Unatumia njia gani kumpata mshauri wa mambo unayopitia?

Unatumia njia gani kumpata mshauri wa mambo unayopitia?

Joined
Jun 12, 2022
Posts
5
Reaction score
8
Watu wengi huwa tunaomba ushauri kwa watu mbalimbali ili watusaidie pale tunapohitaji, lakini ikitokea tumegombana na wale waliotupa ushauri, tunazikuta siri zetu nje ya hapo.

Sasa wewe unatumia njia gani kumpata mshauri anayefaa?

Kuna baadhi huwa tunawachukua marafiki kama washauri ila kibaya ni kuwa kuna mambo huyavutia kwake, yaani kama unamshirikisha kuhusu mahusiano yako na kumbe yeye anampenda mwenzako, hivyo unaweza kujikuta amekupa ushauri ili muachane ili yeye aingie.

Na baada ya hapo anaweza kutumia kusema siri zote ulizokuwa unamwambia kuhusu mpenzi wako, na anajikuta anatengeneza uadui na mpenzi wako.

Unatumia njia gani kumpata mshauri?

Mimi ili mtu anishauri huwa napenda kuangalia vitu vifuatavyo:-
A. Ujuzi wake kwenye masuala ninayohitaji ushauri.

B. Kama mtu ameshawahi kupitia hilo ninalopitia. Kwani watu wanavyokupa wewe ushauri huwa wanajiongelea wao kuhusu mambo waliyopitia

C. Kifua cha kuficha mambo, kama ni rafiki yangu na ananipa ushauri nitaangalia je huwa ananiambia kuwa nani na nani aliwashauri, kama huwa ananipa siri za wengine siri zangu siwezi kumwambia acha niubebe mzigo wangu.

D. Mwanasaikolojia wa suala husika, kama shida yangu ni ya kisaikolojia basi nitatafuta mshauri mwenye uwezo wa kushauri kisaikolojia.

Rafiki pekee uliyebaki naye ni yule adui yako, maana rafiki yako ni adui yako ajae...

Vijana tuepuke kutoa siri za wapenzi wetu kwa marafiki zetu, usimshirikishe kila kitu rafiki yako, angalia uwezo wa kutunza siri.

Ni bora kuonekana mbaya kwa mwanzo lakini huku umemfichia siri mpenzi wako.

Kuna mahusiano yanakufa mapema kwa sababu mpenzi anatangazwa kwa marafiki zake.

Kila mtu ana agenda za siri sehemu yoyote.

Sasa wewe unatumia njia gani kumpata mshauri wa mambo yako na anayekubebea siri?
 
Mimi sijui nipoje aisee.

Jambo langu kukuambia ni ngumu hata kama napitia kipindi kigumu kiasi gani nitakomaa tu na litapita.
Yakinishinda kabisa afadhali niwashirikishe wazazi wangu ila rafiki hell no.

Watu hawana vifua kabisa wewe unamweleza na yeye anaigeuza story ya kuwaambia wenzie.

Mimi mambo yangu huwa napenda yawe siri mana kuna mambo haipendezi watu kuyajua.

Kwanza sina rafiki bali watu tuliozoeana tu.

Rafiki ambaye tulikuwa tunawezana yupo mbali na sijaona kama yeye tena.

Nina mmoja tumezoeana ila ukimweleza jambo linamuwasha lazima aseme sasa sijui wale wanaomweleza huwa wanajiamini nini.
 
Mimi sijui nipoje aisee.
Jambo langu kukuambia ni ngumu hata kama napitia kipindi kigumu kiasi gani nitakomaa tu na litapita.
Yakinishinda kabisa afadhali niwashirikishe wazazi wangu ila rafiki hell no.
Watu hawana vifua kabisa wewe unamweleza na yeye anaigeuza story ya kuwaambia wenzie.
Mimi mambo yangu huwa napenda yawe siri mana kuna mambo haipendezi watu kuyajua.
Kwanza sina rafiki bali watu tuliozoeana tu.
Rafiki ambaye tulikuwa tunawezana yupo mbali na sijaona kama yeye tena.
Nina mmoja tumezoeana ila ukimweleza jambo linamuwasha lazima aseme sasa sijui wale wanaomweleza huwa wanajiamini nini.
Wanasema kuna madhara ya kukaa na mambo magumu bila mshauri!!
Hata kama hawaamiki ila unahitaji mtu wa kumwambia....

