MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,018
- 16,802
Nimekwazika sana tu kusikia ( tena kutoka kwa Msemaji Ahmed Ally akikiri hivi punde EFM Sports Headquarters na kusema zimechelewa tu kidogo kutokana na Masuala ya Fedha ) kuwa Wachezaji wa Simba SC wana manung'unuko ya Moyoni baada ya kutopewa / kutolipwa Posho zao kwa wakati ambazo Sisi Mashabiki tumekuwa tukihakikishiwa kuwa Wameshalipwa kumbe tulikuwa tukidanganywa tu.
Naipenda Simba SC ( hakuna mwana JamiiForums asiyejua hili labda awe ni Juha na Mwendawazimu tu ) ila nakereka / nachukizwa kusikia Mambo ya Kipuuzi kama haya yanafanyika na yanatokea katika Klabu Bora Namba 9 kama siyo Namba 8 kwa Afrika ya Simba Sports Club.
MINOCYCLINE ningesikia Upuuzi na Uswahili huu unafanyika au umetokea Yanga SC wala nisingeshangaa kwani wanastahili na ni haki yao hayo Kuyatokea.
Klabu ambayo Mwekezaji wake ni miongoni mwa Watu Tajiri Barani Afrika Mo Dewji inashindwaje kulipa kwa wakati Posho za Wachezaji?
Tunatumia Nguvu Kubwa mno Kuipambania na Kuitetea Simba SC yetu hapa JamiiForums huku Wengine hadi Tukitukanwa Kutwa na kwa Upuuzi huu uliojaa Uswahili mwingi kiukweli mtatukatisha Tamaa na tutaacha kuwa Watetezi wenu.
Halafu Msemaji wa Simba SC Mdogo Wangu Ahmed Ally acha kudhani kuwa kila Mtu anayetoa Taarifa za Ndani za Simba SC ni mwana Yanga SC au kuna Kikundi fulani cha Watu kina Uadui au Chuki na Klabu yetu.
Usisahau kuwa Wengine ( MINOCYCLINE nikiwemo ) tuko karibu sana na Wachezaji wa Simba SC ( tena Waandamizi ) na Viongozi wa Simba SC hivyo huwa tunapata Taarifa nyingi mno mbaya na nzuri za Klabu ila kutokana na Mapenzi yetu kwa Simba SC huwa tunaamua Kunyamaza / Kuuchuna tu.
Hatutaki kila mara kusikia sijui Mwekezaji Wetu Mo Dewji anaenda Kukutana na Wachezaji bali tunataka kusikia Posho za Wachezaji wetu wa Simba SC zinatoka kwa wakati na hata Mishahara yao inaingizwa kwa wakati.
Taarifa hii imenikera mno na kwa ninavyowajua Wachezaji wa Kiafrika walivyo na Usununu katika Suala la Pesa na Madai yao Mechi yetu ya Kesho dhidi ya Wanaojua, Wababe na Matajiri Wydad Casablanca FC naanza kuiona ni ngumu ( itakuwa ngumu ) japo Watu wa Kamati Maalum ya Umafia na Utamaduni wamenihakikishia kuwa Kesho Mwarabu anakufa / anafungwa Goli 3 au 4 na zikipungua basi ni Goli 2 ila Wydad Casablanca FC anafungwa / anakufa.
Ngoja tuone ila tukifungwa siwaachi.
Naipenda Simba SC ( hakuna mwana JamiiForums asiyejua hili labda awe ni Juha na Mwendawazimu tu ) ila nakereka / nachukizwa kusikia Mambo ya Kipuuzi kama haya yanafanyika na yanatokea katika Klabu Bora Namba 9 kama siyo Namba 8 kwa Afrika ya Simba Sports Club.
MINOCYCLINE ningesikia Upuuzi na Uswahili huu unafanyika au umetokea Yanga SC wala nisingeshangaa kwani wanastahili na ni haki yao hayo Kuyatokea.
Klabu ambayo Mwekezaji wake ni miongoni mwa Watu Tajiri Barani Afrika Mo Dewji inashindwaje kulipa kwa wakati Posho za Wachezaji?
Tunatumia Nguvu Kubwa mno Kuipambania na Kuitetea Simba SC yetu hapa JamiiForums huku Wengine hadi Tukitukanwa Kutwa na kwa Upuuzi huu uliojaa Uswahili mwingi kiukweli mtatukatisha Tamaa na tutaacha kuwa Watetezi wenu.
Halafu Msemaji wa Simba SC Mdogo Wangu Ahmed Ally acha kudhani kuwa kila Mtu anayetoa Taarifa za Ndani za Simba SC ni mwana Yanga SC au kuna Kikundi fulani cha Watu kina Uadui au Chuki na Klabu yetu.
Usisahau kuwa Wengine ( MINOCYCLINE nikiwemo ) tuko karibu sana na Wachezaji wa Simba SC ( tena Waandamizi ) na Viongozi wa Simba SC hivyo huwa tunapata Taarifa nyingi mno mbaya na nzuri za Klabu ila kutokana na Mapenzi yetu kwa Simba SC huwa tunaamua Kunyamaza / Kuuchuna tu.
Hatutaki kila mara kusikia sijui Mwekezaji Wetu Mo Dewji anaenda Kukutana na Wachezaji bali tunataka kusikia Posho za Wachezaji wetu wa Simba SC zinatoka kwa wakati na hata Mishahara yao inaingizwa kwa wakati.
Taarifa hii imenikera mno na kwa ninavyowajua Wachezaji wa Kiafrika walivyo na Usununu katika Suala la Pesa na Madai yao Mechi yetu ya Kesho dhidi ya Wanaojua, Wababe na Matajiri Wydad Casablanca FC naanza kuiona ni ngumu ( itakuwa ngumu ) japo Watu wa Kamati Maalum ya Umafia na Utamaduni wamenihakikishia kuwa Kesho Mwarabu anakufa / anafungwa Goli 3 au 4 na zikipungua basi ni Goli 2 ila Wydad Casablanca FC anafungwa / anakufa.
Ngoja tuone ila tukifungwa siwaachi.