changaule
JF-Expert Member
- Jan 10, 2020
- 6,039
- 10,151
1) ni point ambazo zimepatikana kwa Kaizer Chief kuingia fainali klabu bingwa hivyo wamejikusanyia kiasi cha pesa cha dola 1,250,000Unaweza kueleza hizo points 25 zimemsaidia nini kaizer chief?
2) ni point ambazo zimewafanya kaizer chiefs wapande kwenye rank za Caf za misimu mitano. Hivyo pindi kama ataingia tena kwenye michuano ya kimataifa ndani ya misimu hii minne atakuwa na akiba ya point tano ambazo zitazidishwa na coefficient kulingana na mwaka husika ili kupata point, hivyo hataanza na point 0 bali anaweza kuwa ni point 5 ama 10, 15 au 20
3) ameweza kuingezea shirikisho lao la soka la Africa kusini point 25 ambazo zinasaidia kutoa rank za mashirikisho ambapo kwanzia namba 1 hadi 12 wanafanikiwa kuingiza timu nne katika michuano ya kimataifa.