A
Anonymous
Guest
Stand ya Buzuruga iliyopo Wilaya wa Ilemela Mkoani Mwanza ina changamoto kubwa ya ukosefu wa vifaa vya kuwekea uchafu jambo linalosababisha Wadau wa stendi hiyo kumwaga uchafu chini ikifika usiku, kabla ya kuzolewa kesho yake asubuhi.
Licha ya uzuri na usafi wa stendi hiyo ya daladala ila ukosefu wa vifaa vya kuwekea uchafu unachafua taswira nzima ya eneo na kuhatarisha afya ya watumiaji wakati wa usiku na asubuhi kabla hazijaondolewa na wafanya usafi.
Ushauri wangu ni kwa wasimamizi wa stendi hiyo iliochini ya Halmashauri ya Ilemela kuweka vyombo vya kuwekea uchafu ili kuzuia utupaji holela wa taka na kurundika taka maeneo yasio stahiki.
Licha ya uzuri na usafi wa stendi hiyo ya daladala ila ukosefu wa vifaa vya kuwekea uchafu unachafua taswira nzima ya eneo na kuhatarisha afya ya watumiaji wakati wa usiku na asubuhi kabla hazijaondolewa na wafanya usafi.
Ushauri wangu ni kwa wasimamizi wa stendi hiyo iliochini ya Halmashauri ya Ilemela kuweka vyombo vya kuwekea uchafu ili kuzuia utupaji holela wa taka na kurundika taka maeneo yasio stahiki.