Unaweza kutembelea Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani

Unaweza kutembelea Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani

Mkuranga au mkurunga mi nilifikiri ni mahali kwingine.
Anyway sio ziwa ni bwawa.
Nilipita rouge road kuelekea masaki kuna mlima huko kati niliona hilo bwawa kwa chini
 
Huyu bwana mdogo hajui tofauti ya ziwa na bwawa! Sijui shuleni wanaendaga kufanya
Ukweli ndio huo, hilo ni ziwa na katika idadi ya maziwa madogo kwa makubwa yanayopatikana Tanzania, ziwa Mansi ni mojawapo.
 

Attachments

  • Screenshot_20240704_075119_Chrome.jpg
    Screenshot_20240704_075119_Chrome.jpg
    157 KB · Views: 10
Nilienda mkuranga nikiwa kwenye gari konda anaongea huyo mambo ambayo hapaswi kuongea public, nilivyoshuka nikachukua boda, yule boda njiani ananiambia mambo yake mimi hata simsikii vizuri kwa ajili ya upepo nikabaki kushangaa tu huyu mtu vipi hatujuani lakini ananieleza maisha yake na sijamuuliza, kumbe ndio tabia zao.
Ndio walivyo wote mkuu kama una jamaa yako mtu wa Mkuranga angalia vya kumwambia siku ya kwanza naenda kununua kiwanja,

Nikakutana na mzee muuzaji alinipa habari mpaka za wajukuu zake nikawa najua mjuu wake wa Tanga kaachwa, mwanae wa kiume kazamia kwa kaburu, mkwe wake kawa teja na mambo mengine mengine mengi tu naenda kwa mtendaji huko ndo balaa ananipa stori kuhusu tabia ya mkewe kuunguza samaki na kashamkanya sana

Sijakaa sawa anaingia mgambo wa kijiji akanipa habari nyumbani kwake kuna mchawi🤣🤣🤣
 
Ndio walivyo wote mkuu kama una jamaa yako mtu wa Mkuranga angalia vya kumwambia siku ya kwanza naenda kununua kiwanja,

Nikakutana na mzee muuzaji alinipa habari mpaka za wajukuu zake nikawa najua mjuu wake wa Tanga kaachwa, mwanae wa kiume kazamia kwa kaburu, mkwe wake kawa teja na mambo mengine mengine mengi tu naenda kwa mtendaji huko ndo balaa ananipa stori kuhusu tabia ya mkewe kuunguza samaki na kashamkanya sana

Sijakaa sawa anaingia mgambo wa kijiji akanipa habari nyumbani kwake kuna mchawi🤣🤣🤣
Nmetamani sana kupata shamba mkuranga ila mwenyeji wangu anataka kuhama kumuuliza sababu nini anadai wanga sana😂
 
Ndio walivyo wote mkuu kama una jamaa yako mtu wa Mkuranga angalia vya kumwambia siku ya kwanza naenda kununua kiwanja,

Nikakutana na mzee muuzaji alinipa habari mpaka za wajukuu zake nikawa najua mjuu wake wa Tanga kaachwa, mwanae wa kiume kazamia kwa kaburu, mkwe wake kawa teja na mambo mengine mengine mengi tu naenda kwa mtendaji huko ndo balaa ananipa stori kuhusu tabia ya mkewe kuunguza samaki na kashamkanya sana

Sijakaa sawa anaingia mgambo wa kijiji akanipa habari nyumbani kwake kuna mchawi🤣🤣🤣
Ah ah na wewe ungewapa intro kidogo 😁😁
 
Baada ya pilika pilika za mwezi mzima, siku moja unaweza kupanga kutembelea Wilaya ya Mkurunga Mkoani Pwani na kugundua ziwa moja wapo linalopatikana mkoani hapa.

Hili ni ziwa Mansi, linapatikana takribani kilomita 70 kutoka Dar es salaam. Sio mbali sana na jiji la Dar es salaam na kama hukuwahi kupita njia ielekeayo kusini mwa Tanzania basi utafurahia kuona idadi kubwa ya miti ya minazi njiani na barabara nyembamba na mfululizo wa majengo ya viwanda mbali mbali kote njiani.

