Updates za kifo cha Afande Luteni Kanali Muna aliyeuawa Kawe kwa kuchomwa kisu na dereva bajaji Kato

Ngoma ikilia sana inaelekea kupasuka, kuna nyuzi nyingi sana hapa JF zinazoonesha hawa JEIWII(baadhi) kukosa weledi, busara na kunyanyua mabega kwa wananchi wa kawaida. Aibu ni kupoteza mtu mkubwa (tarajali) kama huyu kizembe kama hivi.

Kwa nini mujisikie fahari kupiga watanzania wenzenu kwa mwamvuli wa uanajeshi? Na nyinyi mnaopiga wananchi hapo Kawe hamuoni kuwa munadhulumu wasio na hatia matokeo yake munatengeneza chuki dhidi ya wananchi!!!
Kama ameua Kato kwa nini mupige wote? Ulimbukeni na ushamba.
 
Mie niliwahi poteza wana kwa ubabe wa kijinga jinga ,pale Ambrosia ,kawe ya chini
Pale Bar one ,enzi zile za kinje

Ukiwa na familia kuwa mpole kuwa mwanadiplomasia
Kinje alikuwa mtu wa aina gani ujanani ? Leta story bana, alafu siku hizi uzi wetu wa usiku wa manane bado upo nao ?
 
Sasa naye marehemu kwanini ampige dogo makofi sasa ndo hayo madhara yake
Mimi naona tusubiri info zaidi, labda hata bajaji alitumia kauli mbaya, askari wote tu jwtz na police lazima aone dharau sana kujibiwa vibaya na raia
Nimesoma sehemu kwamba huyo askari alikuwa kwenye process za kutoa gari lake
 
Watu wengi wanatoa lawama kwa Mwanajeshi. Kwa kuwa ana hiyo title ya MWANAJESHI.

Juzi hapa nilikuwa Kkoo, mbele kuna folen na gari yangu ipo usawa wa makutano yaani (T) sasa kuna Wale wanoendesha GUTA akawa ana haraka zake upande wa ubavuni, akawa anafokafoka pale nimpishe wakati mbele kuna gar imesimama na anaona.

Mie nikakaa kimya, akaona haitoshi, akaanza kupiga body la gari ubavuni tena kwa nguvu. Sasa na mm nikawa hasira tyr zishanijaa kichwani namsubiri aje upande wangu nimshike shingo niendeshe gari nimburuze.

Gari ya mbele ilisogea umbali mrefu tu na mimi sikusogeza gari namsubiri aje upande nilipo. Kwel bhana akajichanganya kuja dirishan kwangu kuchungulia, na mm nikashusha kioo sikuongea sana nilishika kichwa kile nikamvutia ndani alafu nikavuta wese.. nilimburuza sana.. naona siku nyingine hatorudia.
 
Tusisahau pia kumtaja yule mwizi wa bajaji ya Kato ambaye alikuwa ameonekana, na Kato ndio alikuwa anamuwahi.

Katika ulimwengu wa kiroho, kuna wezi huwa hawakamatwi kirahisi kwa kuweka vizingiti.

Jez huyo mwizi wa bajaji ndio kasevu tayari au?
 
Hii iwe fundisho kwa pande zote
 
Kama naskia mwingine kadungwa bisu la mkund*** Maana huwezi kunipiga mbele ya wanangu na mke wangu nikiwa nyumban kwangu tena nyumba niliyojenga kwa pesa zangu. Bro tutakufa wote na hamna anaejua kifo chake kitakuwaje ko hapo ndio nitaamini ni mwisho wngu ila lazima nife na maboya wawili au wa tatu, au yeyote atakaeingia18
 
Huyu lt col ilitakiwa avuliwe cheo kabla ya kuzikwa arudishwe kwenye umeja.

Amelitia hasara taifa kwa kukosa ueledi wa majukumu yake.

Amekufa kizembe sana kwa kutojitambua kwamba yeye ni kiongozi.

Malipo ya mjinga ni hasara
 
Una mwandiko mbaya sana haivutii kusoma, halafu ndio zao la SAUT
Sema ana uandishi mbaya sio mwandiko mnaya. Mwandiko hauusiani na alama za uandishi na upangaji wa maandishi.
Mwandiko ni muunganiko wa herufi tu, na upo wa kuchapa na kuunga wengine huita mcharazo na wima..
Mwandiko mbaya ni ule usiosomeka .
Je mwandishi mwandiko wake hausomeki ?
Mpo wengi sana mnaoshindwa kutofautisha mwandiko na uandishi.
Soma la Insha lilikupita kushoto ila unajifanya unajua kukosoa.
Huwa sipendi mnavyochanganya insha na mwandiko? Mwandiko ni 'subset" ya insha
UANDISHI !UANDISHI!
Ndio maana wanahabari wanaitwa waaandishi wa habari hawaitwi wanamwandiko wa habari, kwa sababu wanaandika habari sio mwandiko( mwandiko ni tool ).
Mwandiko ni art of making letters.
Mwandiko ni somo la chekechea na drs la kwanza.
Uandishi in sanaa ya kuunda maneno ssentensi a insha kwa kuzingatia kanuni zote za uandishi.
Picha hii ni somo la kusoma na kuandika. Mtoto ataunda hizo herufi bila kujali zinaleta maana au la na baadae kuunganisha ili kipata maana na kusoma maneno yatayoundwa na herufi hizo.


 
Vikosi visivyojielewa ni vipi hivyo au unamaanisha malezi mkuu
Kiufupi wanajeahi wetu wengi hawajitambui, kazi kama hizo za kusaka na kukamata wahalifu zinahusu polisi maswala ya kupiga watu hayo ndio kabisaaa hayawahusu labda kukiwa na tukio fulani ambalo wao watahitajika. Sasa unakuta mwanajeshi yupo bar analeta ubabe kisa kazi yake haya mfano huyo aliekufa kaenda kizembe tu ww unagari unabishana nn na mtu wa bajaji basi angalia hata hadhi yako cheo ulicho nacho ya nini ukabishane au utake kumpiga dereva bajaji hii ni kutojiamini na ni udhaifu mbaya sana kwa mtu kama mwanajeshi. Ona sasa kafa vyeo kaviacha mke kamuacha na utakuta mwishoe aliwe na hao hao mabajaji waliomuua😂😂
 
Huyu lt col ilitakiwa avuliwe cheo kabla ya kuzikwa arudishwe kwenye umeja.

Amelitia hasara taifa kwa kukosa ueledi wa majukumu yake.

Amekufa kizembe sana kwa kutojitambua kwamba yeye ni kiongozi.

Malipo ya mjinga ni hasara
Kesi itakuwa kuua bila kukusudia bila kujali cheo. Kwa hio muuaji anaweza fungwa muda mfupi tu kama Lulu alivyomuua Kanumba au Ditopile dhidi ya dereva daladala
 
Wahuni wote wa Dar es salaam mjiandae kisawasawa.

Ewe mzazi kama unajua mwanao ni muhuni,
Mkanye na mwambie aache mara moja.

Kitakachomkuta hatokuja kusahau maisha yake yote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…