figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,724
- 55,906
UNESCO: Wenyeji wa Ngorongoro Wahame. Wafanyakazi wa NCAA na Mahoteli waishi nje ya Hifadhi
Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro si eneo ambalo ni Hifadhi ya Taifa na vile eneo hili la Ngorongoro halipo chini ya shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na badala yake ni shirika huru kama jinsi ilivyo TANAPA likijitegemea kazi na majukumu ya TANAPA na Ngorongoro yanafanana katika kuhifadhi viumbe hai na makazi yake kuwa endelevu kwa ajili ya vizazi vilivyopo na vijavyo.
Lakini kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ni eneo ambalo ni hifadhi mseto ambapo kuna viumbe hai aina tatu vikiishi kwa pamoja ambavyo ni watu ambao zaidi ni jamii ya kabira la wamaasai, mifugo yao kama kondoo, mbuzi na ngo’mbe na wanyamapori.
HISTORIA YAKE:
Sababu ya msingi iliyopelekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ni ukweli wa mambo ya kwamba jamii ya kabila la maasai ilikuwa likiishi katika eneo la Serengeti na Ngorongoro kwa miaka mingi pamoja na wanyamapori.
Wamaasai ni jamii ya nilotiki ambao asili yao ni kusini mwa Sudan na ni jamii ya wafugaji kiasili. Kwa kuwa jamii ya wamaasai ilikuwa ikiishi ndani ya maeneo haya ya uhifadhi pasipo utaratibu maalumu na mwongozo jamii hii ya kabila la wamaasai ilikuwa katika janga kubwa la wanyamapori kama vile magonjwa maambukizo ya wanyamapori na majanga mengineyo.
Hivyo basi serikali ya wakoloni Waingereza wakati wa kipindi hicho iliamua kuanzisha maeneo mawili tofauti ya uhifadhi eneo moja la uhifadhi litumike maalum kwaajili ya uhifadhi wanyamapori pekee ambayo ndio Serengeti ya leo hii na vile vile eneo jingine la uhifadhi llitumike kama Hifadhi mseto ambapo wamaasai wataishi kwa pamoja yaani (Conservation). Hatimaye wamaasai wote waliokuwa wakiishi Serengeti ya wakati wa kipindi kile wakahamishiwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ya leo hii.
Vilevile malengo mengine yalikuwa ni katika kulinda maslahi ya jamii kabila la wamaasai ambao wameishi na wanyamapori pasipo uharibifu wowote ule kwa miaka mingi jamii ya kabila la wamaasai wanachukuliwa kuwa ni wahifadhi asili kwa sababu ya kuishi na wanyamapori kwa muda mrefu kihistoria.
Ikumbukwe naieleweke hapa ya kwamba hifadhi za Taifa zote zilipo chini ya shirika la hifadhi za Taifa (TANAPA) pamoja na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro uanzishwaji wake ulikuwa ni mwaka 1959.
Aprili 17, 2018 ilitambuliwa na Umoja wa Matyaifa kupitia shirika lake la Elimu Sayansi na Utamaduni (Unesco) kuwa hifadhi jiolojia ya Ngorongoro Lengai hivyo kuingizwa kwenye mtandao wa hifadhi zenye hadhi hii duniani. Kijiografia inapatikana mkoani Arusha.
Eneo hilo linajumuisha Bonde la Ngorongoro (Ngorongoro Crater), Engaruka, Selela, Engaresero, bonde la Empakai, mlima Oldoinyo Lengai mlima pekee Tanzania ambao volkani yake bado ni hai, Bonde la Oldupai (Oldivai) sehemu ambayo ni chimbuko la historia ya binadamu.
MIVUTANO NA SULUHISHO
HOJA ZA WENYEJI
*Vibali vya kujenga nyumba za kudumu ndani ya hifadhi
*Wanahitaji faida Zaidi kutokana na Mapato ya Utalii
*Hati Miliki ya Ardhi ndani ya NCA
*Waruhusiwe kulima ndani ya hifadhi
*Wanahitaji kujenga huduma za Kijamii ndani ya Hifadhi
HOJA ZA JAMII
*Wanahitaji marisho katika maeneo yayokatazwa kama Kreta, Northern Highland Forest Reserve (NHFR), eneo oevu la Ndutu)
*Wanahitaji kushirikishwa katika maswala yanayohusu Maamuzi ndani ya Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA)
*Fidia ya Mifugo inayoliwa na Wanyamapori (Compensation for livestock depredation and Human attacks)
*Mipaka Mipya imepunguza ukubwa wa eneo la Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA), hivyo jamii inaomba maeneo yaliyochukuliwa yarudishwe
USHAURI WA UNESCO
Unesco kwa Ujumla wake imeshauri yafuatayo:
*Yafanyike Mapitio ya Mfumo wa Matumizi Mseto ya ardhi ya hifadhi ya eneo la Ngorongoro ambao kwa sasa umebainika kushindwa kufanya kazi ipasavyo
*Kuhamasisha uhamaji wa wenyeji kutoka eneo la hifadhi kwa kutoa Motisha kwa wenyeji ili waweze kuhama. Aidha UNESCO inashauri kuhamisha Wafanyakazi wa Taasisi ya Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA) na Wafanyakazi wa Mahoteli ili waishi nje ya eneo la Hifadhi
Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro si eneo ambalo ni Hifadhi ya Taifa na vile eneo hili la Ngorongoro halipo chini ya shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na badala yake ni shirika huru kama jinsi ilivyo TANAPA likijitegemea kazi na majukumu ya TANAPA na Ngorongoro yanafanana katika kuhifadhi viumbe hai na makazi yake kuwa endelevu kwa ajili ya vizazi vilivyopo na vijavyo.
Lakini kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ni eneo ambalo ni hifadhi mseto ambapo kuna viumbe hai aina tatu vikiishi kwa pamoja ambavyo ni watu ambao zaidi ni jamii ya kabira la wamaasai, mifugo yao kama kondoo, mbuzi na ngo’mbe na wanyamapori.
HISTORIA YAKE:
Sababu ya msingi iliyopelekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ni ukweli wa mambo ya kwamba jamii ya kabila la maasai ilikuwa likiishi katika eneo la Serengeti na Ngorongoro kwa miaka mingi pamoja na wanyamapori.
Wamaasai ni jamii ya nilotiki ambao asili yao ni kusini mwa Sudan na ni jamii ya wafugaji kiasili. Kwa kuwa jamii ya wamaasai ilikuwa ikiishi ndani ya maeneo haya ya uhifadhi pasipo utaratibu maalumu na mwongozo jamii hii ya kabila la wamaasai ilikuwa katika janga kubwa la wanyamapori kama vile magonjwa maambukizo ya wanyamapori na majanga mengineyo.
Hivyo basi serikali ya wakoloni Waingereza wakati wa kipindi hicho iliamua kuanzisha maeneo mawili tofauti ya uhifadhi eneo moja la uhifadhi litumike maalum kwaajili ya uhifadhi wanyamapori pekee ambayo ndio Serengeti ya leo hii na vile vile eneo jingine la uhifadhi llitumike kama Hifadhi mseto ambapo wamaasai wataishi kwa pamoja yaani (Conservation). Hatimaye wamaasai wote waliokuwa wakiishi Serengeti ya wakati wa kipindi kile wakahamishiwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ya leo hii.
Vilevile malengo mengine yalikuwa ni katika kulinda maslahi ya jamii kabila la wamaasai ambao wameishi na wanyamapori pasipo uharibifu wowote ule kwa miaka mingi jamii ya kabila la wamaasai wanachukuliwa kuwa ni wahifadhi asili kwa sababu ya kuishi na wanyamapori kwa muda mrefu kihistoria.
Ikumbukwe naieleweke hapa ya kwamba hifadhi za Taifa zote zilipo chini ya shirika la hifadhi za Taifa (TANAPA) pamoja na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro uanzishwaji wake ulikuwa ni mwaka 1959.
Aprili 17, 2018 ilitambuliwa na Umoja wa Matyaifa kupitia shirika lake la Elimu Sayansi na Utamaduni (Unesco) kuwa hifadhi jiolojia ya Ngorongoro Lengai hivyo kuingizwa kwenye mtandao wa hifadhi zenye hadhi hii duniani. Kijiografia inapatikana mkoani Arusha.
Eneo hilo linajumuisha Bonde la Ngorongoro (Ngorongoro Crater), Engaruka, Selela, Engaresero, bonde la Empakai, mlima Oldoinyo Lengai mlima pekee Tanzania ambao volkani yake bado ni hai, Bonde la Oldupai (Oldivai) sehemu ambayo ni chimbuko la historia ya binadamu.
MIVUTANO NA SULUHISHO
HOJA ZA WENYEJI
*Vibali vya kujenga nyumba za kudumu ndani ya hifadhi
*Wanahitaji faida Zaidi kutokana na Mapato ya Utalii
*Hati Miliki ya Ardhi ndani ya NCA
*Waruhusiwe kulima ndani ya hifadhi
*Wanahitaji kujenga huduma za Kijamii ndani ya Hifadhi
HOJA ZA JAMII
*Wanahitaji marisho katika maeneo yayokatazwa kama Kreta, Northern Highland Forest Reserve (NHFR), eneo oevu la Ndutu)
*Wanahitaji kushirikishwa katika maswala yanayohusu Maamuzi ndani ya Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA)
*Fidia ya Mifugo inayoliwa na Wanyamapori (Compensation for livestock depredation and Human attacks)
*Mipaka Mipya imepunguza ukubwa wa eneo la Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA), hivyo jamii inaomba maeneo yaliyochukuliwa yarudishwe
USHAURI WA UNESCO
Unesco kwa Ujumla wake imeshauri yafuatayo:
*Yafanyike Mapitio ya Mfumo wa Matumizi Mseto ya ardhi ya hifadhi ya eneo la Ngorongoro ambao kwa sasa umebainika kushindwa kufanya kazi ipasavyo
*Kuhamasisha uhamaji wa wenyeji kutoka eneo la hifadhi kwa kutoa Motisha kwa wenyeji ili waweze kuhama. Aidha UNESCO inashauri kuhamisha Wafanyakazi wa Taasisi ya Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA) na Wafanyakazi wa Mahoteli ili waishi nje ya eneo la Hifadhi