Unyanyasaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Unyanyasaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

marine 1

Member
Joined
Jul 29, 2015
Posts
60
Reaction score
67
Habari za muda huu ndugu zangu.

Kwa kweli Kwa Hali ilivyo, inabidi jambo kubwa sana lifanyike katika nchi yetu kubadili mifumo yetu ya ulinzi na usalama wa raia.

Asubuhi ya Leo, nasikiliza Power Breakfast ya Clouds FM, kuna habari ya kijana ISSA, ambaye amefanyiwa ukatili uliopitiliza na kuondolewa utu wake. Kijana kapigwa, katobolewa kwenye koo na vitendo vingine kinyume na ubinadamu.

Sababu ni tuhuma za kijana Kuiba TV, ambapo Askari wa kituo cha Goba walitaka rushwa ya laki nane. Mama akaomba punguzo Hadi laki tano. Lakini PESA haikutumwa kwakua wazazi walitaka itumwe kwa namba ya Askari, lakini Askari wakagoma na kutaka itumwe Kwa namba ya mtuhumiwa.

Kinachoumiza zaidi ni majibu ya dharau na kejeli ya IGP Sirro na Ramadhani Kingai.

Mwandishi alipomhoji Sirro, Sirro alimjimu kama amemuona na ana udhibitisho. Mwandishi akamjibu ndio, Sirro kuona hana cha kujitetea akamwambia amtafute kamanda wa Kinondoni.

Kingai yeye anaongelea kwa wepesi tu kwamba kijana yupo hospitali na watamfungulia mashtaka.

Kwa kweli watu hawa (Polisi), Kwanza ndo wanaongoza Kwa vitendo vya kikatili na ugaidi dhidi ya watu na Mali zao. Hawana weledi katika kazi na hawazijui kanuni za kazi yao.

Huyu IGP amekuwa na Ile mentally ya awamu iliyopita, ya uongo, chuki na uonevu. Na Kingai ni mtekelezaji WA vitendo hivyo.

Hawa ndio waliomshauri Mama vibaya kuhusu Mbowe na kumpelekea kuonekana Mwongo, kinyume na dhamira yake. Wanahitajika kupumzishwa.
 
Kama Kingai anasema kijana yupo hospitali na atafungiliwa mashtaka, yupo hospital chini ya polisi au mzazi?

Ilikuaje mtihumiwa aliyekuwa chini ya polisi akateswa na wakamwachia na leo waseme tutamkamata?

Huyu angekufa naamini kabisa polisi wangesema hatujui na hatujawahi kumkamata mtu kwa jina hilo la Isa
 
Kungai na Siro wasipofunguliwa mashtaka kwa madhambi waliyofanya, basi nitajua hii nchi kila mtu apambane mwenyewe ili usitiwe mikononi mwa polisi.

Ni bora ukamatwe na mgambo wa ADF au alshabab kuliko kukutana na polisi hawa.

ADF huwezi kuambiwa toa laki ngapu hizo alafu ukawaambia huna wakutoe koo,sasa utamezaje ugali?
 
ni Bora uangukie mikononi mwa mtoa roho kuliko hawa police wa hapa kwetu huwa ni kama wanashikwa wazimu hawawezi kujizuiaa kabisa.
 
Katika watu ambao natamani sana mkono wa mungu umguse ni huyu Kingai, haifa na hana utu kabisa.

Hivi hii nchi inawachawi kweli itusaidie kwa huyu kiumbe.

Jeshi la polisi linatakiwa kusimamiwa na chombo kingine.
 
Nakuandikia kwa wema mdogo wangu ACP Ramadhani Kingai. Jua kuwa nakupenda na kukuombea sana kwenye kazi zako. Lakini, kama binaadamu, unapaswa kupata muda wa kutosha kujitafakari na kujirekebisha.

Kazi yako isikuondolee ubinaadamu wako na utu wako. Jua kuwa ninakufahamu na ninakufuatilia. Amini nakwambia, leo umenisikitisha kwa majibu yako uliyoyatoa kwa Mtangazaji wa Clouds FM kuhusiana na tuhuma za kuteswa kwa kijana Issa pale Kituo cha Polisi Goba.

