Unawezaje kufanikiwa bila nguvu ya ziada nyuma yako?

Unawezaje kufanikiwa bila nguvu ya ziada nyuma yako?

Mkuu,mbona Ibrahim,Daud na Suleman walikuwa matajiri wakubwa na walimtegemea Mungu?
mwisho wa safari unajua nini kilitokea?suleman alikiri wazi huu ni upuuzi mtupu,wakati ayubu akinyang,anywa kila kitu na kupewa baadae.

halafu mkuu,unajua baada ya agano jipya nini kinaendelea!,zamani hata kuoa wake zaidi ya mmoja ilikuwa ni baraka kutoka kwa Mungu.
 
Hata shetani mwenyewe ni mali ya Mungu, wachungaji ni waongo sana wanachotaka ni kujipatia pesa huku wakiishi maisha ya anasa, changamoto ni kuwa Mungu anataka aabudiwe kwa sababu ni Mungu na sio kwa sababu amekupa kitu fulani, katika mazingira yyte yale, utajiri, umaskini, maradhi, Fadhaa, Tabu, Raha. Na hata kifo , sasa anachotaka imani yako kwake iwe costant katika mazingira hayo yote ndo anakupa utajir,....

Swala linakuja kuwa Utajiri ni sehemu alipojibanza shetani, una changamoto sana za kiimani, mtu akiwa tajiri automaticaly anakuwa subjected na majaribu makali kabisa, ambayo ni vigumu kuyakwepa mara nyingi matajiri huwa wanaturnout kumwabudu Mungu, kitu ambacho Mungu hataki kabisa, na kumbuka mission kubwa ya Mungu ni kukutoa kwenye Ulimwengu huu mana kiuhalisia hakuna raha yoyte na maisha ni unpredictable...na ndio maana fahari kuu ya mkristo ni uzima wa milele na sio kitu kingine, Zaidi ya hapo ni surplus

Sasa ili Mungu akupe utajir unahitajika uonyeshe imani isiyoyumba katika nyakat zote za maisha, za amani na shida, Yusuph baada ya kuonyesha imani dhabiti wakati wa taabu na raha mwisho aliruhusiwa kuwa wazir mkuu wa nchi kubwa zaidi kipind hicho, Ayubu baada ya kuonyesha imani kubwa wakati wa taabu na wakati wa raha arihusiwa kuwa na ukwasi wa hatari. Daniel baada ya kuhustle kuisimamia imani aliruhusiwa kuwa kiongozi wa juu wa mataifa makubwa dunian by that time,
Shida kubwa mtu anataka utajiri ili afanye mambo kinyume na Mungu, awe mzinzi, mlevi, majivuno n.k...kwa mazingira hayo lazima uende kwa mganga tuuu,
Mkuu biblia yenyewe inajitosheleza kukupa Mwongozo achana na wachungaji hao ni wahuni tu na wavivu wa kufanya kazi, wangekuwa watu wa Mungu kwa nini hawapatani
asante mkuu,wewe sio mlokole masuti.
 
Maombi hayawezi kukufanya utajirike bali unaomba Mungu akufungue akili zaidi. Swala la Kufanikiwa ni wewe na wewe. Mungu anakupa afya njema tu.
 
Maana ukishazaliwa na wazazi tu, tayari mtu mwingine kashachangia katika mafanikio yako kwa namna moja ama nyingine.


👆🏻 Sasa hao wazazi walikujaje hapa duniani kama siyo Mungu aliyewaleta (super natural being)

Popote ukimbiliapo huwezi kumkosa Mungu, Yeye ndiye "CAUSA CAUSANS", mwanzilishi wa kila kitu.
 
Mkuu elezea vizuri unajizaaje?
Sijaandika unaweza kujizaa, ningeandika hivyo, swali la unajizaaje lingekuwa sawa sawia kwangu.

Nimeandika unahitaji kujizaa.

Unaweza kuhitaji kurudi mwaka uliokuwa darasa la kwanza lakini usiweze.

Point yangu ni kwamba, hakuna mtu aliyefanikiwa bila kuhitaji msaada wa wengine, kwa sababu kwanza wote tunazaliwa na wengine.

Ili mtu aweze kusema kafanikiwa bila ya msaada wa wengine, itabidi maisha yake yaanze kwa kujizaa mwenyewe, kitu ambacho hakiwezekani kwa sexual reproduction yetu.
 
Point yangu ni kwamba, hakuna mtu aliyefanikiwa bila kuhitaji msaada wa wengine, kwa sababu kwanza wote tunazaliwa na wengine.


Kuzaliwa ndiyo aina moja ya kuumbwa, kwa sababu hatua zote hadi mtoto kuzaliwa hujiendesha (automatically), ni hatua moja tu ndio wazazi uhusika sana nayo ni tendo la ndoa, sasa swali ni hili ni kitu gani kilitengeneza hiyo automatic process ndani ya tumbo la mama hadi mtoto akapatikana, pili je, wazazi na viumbe hai vyote vinavyizaliana vilikuja kwa bahati tu au kuna kitu kilivileta hapa duniani??.

Majibu ya maswali hayo yanampeleka mtu MWENYE AKILI moja kwamoja kwa "Conscious minded being" causa causan ambaye ni Mungu.
 
Nguvu ya mafanikio ni nguvu zako mwenyewe na kuweka aibu pembeni.........wengi tunashindwa kutekeleza zile kazi zinazoweza kutupa mafanikio kwa sababu ya kuona aibu;mfano kuuza karanga kwa kutembeza,kuzibua vyoo n.k
 
Back
Top Bottom