Awali ya yote napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza Rais wetu Dr. John Joseph Magufuli kwa jitihada nyingi anazo zifanya katika kuipeleka nchi yetu kwenye nchi ya uchumi wa kati. Hata hivyo sina budi kutoa masikitika yangu kwa watendaji wake anao waamini kuto kuwa na uwezo wa kukabilina na janga la mafuriko ya kila mwaka.
By the way by definition:
Civil engineering is an engineering science that deals with the conception, planning, design, construction, calculation, manufacture and operation of buildings in civil engineering, transport and hydraulic engineering.
Sasa mbona inakuwa ni aibu kubwa sana kwa wasomi wetu wa hicho kitivo cha Civil Engineering kuendelea kujiona kama ni Ma-Professor na Ma-Engineer wakati ambapo hamna uwezo wa kulisaidia Taifa letu kutatua matatizo kama haya ya mafuriko yanayo tokea kila mwaka. Ni maengineer gani nyie ambao hmtambui wajibu kama wabobeaji wa maswala haya? Mnatia aibu kiasi kwamba hata sisi maengineer wa Faculties nyingine kama Mechanical, Elictrical na wengineo tunaoneka vilaza kama nyie.
Masikitiko yangu makubwa yawaende watu wanao jiita Ma Professor, wahandisi na wasomi wa vyuo vikuu vyetu vya Faculty ya Civil Engineering nchini kwa kushindwa kukabilina na changamoto kama hii ambayo kila mwaka ina wahathiri wakazi wa jiji letu la Dar es salaam na hivyo kuifanya nchi nzima iwe paralyzed.
Professor Mbalawa, Engineer Kamwelwe, Maprofessor na wahandisi wote mlio maliza na ambao bado mko masomoni kwenye Kitivo cha Civil Engineering wa vyuo vikuu nchini, mnadhani kuna umuhimu wa watanzania kuendelea kugharamia Faculty hii ya Civil Engineering kwenye vyuo vyetu?
Mimi inaniwia vigimu sana kuelewa kwa nini wasomi na wataalam walio bobea wa kitengo hiki cha ujenzi kushindwa kuthibiti hali hii ambayo kila mwaka hutokea na kuathiri maisha, mali na shughuli zetu wenyewe. Kama wasomi na wataalam mnaweza kulala vizuri na kwa amani kweli?
Professor Mbalawa na Engineer kamwelwe, Maprofessor na Ma-Engineer wengine wa hii Fuculty ya Civil Engineering na watu wa mipango miji wa mkoa au Taifa mnashindwa kweli kushauriana na Rais Magufuli na mawaziri wengine wanao husika kuacha mara moja miradi yote mingine ambayo iko katika pipe line ya mpango wa kutekelezwa, ili kuanza mara moja uwezekano wa kutafuta jawabu la hii changamoto ambayo ina wafanya wananchi wote kuwa paralyzed na maafa haya ya mafuriko kila mwaka? Kama mvua ya masaa machache inasababisha maafa ya aina hiyo je mvua za siku tatu mfululizo zita leta maafa ya namna gani?
Hivi, hamjitabui kuwa nyie ndiyo malaika wa nchi yetu, na kwamba ustawi wa miji yetu inawategemea nyinyi? Sasa kama nyie malaika wetu kwa vipaji mlivyo navyo, uwezo mlio nao na utashi wenu collectively mnashindwa kujituma kukabilina na matatizo haya, mnategemea nani atayatatua? Na je, mnategemea serikali inayo tawala na wananchi kwa ujumla wataweza kuwaamini nyie na kuwapa miradi ambayo kila mara mnashindwa kuitekeleza kwa ufanisi unao takiwa? Mnataka watu wawe wanawazomea kama wana CCM awamu ya nne walivyo kuwa wakinyanyasika kwa kuzomewa na kuwa mocked wakionekana wamevaa magwanda yao ya kijani na yellow?
Hivi, kitendo cha kukahidi au kushindwa kutekeleza wajibu wenu kama wataalam, mnadhani mnamkomoa nani? Hamjui kuwa nyie ndiyo watu mnaotakiwa kulisimamia Taifa letu lika imarika kwa manufaa yetu sote na vizazi vyetu vya baadae?
