Uongozi wa kupeana hisani kutaigeuza nchi kuwa ya kisurutani

Uongozi wa kupeana hisani kutaigeuza nchi kuwa ya kisurutani

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Sisi tunatoa tu maoni yetu hatujui yataisaidiaje nchi yetu leo na kesho, lakini ni heri kusema kuliko kunyamaza.

Nchi yenye watu zaidi ya 60m hawakosekani watu safi wenye sifa ya kuongoza wenzao kupata maendeleo. Kama ukiwekwa utaratibu na mfumo mzuri wa kuwapata viongozi bora unaofanana na mfumo wa kuwapata wachezaji mpira wazuri kwenye timu taifa letu litasonga mbele haraka. Kwenye mpira hata Rais wa timu au mmiliki wa timu hawezi kumsajili mtoto wake acheze mpira nafasi ya golikipa kama mtoto huyo hana sifa ya kuwa golikipa.

Taifa letu linadumaa kwasababu teuzi nhyingi za viongozi nchini ni za kulipana hisani na kuenziana bila kuzingatia vigezo vya sifa. Mfano, mimi sina uhakika kama watu kama Mwl. Nyerere, Mzee karume, Kawawa, Mzee Malecela, Mkapa, Kikwete, Warioba, Sokoine, Magufuli, nk walikuwa na watoto nma wajukuu ambao wana sifa (tabia, karama, uadilifu na uzalendo) kama wazazi wao kiasi cha kustahili lazima wawe viongozi wa nchi hii.

Tutafute mfumo wa uteuzi ambao utaruhusu watu wote wenge sifa wawe na fursa sawa na kuwa wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Mikoa, wakurugenzi na nafasi nyingine za umma kuliko ilivyo sasa. Sifa na juhudi binafsi ya mtu iwe ndiyo kigezo pekee cha kuwa Mkuu wa Mkoa.
 
Mwarobaini ni ile rasimu ya warioba ipite iwe katiba mpya. Imeondoa mamlaka ya kuteua watu wengi wasio na sifa wala elimu ila uanachama wa kwa ccm
 
Tayari ni nchi ya usultani, Oligarchs. Ni watu walewale, watoto wao, ndugu, washkaji zao toka uhuru hadi leo wanaoshilikia ngazi zote za juu za uongozi, vitengo na idara zote muhimu.
 
Sisi tunatoa tu maoni yetu hatujui yataisaidiaje nchi yetu leo na kesho, lakini ni heri kusema kuliko kunyamaza.

Nchi yenye watu zaidi ya 60m hawakosekani watu safi wenye sifa ya kuongoza wenzao kupata maendeleo. Kama ukiwekwa utaratibu na mfumo mzuri wa kuwapata viongozi bora unaofanana na mfumo wa kuwapata wachezaji mpira wazuri kwenye timu taifa letu litasonga mbele haraka. Kwenye mpira hata Rais wa timu au mmiliki wa timu hawezi kumsajili mtoto wake acheze mpira nafasi ya golikipa kama mtoto huyo hana sifa ya kuwa golikipa.

Taifa letu linadumaa kwasababu teuzi nhyingi za viongozi nchini ni za kulipana hisani na kuenziana bila kuzingatia vigezo vya sifa. Mfano, mimi sina uhakika kama watu kama Mwl. Nyerere, Mzee karume, Kawawa, Mzee Malecela, Mkapa, Kikwete, Warioba, Sokoine, Magufuli, nk walikuwa na watoto nma wajukuu ambao wana sifa (tabia, karama, uadilifu na uzalendo) kama wazazi wao kiasi cha kustahili lazima wawe viongozi wa nchi hii.

Tutafute mfumo wa uteuzi ambao utaruhusu watu wote wenge sifa wawe na fursa sawa na kuwa wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Mikoa, wakurugenzi na nafasi nyingine za umma kuliko ilivyo sasa. Sifa na juhudi binafsi ya mtu iwe ndiyo kigezo pekee cha kuwa Mkuu wa Mkoa.
Sawa
 
Tayari ni nchi ya usultani, Oligarchs. Ni watu walewale, watoto wao, ndugu, washkaji zao toka uhuru hadi leo wanaoshilikia ngazi zote za juu za uongozi, vitengo na idara zote muhimu.
Hivi unataka kusema Nape mnauye ana akili, hekima na maarifa kama ya baba yake Mzee Mnauye (mwanajeshi)?

Kama Kuna sehemu ambayo inapaswa kuwa na viongozi imara, wasomi na wenye maarifa makubwa ni sehemu ya Wilaya. Wilaya ndiko waliko watu na shughuli nyingi za kiuchumi, kilimo, ufugaji, uvuvi na uchimbaji. Huwezi kupeleka DC wa hisani kule.
 
Back
Top Bottom