Uongozi wa Yanga uhusike na kulipa gharama zote za kuharibu mechi ya Derby iliyotakiwa kufanyika hivi leo. Uhuni kwenye soka haukubaliki

Uongozi wa Yanga uhusike na kulipa gharama zote za kuharibu mechi ya Derby iliyotakiwa kufanyika hivi leo. Uhuni kwenye soka haukubaliki

Mkono Mmoja

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2019
Posts
3,359
Reaction score
6,568
Ahlan bik

Football ukipenda iite Soccer ni mchezo wa kiungwana sana unaozingatia sheria , kanuni na taratibu zilizowekwa na shirikisho la mpira duniani kwa maana ya FIFA na shirikisho la mpira katika nchi husika.

Kanuni zipo wazi kabisa na uongozi wa Yanga unafahamu fika kuwa timu ambayo itakuwa ni mgeni inatakiwa iruhusiwe kufanya mazoezi ya mwisho siku moja kabla ya mechi tena kwa kuzingatia muda ule ule wa mechi.

Simba Sc kwa kulijua hili walifata sheria zote , cha ajabu uongozi wa timu ya Yanga umeamua kufanya uhuni kwa kuweka vikundi vya wahuni wanaodai kuwa ni Makomandoo wa Yanga kwa ajili ya kuulinda uwanja na kupelekea kuzuia timu ya Simba sc isiingie uwanjani kufanya mazoezi.


Wito wangu kwa TFF na Bodi ya Ligi iangalie namna ya kutoa adhabu kali sana kwa uongozi wa timu ya Yanga ili iwe fundisho kwa wahuni wote wanaolenga kuchafua taswira na hadhi ya Ligi kuu ya NBC.

Dunia nzima ilijiandaa leo hii kushuhudia moja kati ya derby kongwe na bora zaidi kutokea katika bara la Africa na dunia nzima. Ila jambo la ajabu na aibu kusikia kuwa mechi hii haitachezwa kutokana na viongozi na uongozi wa timu ya YANGA kufanya uhuni.

Watanzania wengi wamenunua ving'amuzi kwa ajili ya kushuhudia mechi hii , Je nyinyi viongozi wahuni wa Yanga ,mtawalipa nini watanzania waliopoteza pesa zao kwa ajili ya kulipia ada ya ving'amuzi??

Kuna wanachama na mashabiki wenu wamesafiri kutoka mikoa mbalimbali kuja Dar-es-salaam toka juzi kuja kushuhudia moja ya tukio hili la kihistoria ila chakusikitisha wanakuja kuambiwa kuwa mechi haitakuwepo. Je mnawalipa nini hawa wanachama wenu waliopoteza nauli, gharama za malazi na vyakula na kikubwa zaidi muda wao kuja kushudia mechi hii???

Uongozi wa Yanga umefanya makusudi kabisa kwasababu walikuwa na uwezo wa kuwasiliana na wahuni wao waliowaandaa kuharibu mechi kuwa waruhusu msafara wa Simba sc uingie uwanjani.Ila cha ajabu hawakufanya hivyo na ni wazi tukio hili limeonesha dhamira yao ya kuamini imani potofu za kishirikina na pia kuharibu mechi.

Kuna viongozi wa FIFA na CAF pamoja na waandishi wa habari wa kimataifa wamesafiri kutoka mataifa yao kuja kushuhudia mechi hii live ila cha ajabu wanaambiwa kuwa mechi haitafanyika.

TFF na TPBL msipochukua hatua kali za kinidhamu dhidi ya timu ya YANGA ,tambueni kuwa taifa zima litajua kuwa mnashirikiana na wahalifu hawa wa jangwani kuchafua taswira na hadhi ya moja ya ligi bora zaidi hapa barani Africa.

Wapo mashabiki wa timu hizi mbili walionunua tiketi kwa ajili ya kuingia uwanjani kuishuhudia hii Derby..Je pesa zao mnawarudishia?

Wasimamizi wa uwanja pia wametumia gharama zao kwa ajili ya kuhakikisha mechi hii inachezwa katika mazingira mazuri, Je Yanga mtarudisha gharama zao.?

