Kutoka Mirembe
JF-Expert Member
- Mar 7, 2014
- 294
- 87
- Thread starter
-
- #21
Nakuelewa vizuri sana! Kwa mtazamo wangu, elimu yetu inatufundisha woga wa maisha badala ya kutufungua na kutuwezesha kukabiliana na changamoto za kila siku maishani.
Mfano mdogo tu, mtu mwenye elimu ya kawaida yuko ki halisia zaidi (more practical) kuliko mtu mwenye shule kubwa japo sio wote. Laiti tungepewa mtihani wa kuulizwa na watoto umefanya nini leo kazini, kuna watu wangeshundwa kujibu licha ya kwamba kila siku wanaenda kazini na wanalipwa mishahara mikubwa. Nasema watoto ili uweze kumweleza akuelewe unachokifanya kwa sababu mtu mzima ata jifanya amekuelewa hata kama kimsingi hujamshawishi kile unachokifanya unapokua kazini.
Mathalani, ma cashier kwenye ma benki wangelipwa pesa nyingi kwa sababu kazi yao inatambulika na kila mtu kuanzia aliyeenda shule hadi asiyejua kusoma. Kuna watu watakwambia sijui strategies, hawezi quantify kwa siku amefanya kitu gani tangible lakini mishahara ndio hiyo lumbesa.
Ndio maana tumekua na vijana wanaotafuta namna ya kupata mishahara mikubwa bila ya kujali kama watakua na uwezo wa kuzifanya hizo kazi zenyewe, mwisho wa siku ni frustration kibao.
Elimu ni nzuri sana kama itatafutwa kwa lengo la kuongeza uwezo na maarifa ya kukupatia ujasiri na maarifa ya kutatua matatizo yako na yanayoizunguka jamii kwa ujumla.
Nafurahi kuwa Jf na member kama wewe!
Kuna linalo weza kufanyika kufanya elimu yetu more practical?
Cc mpigamsuli
Last edited by a moderator: