All about Tanzania life
Member
- Jul 6, 2023
- 40
- 83
Baada ya pilika pilika za mwezi mzima, siku moja unaweza kupanga kutembelea Wilaya ya Mkurunga Mkoani Pwani na kugundua ziwa moja wapo linalopatikana mkoani hapa.
Hili ni ziwa Mansi, linapatikana takribani kilomita 70 kutoka Dar es Salaam. Sio mbali sana na jiji la Dar es salaam na kama hukuwahi kupita njia ielekeayo kusini mwa Tanzania basi utafurahia kuona idadi kubwa ya miti ya minazi njiani na barabara nyembamba na mfululizo wa majengo ya viwanda mbali mbali kote njiani.
Ukiwa unaelekea huko, kama utatumia usafili wa uma, utapaswa kushukia eneo linaloitwa Mwarusembe, ni rahisi zaidi kulifikia ziwa hilo kama utaanzia kutembea kutokea hapo. Kwa ushauri zaidi kama utaenda kwa shughuli za kitalii ni bora kutembea kwa miguu kutokea hapo Mwarusembe hadi ziwani. Kwanini nashauri hivyo? Ukiwa njiani utaweza kupata fursa ya kuona aina ya nyumba za nyasi zitumikazo kama makazi na utamaduni wa watu wa kabila la wazaramu, kuwa kama sehemu ya mazoezi na kupata utulivu kukatisha katika maeneo tulivu usiyoyazoea.
Binafsi nilijaribu jambo hili na nikiwa njiani nilibahatika kuona mambo mengi na kupata utulivu wa nafsi kutokana na ukimya na utulivu mkuu kote njiani.
Na kama pia unatumia usafiri binafsi unaweza kuchepusha maeneo hayo na kupata uelekeo kirahisi kusogea kukaribia eneo lilipo ziwa Mansi. Ni rahisi kufika huko, lakini kumbuka kusema nataka kufika bwawani, kwa kuwa wenyeji wengi huko hawafahamu kama hilo ni ziwa.
Nini utegemee kukutana nacho? Hapo ndio kwenye kazi sasa. Hili ni ziwa lenye kuzungukwa kwa kiasi kikubwa na uoto asili na mazao ya kupandwa. Kwa sehemu kubwa limegawanyika kwa maeneo yenye maji na maeneo mengi yenye magugu na uoto mwingi.
Huko uvuvi wa kienyeji ufanyika, wavuvi wengi wazawa wa maeneo hayo hujipatia kipato kwa kuvua samaki wanaopatikana ndani ya ziwa hilo. Hivyo ni rahisi kwako kuweza kupata wasaa wa kupanda mtumbwi na kuona mandhali ya ziwa mansi kupitia wenyeji wanaopatikana huko.
Usitegemee kukutana na wageni wengi au watu wengi wanaoenda kutembelea huko, lakini utaweza kuona jambo jipya na kujifunza kitu kipya juu ya uwepo wa ziwa hili katika wilaya hii kubwa ya Mkuranga.
Karibu mkoa wa Pwani karibu kutembelea ziwa Mansi.
#All about Tanzania life 🔴🟠⚪️
Hili ni ziwa Mansi, linapatikana takribani kilomita 70 kutoka Dar es Salaam. Sio mbali sana na jiji la Dar es salaam na kama hukuwahi kupita njia ielekeayo kusini mwa Tanzania basi utafurahia kuona idadi kubwa ya miti ya minazi njiani na barabara nyembamba na mfululizo wa majengo ya viwanda mbali mbali kote njiani.
Ukiwa unaelekea huko, kama utatumia usafili wa uma, utapaswa kushukia eneo linaloitwa Mwarusembe, ni rahisi zaidi kulifikia ziwa hilo kama utaanzia kutembea kutokea hapo. Kwa ushauri zaidi kama utaenda kwa shughuli za kitalii ni bora kutembea kwa miguu kutokea hapo Mwarusembe hadi ziwani. Kwanini nashauri hivyo? Ukiwa njiani utaweza kupata fursa ya kuona aina ya nyumba za nyasi zitumikazo kama makazi na utamaduni wa watu wa kabila la wazaramu, kuwa kama sehemu ya mazoezi na kupata utulivu kukatisha katika maeneo tulivu usiyoyazoea.
Binafsi nilijaribu jambo hili na nikiwa njiani nilibahatika kuona mambo mengi na kupata utulivu wa nafsi kutokana na ukimya na utulivu mkuu kote njiani.
Na kama pia unatumia usafiri binafsi unaweza kuchepusha maeneo hayo na kupata uelekeo kirahisi kusogea kukaribia eneo lilipo ziwa Mansi. Ni rahisi kufika huko, lakini kumbuka kusema nataka kufika bwawani, kwa kuwa wenyeji wengi huko hawafahamu kama hilo ni ziwa.
Nini utegemee kukutana nacho? Hapo ndio kwenye kazi sasa. Hili ni ziwa lenye kuzungukwa kwa kiasi kikubwa na uoto asili na mazao ya kupandwa. Kwa sehemu kubwa limegawanyika kwa maeneo yenye maji na maeneo mengi yenye magugu na uoto mwingi.
Huko uvuvi wa kienyeji ufanyika, wavuvi wengi wazawa wa maeneo hayo hujipatia kipato kwa kuvua samaki wanaopatikana ndani ya ziwa hilo. Hivyo ni rahisi kwako kuweza kupata wasaa wa kupanda mtumbwi na kuona mandhali ya ziwa mansi kupitia wenyeji wanaopatikana huko.
Usitegemee kukutana na wageni wengi au watu wengi wanaoenda kutembelea huko, lakini utaweza kuona jambo jipya na kujifunza kitu kipya juu ya uwepo wa ziwa hili katika wilaya hii kubwa ya Mkuranga.
Karibu mkoa wa Pwani karibu kutembelea ziwa Mansi.
#All about Tanzania life 🔴🟠⚪️