Inasemwa kuwa (kwa mujibu wa Mama yake Issa) kuwa Issa alikamatwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na simu ya wizi. Akafikishwa kituo cha Polisi Goba ambapo aliwekwa mahabusu.

Baadaye, Polisi wakataka watumiwe shilingi laki nane-walizozipunguza hadi laki tano ili 'walimalize' suala hilo. Mama wa Issa hakufanikisha kuzituma pesa hizo. Issa akaipata vyema. Akateswa na sasa ameachwa na tundu kwenye koo pamoja na madhila mengine aliyofanyiwa.

Issa alilazwa kwa muda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na sasa ameruhusiwa kurudi nyumbani. Wanahabari wakataka kujua maelezo ya upande wa pili wa Polisi. Wakampigia kwanza IJP Simon Sirro. IJP Sirro akawataka wawasiliane na Kamanda wa Kinondoni/Oysterbay. Ndipo ulipopigiwa wewe ACP Kingai.

Ukiongea kwa ukali na kutojali, umekuwa ukisisitiza kuwa Issa ni mhalifu-tenawa kuvunja nyumba na kuiba. Ukasema kwakuwa ametoka hospitali, anapaswa kusakwa na kufikishwa mahakamani kwakuwa hata mashtaka yake yako tayari.

Kimsingi, ACP Kingai hukujibu tuhuma za kuteswa kwa Issa hadi kuachiwa ulemavu wa kudumu. Badala ya kuonesha kupokea tuhuma hizo, wewe uling'ang'ania kumkamata na kumpeleka mahakamani Issa. Hapa ulikosa sifa kuu ya kiuongozi ya kusikiliza na kuelewa.

Hata wewe mwenyewe ulikiri kuwa hujui alipo Issa kwasasa. Hujui yupo kwenye hali gani. Hujui hatma ya kesi yake kule Goba (ingawa Mama Issa amesema Polisi walimwambia baada ya mateso ya mwanaye kuwa Issa amesamehewa).

Ukali hautendi kazi ya weledi. Ukali hautoi suluhisho la maana. ACP Kingai, jitafakari katika hilo. Sikiliza, elewa halafu jibu. Busara hazisababishi hasara.

Vizibiti vya akina Mbowe arudishiwe nani?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Sombetini, Arusha)

Nilikugusia pia humu:Wito wa mpito kwa DPP: Wakili aliyemwandaa ACP Kingai aondolewe jopo la Mashtaka la akina Mbowe
 
Nakuandikia kwa wema mdogo wangu ACP Ramadhani Kingai. Jua kuwa nakupenda na kukuombea sana kwenye kazi zako. Lakini, kama binaadamu....
Mimi nawaza tu kama ile Pisto A5340 Luger mahakama imethibitisha siyo ya Adamoo na uchunguzi wa kutoka Forensic bearal ulionesha A5340 haijasajiriwa Tanzania sasa ni ya nani??
 
Duh! hii movie nimeisikia ila kwa haraka nikasema kile chuo cha uongozi cha mwalimu Nyerere wangepelekwa kizazi kipya cha polisi ili wajifunze tofauti kati ya kuongea na polisi wenzao (amri) na kuongea na raia.

Pale lilikuwa ni jambo rahisi tu kukiri kwamba kesi anaijua na tatizo la Issa analijua liko kwenye uchunguzi wa hali ya juu, na mama Issa atulie apewe msaada. Majibu yake yameonekana yakitetea jeshi la polisi na kukandamiza mtuhumiwa.

Kiujumla kilichosikika Kisutu kati yake na Kibatala pamoja na hili la leo tusitegemee ukamataji wa watuhumiwa wenye weledi hadi kizazi kipya kitakapoelimishwa.
 
Nimesikiliza hiyo habari Leo asubuhi hakika nimeumia Sana hasa baada ya kupata maelezo ya kingai.

Dogo alinunua TV ya wizi na polisi wamempa kesi ya kuvunja na kuiba,nimeshangaa kingai anasema mtoto bado yupo mahabusu wakati huohuo kumbe mtoto yupo nyumbani anauguzwa.

Sirro ni muda wake WA kuachia ngazi huuu
 
Hii kesi inafanana na ya yule alonunua simuuu na ameishia lupango miaka 30

 
Akija alien akaulizia shetani anafananaje unamuonyesha Kingai
 
Back
Top Bottom