Unapolipa deni kumbuka haya (M-pesa, Tigopesa, Halopesa nk)

Unapolipa deni kumbuka haya (M-pesa, Tigopesa, Halopesa nk)

Mi nikikopa kwa mtu hua napiga hesabu ya pesa aliyokatwa wakati ananitumia, pesa atakayotolea na pesa nyingine ya soda ili siku nikikwama asisite kunikopesha.
Ukifanya hivi huwezi kugombana na watu.
Ingawa inaumiza kwa gharama lakini hakuna namna.
 
Nazungumzia namna ya kulipa deni ulilorushiwa kwa M-pesa, Tigopesa, halopesa nk. Katika maisha ni kawaida kukwama na kuomba marafiki watunasue na kamkopo.

Mtu anakukopa tuseme laki tano. Unamrushia kwa mpesa (yaweza kuwa mtandao mwingine wowote) laki tano na elfu kumi ili apate na ya kutolea na atimize shida yake ya laki tano.

Kimbembe kinakuja wakati wa kulipa. Jamaa anakurushia laki tano kamili juu ya alama.

Anasahau ile elfu kumi na ada yako ya kumtumia hela. Mbaya Zaidi, bado huwezi kuitoa laki tano yote lazima ukatwe ya kutolea. Kwa wema au tuseme ujinga wako, unaingia hasara ya elfu 15 hadi 20. Hivi akiwa na shida tena utamkopesha mtu wa aina hii?
Ukilipwa hata bila ya kutolea wewe shukuru maana siku hizi kulipa deni ni mtihani kweli kweli.
 
Mkuu kutuma pesa kwenye mtandao hasara huwa haikwepeki ni bora kupata hasara ya makato kuliko kupata hasara mara mbili ya makato na yakutolea
Tanzania nchi yetu, ina Mambo ya ajabu sana, tunapenda vitu vya ajabu ajabu hatutumiii bank ambazo ni chipu na tunafata simu ambazo ni expensive
 
Kwani ndugu zanguni tatizo NI kiasi ulichonikopesha au ile Ada ya kutuma na kutolea??Kama NI pesa ya kutolea basi nikopeshe Kwanza laki Tano then muda wa kulipa niwe nakutumia ile ya kutolea kwanza
 
Nazungumzia namna ya kulipa deni ulilorushiwa kwa M-pesa, Tigopesa, halopesa nk. Katika maisha ni kawaida kukwama na kuomba marafiki watunasue na kamkopo.

Mtu anakukopa tuseme laki tano. Unamrushia kwa mpesa (yaweza kuwa mtandao mwingine wowote) laki tano na elfu kumi ili apate na ya kutolea na atimize shida yake ya laki tano.

Kimbembe kinakuja wakati wa kulipa. Jamaa anakurushia laki tano kamili juu ya alama.

Anasahau ile elfu kumi na ada yako ya kumtumia hela. Mbaya Zaidi, bado huwezi kuitoa laki tano yote lazima ukatwe ya kutolea. Kwa wema au tuseme ujinga wako, unaingia hasara ya elfu 15 hadi 20. Hivi akiwa na shida tena utamkopesha mtu wa aina hii?
Kama ni pisi Kali, namkopesha tena kiroho safi!
 
Back
Top Bottom