Unawezaje kumtoa machinga katikati ya mji halafu akakae nje ya mji?

Unawezaje kumtoa machinga katikati ya mji halafu akakae nje ya mji?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Nimekuwa nikifuatilia sakata la kuondolewa wamachinga katikati ya miji ili kuwapeleka maeneo maalum pembezoni ya mji. Ni hadithi inayonifanya kucheka sana kila nikiisikia. Kwanza ni jambo lisilowezekana kwa 90% na pili ni hadithi inayojirudia mara kwa mara. Serikali inaweza kuwaondoa wamachinga kinguvu (kwa muda fulani tu) kutoka katikati ya mji lakini haitaweza kuwapeleka kukaa na kudumu kwenye hayo maeneo mapya mbali na katikati ya mji.

Sababu za msingi za jambo hilo kutokuwezekana ni hizi.

1. Asili ya biashara ya umachinga ni kutangatanga, kufuata mikusanyiko ya watu, kudandia wateja barabarani na kusongamana. Mmachinga ni kama kuku wa kienyeji, anaishi vizuri kwa kumuacha azurure mitaani.

2. Wamachinga hawana tatizo na maeneo wanayofanyia biashara sasa, haya maeneo ya barabarani, holela holela na yasiyo rasmi wamachinga ndio wanayataka na wanayapenda sana.
 
Nimekuwa nikifuatilia sakata la kuondolewa wamachinga katikati ya miji ili kuwapeleka maeneo maalum pembezoni ya mji. Ni hadithi inayonifanya kucheka sana kila nikiisikia. Kwanza ni jambo lisilowezekana kwa 90% na pili ni hadithi inayojirudia mara kwa mara. Serikali inaweza kuwaondoa wamachinga kinguvu (kwa muda fulani tu) kutoka katikati ya mji lakini haitaweza kuwapeleka kukaa na kudumu kwenye hayo maeneo mapya mbali na katikati ya mji.

Sababu za msingi za jambo hilo kutokuwezekana ni hizi.

1. Asili ya biashara ya umachinga ni kutangatanga, kufuata mikusanyiko ya watu, kudandia wateja barabarani na kusongamana. Mmachinga ni kama kuku wa kienyeji, anaishi vizuri kwa kumuacha azurure mitaani.

2. Wamachinga hawana tatizo na maeneo wanayofanyia biashara sasa, haya maeneo ya barabarani, holela holela na yasiyo rasmi wamachinga ndio wanayataka na wanayapenda sana.
Siyo kwa serikali sasa.
 
Nimekuwa nikifuatilia sakata la kuondolewa wamachinga katikati ya miji ili kuwapeleka maeneo maalum pembezoni ya mji. Ni hadithi inayonifanya kucheka sana kila nikiisikia. Kwanza ni jambo lisilowezekana kwa 90% na pili ni hadithi inayojirudia mara kwa mara. Serikali inaweza kuwaondoa wamachinga kinguvu (kwa muda fulani tu) kutoka katikati ya mji lakini haitaweza kuwapeleka kukaa na kudumu kwenye hayo maeneo mapya mbali na katikati ya mji.

Sababu za msingi za jambo hilo kutokuwezekana ni hizi.

1. Asili ya biashara ya umachinga ni kutangatanga, kufuata mikusanyiko ya watu, kudandia wateja barabarani na kusongamana. Mmachinga ni kama kuku wa kienyeji, anaishi vizuri kwa kumuacha azurure mitaani.
Basi waliopo na waliohamishwa sio machinga sababu hawa walikuwa hawazururi wala kutangatanga..., tatizo lilikuwa kuacha watu wakavunja sheria kwa muda mrefu mpaka wakadhani ni haki yao kuvunja haki ya mtembea kwa miguu
2. Wamachinga hawana tatizo na maeneo wanayofanyia biashara sasa, haya maeneo ya barabarani, holela holela na yasiyo rasmi wamachinga ndio wanayataka na wanayapenda sana.
Wengi tunapenda vingi, ila hatuvifanyi iwapo vinakinzana na sheria, mipango na utaratibu tuliojiwekea kama jamii
 
Wameshindwa kuwatoa machanguo na wala shisha ambao ni wahalifu wataweza kuwatoa machinga ambao hawamwibii mtu yoyote?

Tatizo huwa hawajifunzi kutokana na historia mkuu wa mkoa wa Dar atashindwa mapema sana.
Hawamwibii mpita njia kwa kunyakua njia yake ya kutembea kwa kujinafasi ?
 
Basi waliopo na waliohamishwa sio machinga sababu hawa walikuwa hawazururi wala kutangatanga..., tatizo lilikuwa kuacha watu wakavunja sheria kwa muda mrefu mpaka wakadhani ni haki yao kuvunja haki ya mtembea kwa miguu

Wengi tunapenda vingi, ila hatuvifanyi iwapo vinakinzana na sheria, mipango na utaratibu tuliojiwekea kama jamii
Sheria ni kwa ajili ya watu.
 