TFF toeni adhabu kali kwa Yanga unaoongozwa na mwenyekiti wa vilabu barani Africa , Hersi Saidi. ili iwe fundisho kwa wahuni wengine wenye lengo la kuchafua ligi yetu.
 
Msiandike kwa mihemko. Kufuata sheria zote mnamaanisha nini? Je Simba waliwataarifu Yanga muda watakaoenda kufanya mazoezi ili mazingira yaandaliwe? Kwanini waende kwa muda wao wakati sheria wanaijua wao si wenyeji?

Kama Simba hawakutaka kuwasiliana na Yanga ambaye ni mwenyeji, je waliwasiliana na meneja wa uwanja ili aandae mazingira mapema? Barua ya Simba inasema meneja hakuwa na taarifa ya Simba kwenda kufanya mazoezi. Vipi kama meneja wa uwanja alianza kuandaa mazingira kwa ajili ya mechi husika kwa kuwa hana taarifa ya timu kwenda kufanyia mazoezi?

Mnaposema makomando wa Yanga mnamaanisha nini? Yanga ina kikosi cha kijeshi? Kuna kiongozi yeyote wa Yanga alikuwepo kuzuia? Polisi walikuwepo kwenye eneo husika walishindwa kuwadhibiti hao mnaoita makomando wa Yanga? Nafikiri kama kuna kosa limefanyika watakuwa walichukua hatua ili wahusika wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria husika.
 
Meneja hana taarifa? Hajui kuwa kuna sheria inataka timu ikafanye mazoezi?
Msiandike kwa mihemko. Kufuata sheria zote mnamaanisha nini? Je Simba waliwataarifu Yanga muda watakaoenda kufanya mazoezi ili mazungira yaandaliwe? Kwanini waende kwa muda wao wakati sheria wanaijua wao si wenyeji?

Kama Simba hawakutaka kuwasiliana na Yanga ambaye ni mwenyeji, je waliwasiliana meneja wa uwanja ili aandae mazingira mapema? Barua ya Simba inasema meneja hakuwa na taarifa ya Simba kwenda kufanya mazoezi. Vipi kama meneja wa uwanja alianza kuandaa mazingira kwa ajili ya mechi husika kwa kuwa hana taarifa ya timu kwenda kufanyia mazoezi?

Mnaposema makomando wa Yanga mnamaanisha nini? Yanga ina kikosi cha kijeshi? Kuna kiongozi yeyote wa Yanga alikuwepo kuzuia? Polisi walikuwepo kwenye eneo husika walishindwa kuwadhibiti hao mnaoita makomando wa Yanga? Nafikiri kama kuna kosa limefanyika watakuwa walichukua hatua ili wahusika wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria husika
 
Ahlan bik

Football ukipenda iite Soccer ni mchezo wa kiungwana sana unaozingatia sheria , kanuni na taratibu zilizowekwa na shirikisho la mpira duniani kwa maana ya FIFA na shirikisho la mpira katika nchi husika.

Kanuni zipo wazi kabisa na uongozi wa Yanga unafahamu fika kuwa timu ambayo itakuwa ni mgeni inatakiwa iruhusiwe kufanya mazoezi ya mwisho siku moja kabla ya mechi tena kwa kuzingatia muda ule ule wa mechi.

Simba Sc kwa kulijua hili walifata sheria zote , cha ajabu uongozi wa timu ya Yanga umeamua kufanya uhuni kwa kuweka vikundi vya wahuni wanaodai kuwa ni Makomandoo wa Yanga kwa ajili ya kuulinda uwanja na kupelekea kuzuia timu ya Simba sc isiingie uwanjani kufanya mazoezi.


Wito wangu kwa TFF na Bodi ya Ligi iangalie namna ya kutoa adhabu kali sana kwa uongozi wa timu ya Yanga ili iwe fundisho kwa wahuni wote wanaolenga kuchafua taswira na hadhi ya Ligi kuu ya NBC.

