MINOCYCLINE
JF-Expert Member
- Apr 2, 2015
- 8,018
- 16,802
Labda niwaambieni tu Uongozi wa Simba SC kuwa Rais mpya wa CAF Bwana Patrice Motsepe haungwi (hakuungwa) Mkono na Rais wa TFF Bwana Wallace Karia ambaye inajulikana alikuwa ni Mtu wa aliyekuwa Rais wa CAF Bwana Ahmad Ahmad.
Hivyo kwa hili Tanzania (hasa TFF) inatakiwa kuwa makini nae sana huyu Rais mpya wa CAF Bwana Motsepe kwani ameshaanza kuonyesha kuwa ana Kisununu (Kinyongo) na Rais wa TFF Bwana Karia na Tanzania kwa ujumla.
Pia Uongozi wa Simba SC tambueni ya kwamba huyu Rais mpya wa CAF Bwana Patrice Motsepe na aliyekuwa Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) Bwana Senzo Mbatha Mazingisa ni Marafiki wakubwa, Washirika, walishakuwa pamoja katika Kamati kadhaa za Mashindano makubwa ya dunia (hasa ya AFCON na FIFA World Cup) ambayo nchi yao ilishaandaa lakini pia kumbukeni Wote hawa ni Raia wa Afrika Kusini wanakotoka.
Simba SC ama kwa kutokulijua hili au kulijua ila mmefanya Kusudi tu Juzi mliagizwa na Mamlaka za CAF kuwa Mechi yenu ya Jana dhidi ya El Merreikh Uwanja wa Mkapa mcheze bila Mashabiki na isitoshe hata nje ya Uwanja hakutakiwa Kuonekana Mtu yoyote ikiwa kama njia za Kuzuia Maambukizi ya Corona (Covid-19)
Cha Kushangaza na hata Mimi All - Rounder nimesikitika mno jana kwa Kiburi chetu cha Upumbavu na Ujeuri usio wa maana Sisi (Simba SC) tukawaona CAF chini ya Rais mpya Bwana Motsepe haina Akili na tunajua zaidi yao na Kukubali kutoruhusu Mashabiki kuingia (zaidi tu ya wale 200 walioruhusiwa) huku nje ya Uwanja tukaruhusu Mashabiki kuwepo kwa wingi tena Wakichagiza kwa Nyimbo zao huku wakipiga Kelele nyingi tu.
Mpaka hapa tu tayari tumeshaonyesha Dharau kwa CAF chini yake Rais wake mpya na Adui yetu Bwana Motsepe hivyo tujiandae mapema Kisaikolojia. Kama Ripoti ya Mtathmini wa Mechi inayotakiwa kwenda CAF akiliweka na hili Simba SC tutegemee Adhabu Kali au hata kuamriwa Kucheza Mechi zetu zilizobaki au nyinginezo katika Uwanja mwingine na wa nchi nyingine (siyo Tanzania)
Nanyi Mashabiki wa Simba SC hebu acheni Upuuzi na Kiburi cha Kijinga. Tujifunze Ustaarabu wa hasa kusikia Maelekezo ya Mamlaka za Mpira CAF. Tutakuja Kuigharimu Timu na hatimaye hata Ndoto zetu za Kufika mbali katika Michuano hii mikubwa Barani Afrika ikapotea na kuanza Kulaumiana na Kuwasingizia Mahasimu wetu wakubwa Yanga SC kuwa wamechangia Kutuhujumu (Kutusagia Kunguni) katika Kikombe.
Kwahiyo Mashabiki wa Simba SC ndiyo wanapenda Mpira na wana Uchungu zaidi na Timu yao kiasi kwamba hawawezi Kubakia Nyumbani na Kutii Mamlaka za CAF? Simba SC ina Mashabiki wenye Uchungu na Mapenzi kwa Timu yao kuliko wa AS Vita Club, Al Ahly, Mamelodi Sundowns na TP Mazembe ambao Wao walitii AMRI za Mamlaka ya CAF na hakuna aliyeenda Uwanjani au hata Kusogelea vilipo Viwanja vyao wakati wa Mechi zao.
Najua wanasimba Wenzangu Ukweli wangu huu Mchungu Kwenu unaweza Ukawakwaza ila All - Rounder sijazoea Unafiki au Kuipendelea Klabu yangu ya Simba SC hata kama inafanya vizuri ndani na nje ya nchi. Mimi ni Muumini Mkuu wa Nidhamu n Utaratibu na huwa nachukia mno Ujinga na Upumbavu. Tuvumiliane ila tubadilike kwa Faida kubwa ya Timu yetu Simba SC na nchi yetu Tanzania.
