeziona toka enzi ya NCCR -Mageuzi na hakuna policy yoyote iliyobadilika kwa sababu ya mawazo ya mbunge mmoja. Hata kama Dr.Slaa hatakuwepo bungeni watakuja kina Dr.Slaa wengine kuwakilisha mawazo ya Dr.Slaa. haikatazwi kwa Dr kusukuma hoja bungeni kupitia mbunge wake iwe Zitto au Mbowe..
Tumechoka na umaarufu, sasa hivi ni wakati wa kuishambulia CCM toka kona zote. Wahenga husema siri ya vita vyovyote ni kwanza muue Jenerali, utakuwa umeshinda vita. Ni maumbile ya viumbe wote duniani kumwondoa mtawala iwe nyuki, Simba au sisimizi. Hata Mapinduzi watu hulenga kwanza Ikulu na sii Bungeni.
Hivyo ifahamike kwamba tunachozungumzia hapa ni Mapinduzi ya Utawala uliopo.. Sii swala la kumwondoa JK madarakani. Huyu ni mtumishi tu wa chama ambaye tumeona kiburi akiwa mwajiri mkuu wa serikali, Mhimili tuliomkabidhi sisi wananchi kuungoza leo amekuwa kiongozi dhidi ya waliomwajiri..
Statement ya JK kuhusiana na wafanyakazi inatisha hasa anaposema hahitaji kura za Wafanyakazi... Haya ni maneno mazito sana ktk nchi yenye kutumia demokrasia na inabidi JK aombe msamaha! zipo lugha za kutumia lakini sii hii hata kidogo..
Nakumbuka hata Dr. Slaa mwenyewe kasema inabidi arudie kuisoma taarifa hiyo kwani haamini maneno hayo yamesemwa na kiongozi wa nchi aliyechaguliwa kwa kura. Na hii ni moja ya silaha kubwa ya mgombea dhidi ya JK kuwakumbusha wananchi hasa Wafanyakazi.

JK uongozi wa nchi umemshinda, hilo halina ubishi.. hata kina Yakhe sie tulokuwa na matumaini na mtoto wa Saigon tumebakia kushika matama yetu hatuamini kilichomtoa Kanga huyu manyoya. Hakika mgomo wa wafanyakazi ktk nchi maskini kama yetu inatisha sana lakini yeye kama Presidaa alitakiwa kulishughulikia hili miaka mitatu iliyopita badala yake zimeongezwa gharama ambazo hazikuwa na msingi wowote..Baraza la Mawaziri, Ndege na magari Mapya Ikulu, Chai na ongezeko la posho kwa mawaziri na viongozi wa serikali. Sasa hivi hata Madiwani na Halmashauri zinapewa fungu kubwa toka bungeni.. Hizi zote ni fedha za wananchi ambao wanalalamika kukatwa kodi kubwa ili kuendesha serikali hii..Sasa maswala kama haya tumsubiri Dr.Slaa hadi arudi bungeni jamani!
Ifike wakati nasi tuwe na mtu wa kuzungumza nje ya bunge..
 
Kama Dr. Slaa agombee urais wa JF mimi naona anafaa sana...nchi si lelemama nyie...Obama keshaota mvi tele kwa stress.

Junius,
Sikufahamu kwa hiyo sintakuhukumu. Ila jambo moja ambalo nina uhakika kabisa ni kuwa Dr. Slaa ni mtu pekee aliyepo hapa JF kwa sasa kama MBUNGE na anatumia jina lake halisi. Huo ni ujasiri tosha na hasa ukichukulia kuna watu wengine wenye maneno kama wamepata juice ya tende kama yako hapo juu. Siyo lazima uchangie kila kitu. Nilivyoona unajadili swala la Muungano nikafikiri una upeo mkubwa sana ila ghafla yakaanza ya Karume alikuwa hajui kusoma, hajui Kiingereza (Mmalawi na baharia huyoo hajui Kiingereza) na maswala mengine, nimeanza kukufahamu kwa ukaribu. Endelea kujifunua. Ila jambo moja tu ni kuwa kama Wanaotaka UHURU wa Zanzibar watu wenyewe ndiyo kama nyie, basi kweli naweza kukubaliana na Nyerere kuwa "nyie watu jamjakomaa kujitawala". Hebu onyesheni kukua basi kidogo hata kwenye majadiliano ya kawaida kabisa.

Wakati watu wanajadili mambo mengine, wewe unakuja na mambo ya RAIS wa JF, nakuona sawa kabisa na huyu Mzee hapa chini:
attachment.php
 
Back
Top Bottom