Kuna njia mbalimbali unaweza kutumia ukiona watu hawana kifua,

Tumia kama unamsimulia stori ya mtu fulani alafu usikie ushauri wake utakusaidia...

Kuna mambo mengine ni magumu sanq, usipopata ushauri kuna watu hupoteza maisha yao....

Mambo magumu ni kama sumu kifuani mwetu . Tunahitaji angalau namna ya kusikia maneno ya watu
 
Wanasema kuna madhara ya kukaa na mambo magumu bila mshauri!!
Hata kama hawaamiki ila unahitaji mtu wa kumwambia....

Kuna njia mbalimbali unaweza kutumia ukiona watu hawana kifua,

Tumia kama unamsimulia stori ya mtu fulani alafu usikie ushauri wake utakusaidia...

Kuna mambo mengine ni magumu sanq, usipopata ushauri kuna watu hupoteza maisha yao....

Mambo magumu ni kama sumu kifuani mwetu . Tunahitaji angalau namna ya kusikia maneno ya watu
Nimeshazoea hiyo hali

Huyu rafiki aliyembali huwa wakati mwingine namweleza ila sio mambo yote.

Halafu kuna ile unaona kama mtu anakuchoka na matatizo yako halafu yeye kama vile hanaga au hakuelezi ya kwako so unajiona labda wewe pia ni tatizo so unajiaskia aibu kumwambia kila unalopitia so mengine unakufa na tai shingoni.

Nikiona maji yanazidi unga nitaleta hata humu waja wanipe ushauri japo humu napo Kuna watu wana roho ngumu badala ya kukupa moyo wanagongelea msumari kwenye kidonda unajikuta umeongezewa stress.
 
Hapo sasa, ukishea na mmoja tu inakuwa vizuri.

Ila wengi wa rafiki zetu ni watu wanaotuona kuwa tunatoa huruma. Na wao ndio watu wanaostahili kukushauri.

Huo sio urafiki na maana yake, rafiki sio kuwa et bila mimi asingefika pale!!!

Rafiki yako awe ni mtu ambaye hajioni bora kuliko wewe, mkiwa pamoja ushauri
 
Wanasema kuna madhara ya kukaa na mambo magumu bila mshauri!!
Hata kama hawaamiki ila unahitaji mtu wa kumwambia....

Kuna njia mbalimbali unaweza kutumia ukiona watu hawana kifua,

Tumia kama unamsimulia stori ya mtu fulani alafu usikie ushauri wake utakusaidia...

Kuna mambo mengine ni magumu sanq, usipopata ushauri kuna watu hupoteza maisha yao....

Mambo magumu ni kama sumu kifuani mwetu . Tunahitaji angalau namna ya kusikia maneno ya watu
Kweli kukaa na mambo moyoni yatakuua mwenyewe
 
Wanasema kuna madhara ya kukaa na mambo magumu bila mshauri!!
Hata kama hawaamiki ila unahitaji mtu wa kumwambia....

Kuna njia mbalimbali unaweza kutumia ukiona watu hawana kifua,

Tumia kama unamsimulia stori ya mtu fulani alafu usikie ushauri wake utakusaidia...

Kuna mambo mengine ni magumu sanq, usipopata ushauri kuna watu hupoteza maisha yao....

Mambo magumu ni kama sumu kifuani mwetu . Tunahitaji angalau namna ya kusikia maneno ya watu
Word up. Asante sana.
 
Back
Top Bottom