Upasuaji wa Mgongo kwa Njia ya Matundu wafanyika Dar, Wagonjwa 13 wafanyiwa upasuaji

Upasuaji wa Mgongo kwa Njia ya Matundu wafanyika Dar, Wagonjwa 13 wafanyiwa upasuaji

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Kufuatia Kongamano la Kimataifa la Madaktari Bingwa wa Ubongo na Mgongo na Mishipa ya fahamu (Global Neurosurgery course) imeelezwa limechangia Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) kuanzisha huduma ya upasuaji wa mishipa ya mgongo kwa njia ya matundu (Endoscopic neurospine surgery).

Kongamano hilo lililoandaliwa kwa ushirikiano Kati ya Taasisi ya MOI na Chuo Kikuu cha Weill Cornell cha Marekani limeshirikisha ambapo ya Wataalam 120 wanashiriki kutoka Mataifa mbalimbali Duniani limefanyika Jijini Dar es Salaam.
WhatsApp Image 2024-03-28 at 17.30.22_c8183921.jpg

WhatsApp Image 2024-03-28 at 17.30.23_0f82bcf2.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya MOI, Prof. Abel Makubi amesema tayari Wagonjwa 13 wa mgongo wamefanyiwa upasuaji kwa mafanikio katika siku mbili (Jumatano na Alhamisi) toka kuanza kwa huduma hiyo.

Amesema uanzishwaji wa huduma hiyo inayotumia teknolojia ya kisasa inayotawala Dunia kwa sasa na itasaidia kuwapunguzia Wananchi gharama za kufuata matibabu ya aina hiyo nje ya nchi na kukuza tiba utalii hapa nchini.

“Hii ni kwa mara ya kwanza kwa MOI na ni mara ya kwanza kwa Taifa kufanya upasuaji wa mgongo kwa kutumia matundu (Endoscopic Spine Surgery), kwa dhati tunakishukuru Chuo Kikuu cha Weill Cornel cha Marekani kwa ushirikiano huu muhimu na kwa niaba ya menejimenti naahidi tutauenzi,” amesema Prof. Makubi.
WhatsApp Image 2024-03-28 at 17.30.25_5bfe3887.jpg

Prof. Abel Makubi
WhatsApp Image 2024-03-28 at 17.30.24_9da511de.jpg

Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Ubongo, Uti wa Mgongo na Mishipa ya Fahamu kutoka Taasisi ya MOI, Dkt. Hamisi Shabani

Upande wake Mkurugenzi wa Upasuaji wa Mgongo kutoka Chuo Kikuu cha Weill Cornel Marekani, Prof. Roger Hartl ameahidi kuendeleza ushirikiano na Taasisi ya MOI katika kuendelea kuwajengea uwezo wataalam, kuwezesha tafiti za kisayansi na vifaa tiba vya upasuaji ili iweze kuwa kituo mahiri cha upasaji wa mgongo barani Afrika.

“Lengo letu kuiona MOI ikiwa kituo cha umahiri kwenye kutoa tiba na mafunzo kwa mataifa mengine juu ya upasuaji wa mgongo kwa kutumia matundu, nimefurahi kuona namna ambavyo MOI inathamini ushirikiano wetu na ninaahidi kuuendeleza,” amesema Prof. Hartl
WhatsApp Image 2024-03-28 at 17.30.27_f83248e2.jpg

Prof. Roger Hartl
 
Hongera Serikali kwa maboresho mengi ktk sekta ya afya licha ya changamoto za hapa na pale.

Taasisi ya mifupa MOI ni taasisi yenye mapana ktk utoaji tiba kwa kuzingatia takwimu za ajali,magonjwa mtambuka yanayohitaji specialised treatment..Hivyo eneo na miundombinu ya sasa bado ni finyu lichs ya uwekezaji mkubwa na upanuzi.

Nashauri kutengwe eneo kubwa la ekari 25 mpaka 100 nje ya jiji kisha ijengwe Hospitali kubwa ya kisasa yenye huduma na vitendea kazi vya kisasa.

Gharama za matibabu MOI ni kubwa sana kwa sasa na Watanzania walio wengi wanashindwa kumudu ama kuzimudu kwa mahangaiko makubwa..Upo utaratibu wa kusamehe wagonjwa wasio na uwezo -HONGERA KWA SERIKALI YETU.

Tatizo ni hizi taasisi za Afya Muhimbili ikiwemo ni kuelemewa na madeni ya wazabuni na kupekelea huduma kuzorota..Ktk hili nadhani kunapaswa kuwa na namna sahihi ya Serikali kuongeza fungu la fedha la kulipia misamaha inayotolewa kwa wagonjwa,ndugu wa wafu wasio na uwezo mara baada ya kuhudumiwa.

Mungu ibariki Tanganyika,Zanzibar na JMT
 
Back
Top Bottom