Uongozi wa Simba kwa Hitimana tumeteleza

Simba sio Namungo au Biashara,kama ulishawai msikia Magori akisema kwenye benchi la ufundi la Simba aachiwi kocha pekee asajili.
mchezaji anaewaniwa na Simba anapita kwenye machujio mengi.alafu yule ni kocha msaidizi tu kocha mkuu bado ni Gomez.
Sasa leo imekuwaje mmewaleta Aigle Noir kama siyo akili za Kirundi ni nini hasa kimetusukuma kama Simba na Weledi wetu wooote kuleta hayo makapi?
 
Kaka kumbuka aliempendekeza hitimana kuwa msaidiz ni gomez mwenyewe maana wanajuana walishafanya kazi pamoja

Hata wakat Gomez kaja simba ilisemekana Hitimana atakuja kuwa msaidizi... Na Hitimana alihojiwaga akasema amezungumza na Gomez ila anajua Simba tayar wana matola ... Sema Simba wakamchomolea Gomez wakataka aendelee na matola ili matola apate uzoefu

Sasa opportunity imetokea ya issue za lesen za CAF gomez akaomba hitimana aje

pia ingawa Gomez anaendelea kusomea CAF pro licences hata akipata bado matola.hawez kusimama kama.msaidizi sababu kuna taarifa matola kafeli mitihani ya CAF lesen clasa B ambayo ndo sifa ya kuwa msaidizi lugha ya kingereza imemuangusha, mitihani alifanya miez kadhaa nyuma.. So bado hatakuwa na sifa ya kukaa benchi kama.msaidizi

Kama unakumbuka alienda kusoma matola, na hata kocha wa makipa nae aliondoka kama two weeks

So kama.Hitimana atazingua kosa.litakuwa la Gomez kumchekea ila sidhan kama kwa Simba ya Sasa hitimana anaweza aka influence usajili wa wachezaj hata angekuwa yeye kocha mkuu..

Kumbuka Hitimana katoka simba bado kawepo hapa Nchini akizunguka na team za humu ndan tu Simba ingekuwa na shida naye wala wasingempa usaidiz matola toka enzi ya sven
 
Mkuuu hapa umeeleweka, umejibu hojja kwa Hojja lkn Matolaaaaa! Wakati mwingine mpira siyo vyeti si unaona Prof. Naabi anapigwa za usso na wenye Ngumbalu Mkuuu. Matola mtoto wa Msimbazi kitambooo
 
Ukweli Ni kwamba huyo kocha kwa simba atatulia..pale Kuna wababe watamtuliza..japo anaonekana mjuaji Sana huyu kocha mrundi
 
Tp mazembe atakuwepo simba day
 
Usikariri! Sio kila timu ipo tayari muda kualikwa wowote. Mabingwa wa CECAFA, Express ya Uganda, kesho kutwa tu tarehe 17/09/2021 wanaenda Sudan kucheza mechi ya marudiano na El Mereikh, halafu wewe unakimbilia kusema eti waje kwanza Tanzania kucheza mechi ya kirafiki! Wakati mwingine inabidi kuwaachia wenye akili wapange, wengine mbaki kuunga mkono tu mipango
 
Inawezekana una hoja, ila hawa makocha waliwahi kufanya kazi pamoja na mrundi alikuwa kocha msaidizi na amependekezwa na Da rosa.
Kwa jinsi usajili wa Simba unavyofanyika ni ngumu huyu kocha kuleta wachezaji wa Burundi kwa sababu Simba ipo level nyingine Afrika.
 
Mkuu acha kulalamika kama Utopolo. Timu zote za CAF Champions League zinacheza mechi za raundi ya awali weekend hii kati ya tarehe 17 hadi 19, ukiondoa zile timu vigogo 10 zilizoingia moja kwa moja. Sio rahisi kihivyo kupata timu. Labda nikupe mfano hai. Hivi ingewezekana vipi kuwaomba Rivers United wacheze mechi ya kirafiki na Simba wakati wanawahi kwao kucheza mechi ya pili weekend hii?
 
Sasa leo imekuwaje mmewaleta Aigle Noir kama siyo akili za Kirundi ni nini hasa kimetusukuma kama Simba na Weledi wetu wooote kuleta hayo makapi?
Labda nikuulize. Simba ikialikwa leo iende ikacheze Misri na Zamalek tarehe 18/09/2021 kwenye mechi ya kirafiki, itaenda? Kwa nini isiende? Jibu hilo ndilo na kwa wengine ni hivyo hivyo. Timu ikikubali mwaliko unashukuru Mungu, maana kwa sasa kila timu na kocha ana programu zake
 
Ukweli ni kwamba Gomez alishawahi kufanya kazi na huyo Hitimana.

