Upande wa pili wa mkataba wa DP world, Mchina na wadau wake wamepigwa bao dakika za majeruhi

Upande wa pili wa mkataba wa DP world, Mchina na wadau wake wamepigwa bao dakika za majeruhi

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Ni kama vile kuna vita baridi ya kugombea Afrika kati ya Marekani (pamoja na mataifa mengine ya magharibi) dhidi ya China. Kila mmoja anajitahidi kuongeza ushawishi wake barani Afrika kupitia vitu kama uwekezaji, misaada N.K

Kwenye hili la mkataba wetu na DP World ni wazi kuwa mchina amepigwa bao dakika za majeruhi.
China ilikuwa na mpango kabambe wa kuwekeza katika bandari kubwa zaidi pale Bagamoyo, laiti wangefanikiwa kwenye hili basi ingewaongezea sana ushawishi wa kiuchumi na kisiasa nchini kwetu na ukanda mzima wa Afrika mashariki.

Sasa kwa masharti yale ya ule mkataba wetu wa IGA sidhani kama kuna mpango wowote wa kuendelea na ule mradi. DP World hawezi kuja kuwekeza mabilioni ya fedha kwenye bandari ya Dar alafu mtu mwingine ajenge bandari pale Bagamoyo na kuleta ushindani.

Kama mnavyojua UAE ni mdau wa karibu sana wa Marekani, na Marekani ni bingwa wa kutumia mataifa mengine kulinda maslahi yake. Ni wazi kuwa kwenye hili Mabeberu wameibuka kidedea. Mchina na wadau wake waliokuwa wanaupigia chapuo ule mradi wa Bagamoyo wamepigwa bao la kisigino.
 
Mchina tumpe Southern Highland corridor ajenge Motorway ya njia sita hadi Tunduma halafu aweke vibanda akusanye RoadToll mpaka arudishe fedha zake na faida nono ndipo atukabidhi Barabara yetu.
 
Ni kama vile kuna vita baridi ya kugombea Afrika kati ya Marekani (pamoja na mataifa mengine ya magharibi) dhidi ya China. Kila mmoja anajitahidi kuongeza ushawishi wake barani Afrika kupitia vitu kama uwekezaji...
uko sahihi wamerekani ni wazuri sana kwenye entrepreneurship skills development kwahiyo wanacho fanya ni kuzitafuta fursa, (opportunity seekers).

They know how to break the ice and will not leave the office without getting what they want
 
Ni kama vile kuna vita baridi ya kugombea Afrika kati ya Marekani (pamoja na mataifa mengine ya magharibi) dhidi ya China. Kila mmoja anajitahidi kuongeza ushawishi wake barani Afrika kupitia vitu kama uwekezaji, misaada N.K

Kwenye hili la mkataba wetu na DP World ni wazi kuwa mchina amepigwa bao dakika za majeruhi.
China ilikuwa na mpango kabambe wa kuwekeza katika bandari kubwa zaidi pale Bagamoyo, laiti wangefanikiwa kwenye hili basi ingewaongezea sana ushawishi wa kiuchumi na kisiasa nchini kwetu na ukanda mzima wa Afrika mashariki.

Sasa kwa masharti yale ya ule mkataba wetu wa IGA sidhani kama kuna mpango wowote wa kuendelea na ule mradi. DP World hawezi kuja kuwekeza mabilioni ya fedha kwenye bandari ya Dar alafu mtu mwingine ajenge bandari pale Bagamoyo na kuleta ushindani.