Kwa maneno yako hawa siyo wamachinga, maana walikuwa na mabanda yenye nguo kuwazidi wengi wenye flemu za maduka, Ubungo darajani pale kulikuwa na Banda kubwa anauza Tshirt na Jeans.

Kifupi wengi walijificha kwa jina ya umachinga ila mzigo waliokuwa nao nisawa na wenye maduka
 
Kwa hiyo mamachinga hawawezekaniki ,.?????..

Unataka kusema serikali haitweza kuwatoa hayo maeneo yasiyo rasmi ????...

Unawajaza kichwa na upepo kuwa machinga Wana nguvu kwa hiyo serikali haiwawezi ???


Serikali haijawahi kushindwa ,hao machinga either kwa fimbo ,virungu au bakora watatoka tu hayo maeneo ,na hakuna kitu wanaweza kuifanya serikali .....!

Thread closed
 
Nimekuwa nikifuatilia sakata la kuondolewa wamachinga katikati ya miji ili kuwapeleka maeneo maalum pembezoni ya mji. Ni hadithi inayonifanya kucheka sana kila nikiisikia. Kwanza ni jambo lisilowezekana kwa 90% na pili ni hadithi inayojirudia mara kwa mara. Serikali inaweza kuwaondoa wamachinga kinguvu (kwa muda fulani tu) kutoka katikati ya mji lakini haitaweza kuwapeleka kukaa na kudumu kwenye hayo maeneo mapya mbali na katikati ya mji.

Sababu za msingi za jambo hilo kutokuwezekana ni hizi.

1. Asili ya biashara ya umachinga ni kutangatanga, kufuata mikusanyiko ya watu, kudandia wateja barabarani na kusongamana. Mmachinga ni kama kuku wa kienyeji, anaishi vizuri kwa kumuacha azurure mitaani.

2. Wamachinga hawana tatizo na maeneo wanayofanyia biashara sasa, haya maeneo ya barabarani, holela holela na yasiyo rasmi wamachinga ndio wanayataka na wanayapenda sana.
Kosa si kuwaondoa mjin ila tatiz wanawapeleka ktk maeneo hayana maji, umeme wala vyoo, machinga kukaa barabaran ni fikra mgando na za kimaskin
 
Kosa si kuwaondoa mjin ila tatiz wanawapeleka ktk maeneo hayana maji, umeme wala vyoo, machinga kukaa barabaran ni fikra mgando na za kimaskin
Fikra mgando akakae wapi sasa akae porini auzie nyani bidhaa ama?
 
Fikra mgando akakae wapi sasa akae porini auzie nyani bidhaa ama?
Achukue bidhaa zake mfano jeans,mikanda,Tshirt aweke begani atembeze kwa wapita njia.

Akianza kujenga banda juu ya mtaro,njia ya wenda kwa miguu au mbele ya fremu ya mwenzie huyu mojakwamoja anakuwa sio machinga.

Huyu anatakiwa aondolewe kistaarabu ikishindikana marungu yahusike.
 
Achukue bidhaa zake mfano jeans,mikanda,Tshirt aweke begani atembeze kwa wapita njia.

Akianza kujenga banda juu ya mtaro,njia ya wenda kwa miguu au mbele ya fremu ya mwenzie huyu mojakwamoja anakuwa sio machinga.

Huyu anatakiwa aondolewe kistaarabu ikishindikana marungu yahusike.
Hapa umeeleweka sasa
 
Tusidanganyane hapa,,,Wale ni wafanyabiashara ...machinga gani anauza vitu vina thamani ya milion nne huko....
 
Kwa hiyo mamachinga hawawezekaniki ,.?????..

Unataka kusema serikali haitweza kuwatoa hayo maeneo yasiyo rasmi ????...

Unawajaza kichwa na upepo kuwa machinga Wana nguvu kwa hiyo serikali haiwawezi ???


Serikali haijawahi kushindwa ,hao machinga either kwa fimbo ,virungu au bakora watatoka tu hayo maeneo ,na hakuna kitu wanaweza kuifanya serikali .....!

Thread closed
Logic ni kuwa, umachinga ni shughuli ya kubangaiza na kuzurura ovyo mitaani kuwasaka wateja, hivyo kuwatengea eneo rasmi huo sio umachinga.

Yote kwa yote, umachinga sio shughuli ya kuendekezwa sana, umachinga ni kazi ya kuunga unga ili siku iende, na mwisho wa siku mmachinga anapaswa kuwa mfanyabiashara kamili na sio kuendelea na umachinga muda wote.
 
Back
Top Bottom