Unapodai risiti dukani na kupewa yenye kiasi pungufu kuliko hela uliyolipa unachukua hatua gani ?

Hatuoni matumizi ya Kodi zetu, ndo maana tupo tayari kupotezwa

Binafsi Huwa sidai risti
 
Kodi imekuwa kubwa kama mwelewa unawaelewa tu wanyonge wenzio.
 
View attachment 3185121

Dukani unaambiwa bidhaa ni kiasi flani na unalipia

unawakumbusha risiti, wanakutolea yenye kiasi pungufu
Kuna wakati hii nchi unaona bora ukwepe kodi au ushirikiane tuu na wakwepa kodi maana matumizi ya hizo fedha serikalini zinatia hasira , watu wana fuja tu wabunge wanajipitishia miposho mikubwa wakati hawana kazi yeyote ya kuwachosha zaidi ya kujuchekesha na kugonga meza bungeni wakati watumishi wachini huku wanalipwa pesa kidogo sana na kazi wanayo wafanya ni kubwa sana, hizo pesa wanafuja haswaa na ndio zinatumika kuhonga wana siasa na kulipa machawa, ndio zinawalipa wanao teka watanzania wenzetu na kuwaua na kuwajeruhi , wananunua migari ya kutembelea wao ya mabilioni wakati watoto wanakaa chini na madawa hakuna , pesa zinahonga vilabu vya mipira wakati mambo ya msingi kabisa hayajitosheleI , kwakweli bora nikwepe kodi angalau itanirudia mwenyewe
 
Ananirudishia pesa yangu / narudisha bidhaa yake
Kipi bora ale mtanzania mwenzio muuza duka au iende serikalini ikawalipe wasio julikana kwa kuteka na kuua watanganyika wenzio ndani ya gari la 300milion lililo nunuliwa na kodi hiyo hoyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…