UNGEKUWA WEWE UNGEFANYA MAAMUZI GANI..

Pure_sapiens

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2016
Posts
2,228
Reaction score
2,064
Habari zenu ndugu.Tukiwa tunaokaribisha mwezi wa ramadhani ni vizuri kutakiana mfungo mwema na Allah atufanyie wepesi katika funga zetu.
Ni hivi ni kama wiki tatu tangu tumefiwa na mfanyakazi mwenzetu.Huyu mfanyakazi mwenzetu tuliishi nae vizuri hapa kazini hivyo baada ya kiso chake ofisi iliamuwa kurudisha kwao mwili wa marehemu,kwao ni Sumbawanga.Kama ilivyoada ikabidi kazini watoke japo wafanyakazi kadhaa ili kupeleka msiba,tunashukuru kwani wenzetu wawili walikubali kwenda na msiba Sumbawanga.katika msafara huo kuna dereva,Mwanamke 1 na mwanaume 1 pamoja na mwili wa marehemu.Yapata wiki tatu sasa tangu waende msibani ila wakati wa kurudi gari lao Limepata matatizo hivyo ni ngumu kurudi nyumbani kwao.
MSAADA WENYEWE NI HAPA...
Yule Mwanamke ni mke wa mtu na mme wake tunafanya kazi ofisi moja.Sasa Mme wake hana furaha kabisa tangu kuondoka kwa mke wake alafu kingine hana amani juu ya mazingira aliyopo mke wake na huyo mwanamme.Kila anapojaribu kumwambia mkewe arudi mke hataki anasema hawezi kurudi na kuwaacha wenzake katika mazingira hayo.Sasa akaja kuniomba ushauri mi nikamwambia mfuate huko huko alipo,je nimekosea kumpa ushauri huo?kama ungekuwa wewe ungeshauri nini
Karibuni kwa mawazo yenu
 
Kwani kuna nini nyuma ya pazia kati ya huyo mwanamke na mwanaume huko safarini?? Harufu ya usaliti kama nainusa vile...Mwambie jamaa awe makini na ndoa yake, Maumivu ya kuchapiwa mabaya aisee..Amuwahi mke wake
 
Huyo mke nae si mtu mzima, atarudi akichoka. Mambo mengine kujitia simanzi bure
 
Tatizo gani hilo ambalo linachukua mda mrefu hapo mbona kitu kimefichika.
 
Kwani kuna nini nyuma ya pazia kati ya huyo mwanamke na mwanaume huko safarini?? Harufu ya usaliti kama nainusa vile...Mwambie jamaa awe makini na ndoa yake, Maumivu ya kuchapiwa mabaya aisee..Amuwahi mke wake
Alafu inaonyesha mwanamke akiambiwa arudi hataki.Mazingira hupeleka uarifu
 
Huyo mke nae si mtu mzima, atarudi akichoka. Mambo mengine kujitia simanzi bure
Kweli ni mtu mzima alafu amejazia balaa vizuri yani namwonea huruma Mme wake
 
Kwani kuna nini nyuma ya pazia kati ya huyo mwanamke na mwanaume huko safarini?? Harufu ya usaliti kama nainusa vile...Mwambie jamaa awe makini na ndoa yake, Maumivu ya kuchapiwa mabaya aisee..Amuwahi mke wake
Kaka nakuona kwenye ubora wako
 
Ebu tujaribu kuvaa viatu vya huyu Mme utagundua ni kwa jinsi gani anakosa furaha,Alafu kingine nilichogundua kwa kuwa wote ni wafanyakazi basi jamaa hana voice kwa mkewe.Kwa mana kila anapomwambia rudi mke hataki mi nahisi anasalitiwa waziwazi ndugu yetu
 
Huu Ni uongo!!
Hata kama gari limeharibika, haiwezekani likawa halijatengenezwa kwa muda wote huo wa wiki tatu!!
Ofisi gani hiyo inashindwa kuwarejesha wafanyakazi wake wakiwa wamepatwa Na matatizo
 
Marehemu alikua hana ndugu hadi asafirishwe na wafanyakazi wenzie peke yao kadiri ya maelezo yako..?? Ninyi ni wafanyakazi ama ni vibarua ktk hiyo ofisi..? Kwamba uwepo usiwepo sawa tu..............Ungesema tu hii ni riwaya kama za akina Ngoswe... (tusingekuchapa)

..............Anyway ndo mana Tahakiki zipo................

Kuhusu rafiki yako, mwambie huu ndo muda mwafaka wa kunoa makofi, akifika tu mkewe amweke vitu hadi ajitambue kua yeye ni mke wa mtu
 
Kama walikwenda Sumbawanga inawezekana wameshakuwa misukule hao. Wiki tatu gari gani hio isiotengezeka?[emoji15] Hio ajira bado inawasubiri tu muda wote huo?[emoji15]
Kwanini hio kampuni yenu isipeleke nauli au hela ya matengenezo ya hio gari?[emoji15] maswali ni mengi sana hata mpaka usaidi kutoa ushauri hapa.



Ndukiiiii[emoji125] [emoji125] [emoji125]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…