Dunia nzima ilijiandaa leo hii kushuhudia moja kati ya derby kongwe na bora zaidi kutokea katika bara la Africa na dunia nzima. Ila jambo la ajabu na aibu kusikia kuwa mechi hii haitachezwa kutokana na viongozi na uongozi wa timu ya YANGA kufanya uhuni.

Watanzania wengi wamenunua ving'amuzi kwa ajili ya kushuhudia mechi hii , Je nyinyi viongozi wahuni wa Yanga ,mtawalipa nini watanzania waliopoteza pesa zao kwa ajili ya kulipia ada ya ving'amuzi??

Kuna wanachama na mashabiki wenu wamesafiri kutoka mikoa mbalimbali kuja Dar-es-salaam toka juzi kuja kushuhudia moja ya tukio hili la kihistoria ila chakusikitisha wanakuja kuambiwa kuwa mechi haitakuwepo. Je mnawalipa nini hawa wanachama wenu waliopoteza nauli, gharama za malazi na vyakula na kikubwa zaidi muda wao kuja kushudia mechi hii???

Uongozi wa Yanga umefanya makusudi kabisa kwasababu walikuwa na uwezo wa kuwasiliana na wahuni wao waliowaandaa kuharibu mechi kuwa waruhusu msafara wa Simba sc uingie uwanjani.Ila cha ajabu hawakufanya hivyo na ni wazi tukio hili limeonesha dhamira yao ya kuamini imani potofu za kishirikina na pia kuharibu mechi.

Kuna viongozi wa FIFA na CAF pamoja na waandishi wa habari wa kimataifa wamesafiri kutoka mataifa yao kuja kushuhudia mechi hii live ila cha ajabu wanaambiwa kuwa mechi haitafanyika.

TFF na TPBL msipochukua hatua kali za kinidhamu dhidi ya timu ya YANGA ,tambueni kuwa taifa zima litajua kuwa mnashirikiana na wahalifu hawa wa jangwani kuchafua taswira na hadhi ya moja ya ligi bora zaidi hapa barani Africa.

Wapo mashabiki wa timu hizi mbili walionunua tiketi kwa ajili ya kuingia uwanjani kuishuhudia hii Derby..Je pesa zao mnawarudishia?

Wasimamizi wa uwanja pia wametumia gharama zao kwa ajili ya kuhakikisha mechi hii inachezwa katika mazingira mazuri, Je Yanga mtarudisha gharama zao.?

TFF toeni adhabu kali kwa Yanga unaoongozwa na mwenyekiti wa vilabu barani Africa , Hersi Saidi. ili iwe fundisho kwa wahuni wengine wenye lengo la kuchafua ligi yetu.
Miaka yote ya mechi za watani,mwenyeji anakabidhiwa uwanja,mgeni anaingia uwanja siku ya mechi akitokea mahali alipoweka kambi.Ndio maana hata meneja hakuwa na taarifa za wao kuja uwanjani. Hata Yanga hii nafasi ya kutumia huu uwanja kabla ya mechi round ya kwanza hakupewa, je hizo kanuni hazikuwepo, maana aliingia uwanjani akitokea Avic Town na mechi alicheza.
 
Simba Sc kwa kulijua hili walifata sheria zote , cha ajabu uongozi wa timu ya Yanga umeamua kufanya uhuni kwa kuweka vikundi vya wahuni wanaodai kuwa ni Makomandoo wa Yanga kwa ajili ya kuulinda uwanja na kupelekea kuzuia timu ya Simba sc isiingie uwanjani kufanya mazoezi.
Hebu thibitisheni uhusika wa Yanga. Maana taarifa zinasema mmezuiwa na meneja wa uwanja, je meneja wa uwanja ana husika nini na Yanga?
 
Meneja hana taarifa? Hajui kuwa kuna sheria inataka timu ikafanye mazoezi?
Kwa hiyo kama anajua ataota kuwa wanaenda kufanya saa 1 jioni au asubuhi? Au meneja wa uwanja naye anashiriki program za Simba? Kwani Simba wanatakiwa waachiwe uwanja na nani?
 
Back
Top Bottom