Updates: Upo maeneo gani, matukio gani kuelekea kuingia mwaka mpya 2018?

Nrangoo

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2017
Posts
3,407
Reaction score
5,418
Habari wanaJukwaa

Zikiwa zimebakia saa chache sana kabla ya Kuaga mwaka 2017 na kukaribisha mwaka mpya 2018.

Tupeane taarifa za matukio yanayojiri katika shamrashamra Hizi..
 
Nipo Coco beach na Wana familia wangu ninaoishi nao kwa Sasa!

Hii ni mbinu yangu kongwe kudhibiti waruka fensi na kwenda kusikojulikana usiku wa Mikesha

Hapa ni Kama Jeshini kwangu ni mwendo wa kuhesabu namba, najua wapo wanaonilaani sana lakin ni kwa Nia njema tu!

Tumezungusha Mduara wa Viti na Soft drink na Kahawa kwa sie wengine na kibaridi hiki japo kwa pemben yetu kizazi cha Firauni nacho hakijaadimika wapo

Nyakati hizi huwa pia najikumbusha Ndugu na Jamaa zangu ambao Miaka ya Nyuma tarehe Kama Hii tulikuwa nao eneo hili Miaka kadhaa iliyopita lakin Leo Hii miili Yao ni sehemu ya Matabaka ya udongo
 
Niko village napata za kienyeji. Huku hakuna makonda wala polisi tutakula nyama choma na pombe mpaka mwakani saa sita
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…