Elections 2015 Updates: Mchakato na Matokeo ya kura za maoni ya Ubunge CCM nchini kote

Elections 2015 Updates: Mchakato na Matokeo ya kura za maoni ya Ubunge CCM nchini kote

Wacha maneno yako, unasemaje in aibu wakati mwenzako nyota yake ndo ishang'aa..na raia wamemwelewa vibaya mno..?!

Bora huyu ajiite ana nyota kuliko mama ubaya maana pamoja na skendo zote bado hajafua dafu.
 
Dhambi ya wizi wa kura itaendelea kuwatafuna, mtu akishaanza kuiba kura haachi maana ushindi wa wizi unakuwa umeshamnogea.
 
Kwenye mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM,yamejitokeza mambo mbalimbali yanayoashiria goli la mkono. Mchakato huo umeanika mambo ya kujipatia kura na kuzuia kura za wengine.

Mfano,kumeripotiwa kutolewa kwa rushwa na hata kukamatwa kwa wagombea mbalimbali. Pia,kumekamatwa kura feki Tarime na kutotangazwa kwa matokeo Buguruni. Bunda,matokeo yalitangazwa chini ya ulinzi mkali. Tena,kumetokea kupigana au kupigwa Bunda na hata Kongwa kwa Ndugai.

Wapo walioambiwa wana kadi feki Arusha na hata waliokamatwa na kadi feki Ilala. Kimsingi,mambo hayo ni mafunzo tosha kwa wapinzani kuelekea uchaguzi mkuu. Mambo hayo ndiyo mambo ya goli la mkono. Shtukeni!
 
Mhe Charles Kitwanga Mawematatu kashinda kwa kishindo naye ndani ya kura za maoni CCM katika Jimbo la Misungwi.

Hawa wawili wako vizuri sana nawakubali kwa kweli. prof. Muhongo kila la kheri. Mh. Simbachawene kila la kheri pia.
Bado Mh. Mawematatu pia naamini atakuwa amepita pale Misungwi.

Nyote Kila la Kheri Katika Uchaguzi Mkuu.
 
BLUE: Tofautisha ushindi kwa kata na kwenye kura za maoni ndani ya chama...
YELLOW: Bado hajawa muwakilishi kwa wananchi, ila wananchi wachache kupitia chama kimoja cha siasa ndiyo wamefanya uteuzi.
JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI, WILAYA YA MUSOMA-MKOA WA MARA

Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Mhe Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo ameibuka mshindi katika kura za maoni ndani ya CCM kwa kupata ushindi wa kishindo katika kata zote 21 za Jimbo la Musoma vijijini.

Hongereni sana wana musoma vijijini kwa kuamua kuanza kujenga uchumi imara na kuutokomeza umasikini kwa kuchagua mwakilishi bora atakayesukumu gurumu la maendeleo kikamilifu pasipo shaka yoyote ile. Hongera sana Profesa Muhongo kawatendee haki wana Musoma vijijni na watanzania wote kwa ujumla.
Alafu atakuwa mwakilishi bora akipewa ridhaa ya uwakilishi kupitia ubunge na kuwasilisha bajeti ya ukarabati wa barabara ya Musoma to Majita ambayo imesahaulika kwa miongo kadhaa sasa.
 
Sikuizi Bungeni wala hakushtui kama zamani hadhi ya bunge imekwisha,sio kwasababu amepata Owoya au mwengine yoyote lakini haiko kama zamani,pamekua sehemu ya mipasho kama Dar live au lango la Jiji..........
 
Kama huna mvuto ni ngumu kuwa mbunge wa viti maalum,dah ndio maana bungeni posho za wabunge hazitoshi.
 
kinachotushangaza sisi kina gogo la shamba ni pale waandaaji wa kipindi cha tuongee asubuhi kinachoandaliwa na Star TV wanapoliongelea jambo hili huwa wanalifanya ni la vyama vyote wakati linafanyika kwenye chama vha ccm pekee
 
Sasa na zile picha za bikini kwenye internet, kweli jamani?
Hakuna kipengele cha maadili hapo.
 
Kuna watu wa ajabu sana, hivi mnafikiria bungeni ni sawa na location ya kutengeneza movie, eti hongera sana Irene, ndio maana hii nchi haitakuja kuendelea, maana usanii mpaka kwenye maswala la Msingi. Wana Tabora kwa hilo mmepotea.
 
Kaona fursa kaitumia hongera sana m bongo muvie
 
Back
Top Bottom