Kila Ia Kheri.
Wenu All - Rounder ( alias ) Brainiac.
Hivyo kwa hili Tanzania (hasa TFF) inatakiwa kuwa makini nae sana huyu Rais mpya wa CAF Bwana Motsepe kwani ameshaanza kuonyesha kuwa ana Kisununu (Kinyongo) na Rais wa TFF Bwana Karia na Tanzania kwa ujumla.
Pia Uongozi wa Simba SC tambueni ya kwamba huyu Rais mpya wa CAF Bwana Patrice Motsepe na aliyekuwa Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) Bwana Senzo Mbatha Mazingisa ni Marafiki wakubwa, Washirika, walishakuwa pamoja katika Kamati kadhaa za Mashindano makubwa ya dunia (hasa ya AFCON na FIFA World Cup) ambayo nchi yao ilishaandaa lakini pia kumbukeni Wote hawa ni Raia wa Afrika Kusini wanakotoka.
Simba SC ama kwa kutokulijua hili au kulijua ila mmefanya Kusudi tu Juzi mliagizwa na Mamlaka za CAF kuwa Mechi yenu ya Jana dhidi ya El Merreikh Uwanja wa Mkapa mcheze bila Mashabiki na isitoshe hata nje ya Uwanja hakutakiwa Kuonekana Mtu yoyote ikiwa kama njia za Kuzuia Maambukizi ya Corona (Covid-19)
Cha Kushangaza na hata Mimi All - Rounder nimesikitika mno jana kwa Kiburi chetu cha Upumbavu na Ujeuri usio wa maana Sisi (Simba SC) tukawaona CAF chini ya Rais mpya Bwana Motsepe haina Akili na tunajua zaidi yao na Kukubali kutoruhusu Mashabiki kuingia (zaidi tu ya wale 200 walioruhusiwa) huku nje ya Uwanja tukaruhusu Mashabiki kuwepo kwa wingi tena Wakichagiza kwa Nyimbo zao huku wakipiga Kelele nyingi tu.
Mpaka hapa tu tayari tumeshaonyesha Dharau kwa CAF chini yake Rais wake mpya na Adui yetu Bwana Motsepe hivyo tujiandae mapema Kisaikolojia. Kama Ripoti ya Mtathmini wa Mechi inayotakiwa kwenda CAF akiliweka na hili Simba SC tutegemee Adhabu Kali au hata kuamriwa Kucheza Mechi zetu zilizobaki au nyinginezo katika Uwanja mwingine na wa nchi nyingine (siyo Tanzania)
Nanyi Mashabiki wa Simba SC hebu acheni Upuuzi na Kiburi cha Kijinga. Tujifunze Ustaarabu wa hasa kusikia Maelekezo ya Mamlaka za Mpira CAF. Tutakuja Kuigharimu Timu na hatimaye hata Ndoto zetu za Kufika mbali katika Michuano hii mikubwa Barani Afrika ikapotea na kuanza Kulaumiana na Kuwasingizia Mahasimu wetu wakubwa Yanga SC kuwa wamechangia Kutuhujumu (Kutusagia Kunguni) katika Kikombe.
Kwahiyo Mashabiki wa Simba SC ndiyo wanapenda Mpira na wana Uchungu zaidi na Timu yao kiasi kwamba hawawezi Kubakia Nyumbani na Kutii Mamlaka za CAF? Simba SC ina Mashabiki wenye Uchungu na Mapenzi kwa Timu yao kuliko wa AS Vita Club, Al Ahly, Mamelodi Sundowns na TP Mazembe ambao Wao walitii AMRI za Mamlaka ya CAF na hakuna aliyeenda Uwanjani au hata Kusogelea vilipo Viwanja vyao wakati wa Mechi zao.
Najua wanasimba Wenzangu Ukweli wangu huu Mchungu Kwenu unaweza Ukawakwaza ila All - Rounder sijazoea Unafiki au Kuipendelea Klabu yangu ya Simba SC hata kama inafanya vizuri ndani na nje ya nchi. Mimi ni Muumini Mkuu wa Nidhamu n Utaratibu na huwa nachukia mno Ujinga na Upumbavu. Tuvumiliane ila tubadilike kwa Faida kubwa ya Timu yetu Simba SC na nchi yetu Tanzania.
Kila Ia Kheri.
Wenu All - Rounder ( alias ) Brainiac.