DOKEZO Uozo: TBS imepoteza hadhi ya kuwa chombo cha kuratibu na kusimamia ubora nchini

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Anonymous

Senior Member
Joined
Apr 6, 2006
Posts
118
Reaction score
339
Kwa Kiswahili kinajulikana kama CHOMBO CHA KUSIMAMIA UBORA TANZANIA (TBS)
Jina zuri lakini la kizungu.. Sio tatizo sana

Jengo zuri la viwango
Mazingira mazuri ya Kazi
Vitendea Kazi bora
Maslahi, marvellous na mishahara yakuvutia LAKINI
Watendaji wake ni waovu, wanuka rushwa wasio na chembe ya uzalendo wa nchi yao

Asilimia 90 ya bidhaa za Tanzania zenye nembo na muhuri wa TBS ni magumashi tupu,, kuanzia kupeleka sampuli, kuzichakata majibu mpaka kupata cheti cha ubora ni rushwa na magumashi mwanzo mwisho
Jaribu kufuata taratibu halali za kupata cheti cha ubora uone utakavyosoteshwa kwenye zile corridor za lile jengo refu la ghorofa pale Ubungo Mataa.

Unaweza kumaliza mwaka hujapata cheti kutokana na sampuli kufeli, kuharibika ama kupotea na usumbufu mwingine mwingi tuu.

Kupata cheti kimoja cha ubora cha TBS ukiachana na ada halali rushwa ni kati ya milion 2 mpaka 5 kwa viwanda vya kawaida Wafanyakazi wa hii taasisi hawaishi kwa mishahara bali kwa rushwa na wanashindana kuvaa kubadili magari na simu za bei mbaya, bado mijengo na party za kila weekend.

Bidhaa nyingi zenye nembo ya ubora ya TBS hazijatimia zimepunjwa ujazo ama zimetengenezwa kwa malighafi hafifu ndio maana miradi mingi yenye ufadhili wa wazungu na inayosimamiwa na wazalendo wenye uchungu na nchi yao vifaa na malighafi za ujenzi huagiza nje ya nchi

Tunapohubiri uhujumu uchumi tusiwawazie tu wafanyabiashara bali na hawa waangalizi wa ubora tuliowaamini.

Soma Pia: Utitiri wa viwanda vya bati Tanzania na paa za nyumba zenye bati mijini kuwa na kutu ni Udhaifu mkubwa uliopo TBS

Inawezekana hii habari ikapata upinzani mkali lakini huo ndio ukweli na uhalisia

TBS imeoza..
 
Haya yote ni upumbafu wa connection!! Vijana wanaajiriwa kwa vimemo vya baba kantuma. Mkurugenzi anaogopa kumsema mtoto kisa baba yake mwenyekiti. Coma nyocle
 
Magufuli alizisimamia hizi taasisi zikafanya kazi leo hii taasisi zote za umma zimelala dolo hakuna anaejali na huwezi kufanya kitu sio TBS pakee taasisi zote zimerudi kulala.
 
Hili la ubora wa bidhaa ni janga kubwa sana kwa nchi yetu. Umenena vyema sana mkuu. Hao watendaji ni watu hatari sana kwa ustawi na usalama wa watanzania. Ubinafsi na ulafi wao umevuka mipaka, kwenye bidhaa za vyakula watanzania wanakula vyakula visivyo salama kabisa, hivi vipombe vya bei chee ni janga kiafya ingawa vimethibitishwa na TBS huku vikiwa si salama hata kidogo
 
Hali ni mbaya sana na Wakuu wa Serikalin wao wanaangalia kamba inapoishia. KAMA WALIVYOAMBIWA
 
 
BUNGE,BUNGE NA WABUNGE nao NI fekii...unategemea TBS, TBL,VMO ENERGY, KONYAGI, UHAI, KILIMANJARO, CEMENT, NONDO, NGANO, SUKARI, MCHELE, GARI, BARBARA, ELIMU, AFYA,BPHAMACY, MAHAKAMA, CCM😁, MSAJIR, TRA, BANK TELLER, HOTEL, TOUR, WANYAMA PORI, BUCHA, KARIAKOO, FERR, TPA, AIRPORT, SAMAKI,AJIRA, VISA, PASSPORT, SERIKALI ZA MITAA, PHD, PROFESSOR JALALA, BODI YA MIKOPO, TANZANIA, ZANZIBAR, MIGODIN, MIPAKANI, P9LICE, MUGAMBO, JWT, VIPODOZ, WACHINA, WAHINDI....AJIRA, TRAFIK, ..WAZEE NIHF, BETING,KAMALI, TV, BODABODA.KANISA,WALOKOLE, SADAKA...viwe Sawa?.
 
Yaan kama taifa tunaenda kuangamia cz hata vinywaji vingi mtaani ni fake ila hao TBS na TRA wamevipitisha kwa kuuza code zao kwa magendo...nmetangaza rasmi kutokunywa tena kinywaji chochote kilichozalishwa ndani kwa mustakabali wa afya yangu
 
Ni muda sasa TFDA irudishwe tu maana tokea TBS wamepewa suala la kudeal na suala la chakula na vidozi Sion kama wanaona linakipaombele kwao
 
Umesema kweli tupu. Makampuni ya hawa jamaa zetu MAGABACHOLI TBS zao ni za namna hiyo. " Sisi tuma veve TBS chukua cheti ya BORA hamuna pata kabisa, SHILINGI NGAPI TBS INATAKA" Ukishaambia ukapewa kiasi hicho siku hiyo hiyo unarudi nacho.
Jambo la kushangaza zile namba hazitaji Kampuni husika.
 
Binafsi, kwenye hizi product zetu za kula Niko na tahadhari sana ya kutumia, ni kweli kufa utakufa lakini siwezi kufa kijongoo kiasi Hiko, Nina karibu mwaka situmii juice Wala soda Wala bia. Pesa tunazipata Kwa maarifa mengi sana...Bora tupunguze sumu kidogo, hata kama tutakula sumu lakini si Kwa kiasi kikubwa hivyo.
 
Ni kama umeamua kuandika ukutani Kwa kutumia kinyesi chako. Embu fafanua vzuri. Bidhaa yako kufeli unamlaimu nani kiongozi. Embu tupe uthibitisho kwamba uliipima bidhaa yako kiwandani na ikafaulu, then ukapeleka TBS ikafeli. Wengi wenu mnazalisha bidhaa hajui au hamna uhakika na ubora wa bidhaa zenyewe. Je unataka ifaulu ata kama imefeli ili imfuraishe nani?
 
TBS is just like a National Disgrace in this country.
Tanzania has become the Major Damping Site of the Waste products from China and from within the country.
 
Yaan kama taifa tunaenda kuangamia cz hata vinywaji vingi mtaani ni fake ila hao TBS na TRA wamevipitisha kwa kuuza code zao kwa magendo...nmetangaza rasmi kutokunywa tena kinywaji chochote kilichozalishwa ndani kwa mustakabali wa afya yangu
Walau Konyagi wanajitahidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…