Ukiwa unaelekea huko, kama utatumia usafili wa uma, utapaswa kushukia eneo linaloitwa Mwarusembe, ni rahisi zaidi kulifikia ziwa hilo kama utaanzia kutembea kutokea hapo. Kwa ushauri zaidi kama utaenda kwa shughuli za kitalii ni bora kutembea kwa miguu kutokea hapo Mwarusembe hadi ziwani. Kwanini nashauri hivyo? Ukiwa njiani utaweza kupata fursa ya kuona aina ya nyumba za nyasi zitumikazo kama makazi na utamaduni wa watu wa kabila la wazaramu, kuwa kama sehemu ya mazoezi na kupata utulivu kukatisha katika maeneo tulivu usiyoyazoea.

Binafsi nilijaribu jambo hili na nikiwa njiani nilibahatika kuona mambo mengi na kupata utulivu wa nafsi kutokana na ukimya na utulivu mkuu kote njiani.

Na kama pia unatumia usafiri binafsi unaweza kuchepusha maeneo hayo na kupata uelekeo kirahisi kusogea kukaribia eneo lilipo ziwa Mansi. Ni rahisi kufika huko, lakini kumbuka kusema nataka kufika bwawani, kwa kuwa wenyeji wengi huko hawafahamu kama hilo ni ziwa.

Nini utegemee kukutana nacho? Hapo ndio kwenye kazi sasa. Hili ni ziwa lenye kuzungukwa kwa kiasi kikubwa na uoto asili na mazao ya kupandwa. Kwa sehemu kubwa limegawanyika kwa maeneo yenye maji na maeneo mengi yenye magugu na uoto mwingi.

Huko uvuvi wa kienyeji ufanyika, wavuvi wengi wazawa wa maeneo hayo hujipatia kipato kwa kuvua samaki wanaopatikana ndani ya ziwa hilo. Hivyo ni rahisi kwako kuweza kupata wasaa wa kupanda mtumbwi na kuona mandhali ya ziwa mansi kupitia wenyeji wanaopatikana huko.

Usitegemee kukutana na wageni wengi au watu wengi wanaoenda kutembelea huko, lakini utaweza kuona jambo jipya na kujifunza kitu kipya juu ya uwepo wa ziwa hili katika wilaya hii kubwa ya Mkuranga.

Karibu mkoa wa Pwani karibu kutembelea ziwa Mansi.

#All about Tanzania life 🔴🟠⚪️

View attachment 3032900
Umesahau au hujaambiwa kuna chatu wakubwa ambao wanaweza kumeza mtu mzima mzima.

Inatakiwa kuwa makini na nyoka pia ni wengi.

Huko ni kuzuri sana kwa mtu anaetaka kuwekeza kwenye mazao ya nyoka.
 
Ni sehemu nzuri kupata utulivu wa nafsi na kugundua eneo jipya la kujiwekea kumbukumbu zako binafsi. Karibu sana mkuu.
Mkuu bila kusahau ziwa Zakwati lililopo Mkola namna ya kulifikia kwa usafiri wa binafsi kwa njia ya kusini unaipita Kimanzichana na Mkiu unakwenda mbele unakuta kiwanda cha vioo unaendelea mbele si mbali sana unakuta kiwanda cha tailizi cha Goodwill unakipita kwa mbele kidogo unakuta kijiji cha Nyamalonda hapo unaingia kushoto njia ya kwenda Magawa una kwenda hadi Lukanga hapo unaachana na njia ya Magawa una kata kushoto hadi Mkola unakuwa umefika ziwa Zakwati.
 
Kwa muonekano hilo ni ziwa kabisa. Kuanzia ekari tano hilo ni ziwa. Vipi kuhusu mamba na viboko, wapo humo?
 
Ndio walivyo wote mkuu kama una jamaa yako mtu wa Mkuranga angalia vya kumwambia siku ya kwanza naenda kununua kiwanja,

Nikakutana na mzee muuzaji alinipa habari mpaka za wajukuu zake nikawa najua mjuu wake wa Tanga kaachwa, mwanae wa kiume kazamia kwa kaburu, mkwe wake kawa teja na mambo mengine mengine mengi tu naenda kwa mtendaji huko ndo balaa ananipa stori kuhusu tabia ya mkewe kuunguza samaki na kashamkanya sana

Sijakaa sawa anaingia mgambo wa kijiji akanipa habari nyumbani kwake kuna mchawi🤣🤣🤣
😂 kwao hawahitaji kulewa ili kumwaga siri za watu, watoto wakizaliwa maeneo yao kiasili si wanabeba izo tabia pia?

Niliambiwa huko mabinti wadogo sana wanaolewa.
 
Back
Top Bottom