Updates za kifo cha Afande Luteni Kanali Muna aliyeuawa Kawe kwa kuchomwa kisu na dereva bajaji Kato

Jeshi halipaswi kabisa kujenga bifu na raia..
Vinginevyo kikinuka, raia wanaweza kuwa upande wa maadui kama ilivyotokea kwa jeshi la Uganda ambapo raia wengi wa Uganda walikuwa upande wa jeshi letu kutokana na kwamba walichoshwa na vitendo vya kionevu na ubabe vya UPDF ya kipindi hicho cha Hayati Alhaj Idd Amin Dada
 
Kuna umuhimu wa kupitia usajili wa kila boba boda Na Bajaji ndani ya hii nchi ili kila mmiliki ajulikane na hii itapelekea hiyo biashara kuwa ki professional.
Sasahivi udhibiti ni mdogo sana mtu amepata ela anagawa boda boda au Bajaji kwa mtu hajui nyumbani kwake hakuna dhamana yoyote imewekwa kwa lolote likitokea matokea yake wizi unaingizwa ndani yake .
Faini za awali ziliponguzwa zirudishwe ama sivyo madhara makubwa yataongezeka kwa watumiaji na abiria .
 
Badala ya kwenda kuwasaidia vita ya Ukrain au Wapalestina wao wanaanzisha vita na raia wema wasio na silaha. Siku za mbabe ni 39.5 na za mwizi ni 40
 
Mimi ngumi ni kitu cha mwisho kabisa hata kufikiria kurusha. Kuna watu hata gari kugusana tu tayari anashuka ngumi mkononi! Kuna watu hata humfikirii lakini ni hatari kwenye hand to hand unaweza kutia aibu na mwili wako.

Mpenda ugomvi yeyote ni vile hajakutana na kisiki kimnyooshe ndio ataanza kwenda taratibu na watu.
 
Nakazia.
 
Huko kazini Kwa Muna huenda walikuwa wanagombea hicho cheo kiasi cha kurogana.

Hivi ina raha gani kama hivyo mwenzio kafa wewe upewe hiyo nafasi yake Halafu utapata amani na furaha Kweli kwenye nafsi na moyo wako?
Labda iwapo dhamiri yako ilishakufaga! [emoji848][emoji848]
 
Asante kwa kuamua Kutenga muda wako Kulielimisha hilo Pumbavu la Milele Medecin ila usitegemee kama litakuelewa kwani Limerithi huo Upumbavu wa Milele unaomgharimu.
 
Japo kuna vitu vime ongezwa kwenye hii story lakini sawa, Mwisho wa siku Mwanajeshi kazi yake ni kifo japo tumekula hasara hajafia kazini. Nidhamu na Utii viwe mbele katika yote
 
Umeandika ukiwa na bia ngapi kichwani!??
 
Sawa sawa, mkuu
 
Haya mambo nasikiaga kama story tu. Bado huwa siamini unaweza ukawa umekaa zako ukaja ukaanza kupigwa kisa kuna mtu mwingine huko kafanya makosa..

Sasa kwa karne hii ya Technology, what if mtu akachukua video?? Kwa kweli sidhani kama ni kweli raia wanaweza kupigwa bila kosa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…