Hivyo anamfahamu utendaji wake wa kazi.

Halafu Simba ni next level ( Sio sahihi kuilinganisha kiutendaji na Biashara au Namungo)
 
Ukweli Ni kwamba huyo kocha kwa simba atatulia..pale Kuna wababe watamtuliza..japo anaonekana mjuaji Sana huyu kocha mrundi
Very true Mkuu, Imagine alifika Mtibwa akatoa orodha ya watu kadhaa waondolewe akiwamo Barnabas eeti ndio afanyekazi pale Klabuni. Sasa mtu wa aina hii leo ndio tunamleta Klabuni kwetu. Brand ya Simba Isichezewe ovyo jamani wakati mwingine wacha tutoe nyongo zetu kwa watu Utopolo kama hawa.
 
Sasa leo imekuwaje mmewaleta Aigle Noir kama siyo akili za Kirundi ni nini hasa kimetusukuma kama Simba na Weledi wetu wooote kuleta hayo makapi?
Simba hii ni next level.uyo mrundi kocha Gomez ndo alimpendekeza yeye mwenyewe.uo ubinafsi wake uliosema kwa Simba hii hana nafasi,atafanya kazi vizuri ili aijenge vema cv yake,kwakuwa Simba ina ndoto za kufika nusu fainali au fainali.
ondoa mitazamo yako ya sasa uliyonayo juu ya kocha Hitimana.
 
Mbona mbademka Sana. Hizi Ni mechi za kocha kupanga tu first 11 yake na kuona atengeneze vipi timu yake. Siyo mechi za wazi za kirafiki km mnavyowaza.

Subirini tarehe 19 September ndiyo siku ya kupata ladha ya mechi ya kirafiki halisi.

Kuhusu huyo kocha sidhani km mifumo ya SIMBA ya usajili ilivyo kwa sasa itampa nafasi ya kujaza watu wake.

Pia nadhani mleta hoja ana HOJA sana kwasababu huwezi kuwa kocha halafu ukaigeuza klabu kuwa sehemu ya ajira kwa ndugu zako. Tutakuwa tunafanya yaleyale ya Yanga na Hersi kuchukua wachezaji 6 kutoka nchi moja na pengine klabu moja. Na wengi ni wachezaji huru hamna afya hapo.

BILA SHAKA NI TAHADHARI NZURI .
 
Mkuuu hapa umeeleweka, umejibu hojja kwa Hojja lkn Matolaaaaa! Wakati mwingine mpira siyo vyeti si unaona Prof. Naabi anapigwa za usso na wenye Ngumbalu Mkuuu. Matola mtoto wa Msimbazi kitambooo

Yeah ndo maana Simba bado wanaye matola Hitimana kama kama kivuli tu cha CAF kwa sababu inabid kule CAF waseme nani kocha mkuu so kwenye makaratasi ya CAF atasomeka Hitimanankama head coach ikiwa kama bado Gomes atakuwa hajamaliza masomo na Gomez atasomeka msaidizi.. Ila kiuhalisia Gomez ndo Boss wa bench la ufundi
 
Malengo ya hizo mechi siyo haya mnayowaza nyie. Km Ni mechi halisi ya kirafiki ni tarehe 19 Sept. Hizi Ni za kocha kupanga first 11 yake na kuona performance ktk mbinu, mifumo nk

Acheni KUDEMKA bila kujua .
 
Simba Kama taasisi kubwa nchini wanayo mahusiano mazuri na taasisi nyingine kubwa duniani katika soka hivyo Simba hupata mawasiliano mapema kabla ya mtu yeyote na kisha hujiaanda.na hii ndo dhana kamili ya next level

Sio ubondia na mizengwe kibao wakati soka ni mchezo wa kirafiki
 
Daaaaaah unapoanzisha propaganda angalau uwe na taarifa sahihi.
Morocco sio aliyeipeleka Namungo mashindano ya kimataifa, Tafuta ajenda nyingine
 
Daaaaaah unapoanzisha propaganda angalau uwe na taarifa sahihi.
Morocco sio aliyeipeleka Namungo mashindano ya kimataifa, Tafuta ajenda nyingine
Nimekupata Mhutu wa Burundi na Vipi ajenda yenu ya Siri kuwaleta magarasa kwenye timu mnazofundisha itaendelea au mtaaachana nayo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…