UPDATE: Boniface Jacob kuendelea kusota rumande baada ya jeshi la Magereza kukosa usafiri wa kumfikisha Mahakamani Kisutu kusikiliza dhamana yake

UPDATE: Boniface Jacob kuendelea kusota rumande baada ya jeshi la Magereza kukosa usafiri wa kumfikisha Mahakamani Kisutu kusikiliza dhamana yake

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Hatima ya dhamana ya Boniface Jacob "Boni Yai," itajulikana leo, Septemba 23, 2024, wakati Mahakama itakapotoa uamuzi kuhusu maombi ya Serikali ya kuzuia dhamana yake. Boni Yai alikamatwa na kuletwa mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, ambapo alikabiliwa na mashitaka mawili, ambayo aliyakana.

Upande wa mashitaka, ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga, ulieleza kwamba upelelezi bado haujakamilika na kuwasilisha maombi mawili: moja ikihusisha kuingiliwa kwa vifaa vya kielektroniki vya mshitakiwa na nyingine ikidai kuzuia dhamana kwa ajili ya usalama wa mshitakiwa.

Katuga alidai Yai alieleza kuwa anajua atatekwa na kuuawa. Hata hivyo, mawakili wa utetezi, wakiongozwa na Peter Kibatala, walipinga maombi hayo wakidai kuwa yalifanywa kinyume cha sheria na yana kasoro.


UPDATE
Uamuzi wa dhamana ya Meya wa zamani wa Ubungo, Boniface Jacob 'Boni Yai' umekwama kutokana na Jeshi la Magereza kushindwa kumfikisha katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kilichoelezwa mahakamani hapo kuwa hakuna usafiri wa kumfikisha mahakamani hapo.

Mahakama hiyo itatoa uamuzi tarehe 26 Septemba 2024, siku ya

---

Pia soma
 
Usafiri umekosekana

Screenshot_20240923-131731.jpg
Uamuzi wa dhamana ya Meya wa zamani wa Ubungo, Boniface Jacob 'Boni Yai' umekwama kutokana na Jeshi la Magereza kushindwa kumfikisha katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kilichoelezwa mahakamani hapo kuwa hakuna usafiri wa kumfikisha mahakamani hapo.

Mahakama hiyo itatoa uamuzi tarehe 26 Septemba 2024, siku ya

Pia soma:Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imepanga kutoa uamuzi wa dhamana Boniface Jacob, septemba 23, 2024
 
Wakati maandamano ya CHADEMA yakiendelea kushika kasi Hakimu Kiswaga ameahirisha kesi ya Meya huyo wa zamani mpaka Alhamisi, Septemba 26, 2024.

Uamuzi wa dhamana ya Meya wa zamani wa Ubungo, Boniface Jacob 'Boni Yai' umekwama kutokana na Jeshi la Magereza kushindwa kumfikisha katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kilichoelezwa mahakamani hapo kuwa hakuna usafiri wa kumfikisha mahakamani hapo.

Jacob, mkazi wa Msakuzi, mfanyabiashara na mwanasiasa anakabiliwa na kesi ya uchapishaji taarifa za uongo kwenye mitandao, kinyume cha Sheria ya Makosa ya Mtandao namba 14 ya mwaka 2015.

Alipandishwa kizimbani mahakamani hapo Alhamisi, Septemba 19, 2024, na upande wa mashtaka pamoja na mambo mengine, uliiomba Mahakama izuie dhamana yake kwa madai ya usalama wake mshtakiwa, hoja zilizopingwa na jopo la mawakili wake likiongozwa na Peter Kibatala.

Baada ya mvutano wa hoja za mawakili, Hakimu Mkazi Mfawidhi, Franco Kiswaga aliahirisha mpaka leo Jumatatu, Septemba 23, 2023 saa 5:00 asubuhi kwa ajili ya dhamana lakini Boni Yai hakufikishwa mahakamani.
 
Usafiri umekosekana

Uamuzi wa dhamana ya Meya wa zamani wa Ubungo, Boniface Jacob 'Boni Yai' umekwama kutokana na Jeshi la Magereza kushindwa kumfikisha katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kilichoelezwa mahakamani hapo kuwa hakuna usafiri wa kumfikisha mahakamani hapo.

Mahakama hiyo itatoa uamuzi tarehe 26 Septemba 2024, siku ya

Pia soma:Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imepanga kutoa uamuzi wa dhamana Boniface Jacob, septemba 23, 2024

Samia ni Magulifuli part two ..... Haya haya ndiyo yaliyokuwa yakitokea awamu ya 5!!
 
Back
Top Bottom