Kwenye daraja kama hili la Mbezi ya chini kuna ugumu gani kulitengeneza likawa imara na kudumu mda mrefu? Na hela ambazo serikali inge serve zingeweza kutumika katika maeneo mengine ambako hakuna miundo mbinu mizuri na watu kupata shida?
Lawama nyingine ningependa ziwaendee watendaji na watumishi wa serikali wanao husika na maswala ya uokoaji. Ina maana vitengo vyote vya serikali vinavyo husika na maswala ya uokoaji kama Zimamoto na vinginevyo vilishindwa kweli kupeleka wataalam na vifaa kwenye maeneo ambayo wana yaona critical?
Scene kama hii ina maana kikosi cha zimamoto kilishindwa kweli kupeleka wataalam na vifaa vinavyo husika kwa kazi hiyo ili kumwokoa huyu mwana dada kutoka kwenye hilo janga? Kama huyu mwana dada alikaa mda mrefu bila kuokolewa na Fire Briged, kunafaida gani kuendelea kuwa na kitengo kama hiki ambacho hakina faida kwa wananchi? Si afadhali hiyo kazi ikapewa private sector ikatoa Service nzuri kwa umma? Jangwani yote sijaona gari la zimamoto na wanajeshi wa zima moto wakiwa stand by. Ni polisi tu ambao walikuwa wakizuia watu wasipite na hiyo baadae sana.
Mimi nashindwa elewa inakuwaje mtu anapewa mafunzo ya kuperform task fulani na kuwa specialist, halafi kwenye incidents kama hizi, ambapo anatakiwa kuwajibika, anashindwa kutekeleza wajibu wake ambao umma umemwamini na badala yake kujichimbia kwenye ofisi zao au nyumba zao. Watu kama hawa watakuwa na akili gani hasa ya kukosa uelewa na wajibu wa kutekeleza kazi zao?
Kwa swala hili la kukosa utendaji wa majukumu waliyo pewa, ningependa kusikia majibu ya watumishi wa serikali wanao husika na maswala ya uokoaji, nini hasa mpangilio wao wa kazi, kiasi kwamba wakakosa ile uhodari na ujasiri wa kujituma kufanya kazi zao kwa Passion?
Rais Magufuli nakuomba hii hali ya kutopenda kjituma na kuwajibika kwa watu walio pewa dhana na umma inayoendelea nchini, kuiangalia kwa makini sana, maana inaonyesha kana kwamba kwenye jamii yetu kuna ugonjwa umetuingia ambao unatufanya sisi kuwa unconcerned. Hatu react ipasavyo katika Situation knapp bidi kufanya hivyo.
Watanzania tumekuwa watu wa porojo sana na wavivu katika kuwaza na kutenda pindi inapo bidi. Tukiendelea hivi sita shangaa wala kustaajabu kusikia kuwa vizazi vyetu huko mbele vinashindwa kukabilina na matatizo yanayo wahusu wao, na hivyo kukubali kirahisi kuwa watumwa tena wa vizazi vya wenzetu tunao dai wametuzidi maarifa.
Ombi langu kwa Rais Magufuli, tafadhali itisha mkutano wa wahandisi wote na maprofessor wote nchini ili tuli jadili hili tatizo la kukosa uwajibikaji wa wahandisi wetu. Huo mkutano usiwe wa siku moja unaweza ukachukua hata wiki moja ili wahandisi wengi wapate nafasi ya kujieleza na kutoa mawazo yao ili tujie nini kifanyike ili kurudisha ile hali iliyo kuwepo enzi ya Mwalim Nyerere.
Kingine wape maengineer wetu wajibu wa kusimamia na kuchimba bonde la Msimbazi kwa uwezo wao wenyewe na kulifanya liwe bahari mpaka Surrender na kuwa tuorist attraction. Wakishindwa hiyo project basi ningekushauri kitivo chote cha Civil Engineering kwenye vyuo vyetu kifutwe completelly na wanafunzi watakao chukua masomo hayo wapelekwe kusoma nje.
Inatisha! Maengineer wazima wanashindwa hata kuweka Dimensions za kutengeneza ma-Culvert?
Ni aibu kubwa sana!
Ni aibu kubwa sana!
Ni aibu kubwa sana!
Ni aibu kubwa sana!
Ni aibu kubwa sana!
Sent using
Jamii Forums mobile app