Kama mnavyojua UAE ni mdau wa karibu sana wa Marekani, na Marekani ni bingwa wa kutumia mataifa mengine kulinda maslahi yake. Ni wazi kuwa kwenye hili Mabeberu wameibuka kidedea. Mchina na wadau wake waliokuwa wanaupigia chapuo ule mradi wa Bagamoyo wamepigwa bao la kisigino.
Umeona mbali. Ila zikijengwa au kuendelezwa zote mbona MSWANO (Kwa sauti ya Kigogo watani zangu)
 
Umeona mbali. Ila zikijengwa au kuendelezwa zote mbona MSWANO (Kwa sauti ya Kigogo watani zangu)
Ni kweli, lakini hiyo itawezekana kama zitaendeshwa na mtu mmoja. Hata wachina miongoni mwa masharti yao ilikuwa ni tusiendeleze bandari nyingine yoyote kama wakijenga ya Bagamoyo. Kwa kifupi watahitaji kuhakikishiwa usalama wa uwekezaji wao dhidi ya ushindani wa aina yoyote.
 
Mchina tumpe Southern Highland corridor ajenge Motorway ya njia sita hadi Tunduma halafu aweke vibanda akusanye RoadToll mpaka arudishe fedha zake na faida nono ndipo atukabidhi Barabara yetu.
Ni njia moja wapo ya kuharakisha maendeleo.
 
Bandari ya Bagamoyo ndo byebye.

USA kupitia CIA atakuwa kamtumia mshirika wake yaani mwarabu wa Dubai kumkatia denge mchina, Ndiyo maana mkataba huu una kila sign ya kikoloni mkongwe
It's a new scramble for Africa. Cha muhimu ni sie waafrika tuhakikishe maslahi yetu yanazingatiwa na sio kuibiwa kizembe.
 
Sema mchina nae tusim write off mapema nae ana mbinu zake za kivita linapokuja swala la uwekezaji wa kihuni.. JPM aliwabania kwenye kandarasi ya SGR ila mwisho wa siku nadhani ndo wenye kazi kubwa wamempita mturuki.
 
Ni kama vile kuna vita baridi ya kugombea Afrika kati ya Marekani (pamoja na mataifa mengine ya magharibi) dhidi ya China. Kila mmoja anajitahidi kuongeza ushawishi wake barani Afrika kupitia vitu kama uwekezaji, misaada N.K

Kwenye hili la mkataba wetu na DP World ni wazi kuwa mchina amepigwa bao dakika za majeruhi.
China ilikuwa na mpango kabambe wa kuwekeza katika bandari kubwa zaidi pale Bagamoyo, laiti wangefanikiwa kwenye hili basi ingewaongezea sana ushawishi wa kiuchumi na kisiasa nchini kwetu na ukanda mzima wa Afrika mashariki.

Sasa kwa masharti yale ya ule mkataba wetu wa IGA sidhani kama kuna mpango wowote wa kuendelea na ule mradi. DP World hawezi kuja kuwekeza mabilioni ya fedha kwenye bandari ya Dar alafu mtu mwingine ajenge bandari pale Bagamoyo na kuleta ushindani.

Kama mnavyojua UAE ni mdau wa karibu sana wa Marekani, na Marekani ni bingwa wa kutumia mataifa mengine kulinda maslahi yake. Ni wazi kuwa kwenye hili Mabeberu wameibuka kidedea. Mchina na wadau wake waliokuwa wanaupigia chapuo ule mradi wa Bagamoyo wamepigwa bao la kisigino.
Naunga mkono hoja, kitu kama hiki nilikuona, nikakinote na kuwaambia watu humu Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee!
Wanabodi,
  1. Jambo jingine, kuna kipengele cha kuizuia nchi isiendeleze Bandari nyingine, hivyo kuiweka mashakani Bandari ya Bagamoyo, hili halikubaliki hata kidogo!.
Hitimisho
Kwa vile Rais Samia ana nia njema ya dhati kuisaidia nchi yetu, wasaidizi wa rais na sisi Watanzania wengine wote tuna wajibu wa kumsaidia rais wetu na kulisaidia taifa letu na huu ndio uzalendo wa kweli.

Paskali.
P
 
So far Mchina ana ushawishi mkubwa hapa Afrika miradi mingi ya ujenzi wa miundombinu inafanywa na makampuni ya China
Kuongeza ushawishi ni jambo endelevu, kuna maeneo China amejitahidi lakini overall Marekani ana ushawishi wa hali ya juu mno nchini.
 
Back
Top Bottom