Uongozi, madaraka ni mapambo ya muda - usijisahau

Uongozi, madaraka ni mapambo ya muda - usijisahau

Makumbele

Member
Joined
May 9, 2009
Posts
77
Reaction score
431
Kiongozi si lazima awe mtu aliye katika nafasi ya mamlaka au mwenye cheo. Kimsingi, dhana nzima ya nafasi na vyeo ni mpangilio wa muda, ambao wakati mwingine hukuzwa mno na kutiwa nakshi isiyo sahihi.

Kwa bahati mbaya, wengi wakishapata vyeo/madaraka ‘hupoteza fahamu’ waziwazi! Tumewaona wenzetu kadhaa ambao awali tuliwaona wakiwa watu wenye uelewa, uwezo mkubwa wa kufikiri na utambuzi lakini walipopata vyeo (uteuzi au kwa kupanda madaraja) wamejisahau na wengine kugeuka ‘Miungu-watu’. Madaraka na uwezo vimewalevya.

Mamlaka na nguvu inayoambatana na madaraka ni nzuri, tamu kwa kadiri inavyodumu; lakini wakati mamlaka na nguvu zinachukuliwa (ukivuliwa/tumbuliwa cheo), basi jina lako pia hushuka au kuporomoka wakati huo huo.

Ikiwa unaweza kufanikiwa kujishughulisha, basi fanya hivyo. Ni hakika utakabiliwa na vikwazo vingi njiani, pia kuna wakati utashindwa, lakini kuwa na subira na usonge mbele. Toa mchango, alama na ongeza thamani.

Mafanikio ya kudumu huchukua muda mwingi na si kwa wenye moyo dhaifu. Kumbuka: Ukuu hauji kirahisi, unakuja kwa gharama kubwa hivyo lazima mtu ujitoe kikamilifu.

Mwisho: Jitahidi kuwa kiongozi katika eneo lako, hasa wakati huna mapambo au cheo! Kuwa na uongozi unaoacha alama (legacy).
 
Mleta mada, zamani Wafalme walirithi madaraka kutoka kwa wazazi wao. Kadiri dunia ilivyoelimika waligundua mapungufu mengi katika mfumo huu wa utawala. Mnaweza kumpata mtu ambae hastahili kuwa kiongozi lakini ni kwasababu ni haki yake ya kuzaliwa.

Pongezi nyingi ziwaendee Wagiriki kwa kuanzisha utawala wa kidemokrasia. Wananchi kupata haki ya kumchagua kiongozi wanaemuona anafaa. Hii demokrasia katika nchi za kisoshalist ni ngumu kutekelezeka.
 
Hii demokrasia katika nchi za kisoshalist ni ngumu kutekelezeka.
Nchi nyingi za Kiafrika ni za Kisoshalist?

Maana huku ndiko kuna viongozi wengi wanaong'ang'ania kuongoza kwa nguvu bila ridhaa ya wananchi.

Wako tayari kuua wananchi wao kwa wao kutaka kuongoza.

China, wakomunisti, kwa utaratibu wa chama chao wanaouwezo wa kumwondoa Xi akivurunda. Xi hawezi kuamrisha polisi au jeshi likawaue wananchi ili abaki madarakani, lakini hapa (sijui kama Tanzania ni wasoshalist), hilo halimstui kiongozi mmoja tu anayeshikilia kila chombo cha kulinda wananchi.

Kim Jong Il, hata huyu kuna utaratibu wa chama chao. Chama kinaweza kumtia msukosuko mkubwa kama akikiuka taratibu zao za kichama. Hawa ni wakomunisti.

CCM ya Tanzania haina uwezo wa kumwajibisha mwenyekiti wake, badala yake, yeye ndiye anayeweza kuwaadabisha wajumbe wa chama hicho wakikiuka anayoyataka yeye. Kwa sababu yeye anayo mabunduki na mabomu, wao hawana.

Kuna nchi zinazofuata mfumo wa Kisoshalist huko nchi za Scandinavia , lakini wana taratibu nzuri za kuwachagua viongozi wao kwa njia za kidemokrasia.

Kwa hiyo sielewi ulikuwa na maana gani katika sentensi moja hiyo.
 
Good thinking 'hawa tunaodhani usomi wao utalisaidia Taifa ndiyo wa kwanza kujitoa ufahamu likoje hilo?
 
Ila mm tuachane na yote...mie mpaka leo hii wafanyakazi hawajongezewaga mshahara..hv huyo Rais wenu anahis wanaishije jamani!!mie hiki ndo kinanitia hasira balaa jamani.
 
Demokrasia ,kwa maoni yangu, haiwezi kushamiri sehemu ambayo kuna umasikini wa kutupwa.

Maana umasikini Mara nyingi unaambatana na ujinga.Mtu mjinga hana awareness yoyote kuhuhusu mambo muhimu zikiwemo haki zake za kiraia. Huyu ni mtu ambaye akipewa sahani ya ubwabwa anaweza kuuza kura yake.

Kwa kifupi masikini anaweza kununuliwa wakati wowote. Demokrasia ya kweli kwa nchi nyingi za kijamaa itachukua mda mrefu kupatikana.
 
Back
Top Bottom