Uongo upi unaoukumbuka uliambiwa wakati ukiwa mdogo na ulijua ni ukweli

Kuna kitabu nilisoma hivyo nikakutana na neno wazinzi bahati nzuri nilikuwa karibu na mama yangu ikabidi nimuulize maana ya hilo neno mama akaniambia kuwa wazinzi=wezi . Nilipokuja kujua ukweli nilikuwa nimeshalitumia sehemu nyingi sana hilo hata sehemu ambayo haihusiki.
 
Kuna hii first time napanda pantoni nilikua na mdogo wangu mzee akatuambia tunaenda zanzibar basi dah tupo ndani ya kivuko najua ndio tunaenda zenji hata baada ya kurudi stori za mtaani kwa madogo wenzangu ni kua nimetoka zenji hii chai ilikaa muda sana nilikuja kujua ukweli miaka mitano mbele kua mzee aliniingiza chaka
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
ha ha ha wamama sio watu wa kisportsport
 
Kulikuwa na mzungu mmoja hivi [German]alijitolea kuijenga shule yetu ,basis wakat ujenz unaendelea kipindi hicho nasoma darasa LA NNE,mwalimu anatufundisha ghafla yule mzungu akawaanazunguukia yale maengo ndio mwalimu wetu akalopoka""WAZUNGU HAWANYI NA WAMASAI HAWALI UGALI KABISA"sijui alifikilia nn yule mwalimu na sisi kuamini kabisa,
 
aisee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…